Mgagaa na Upwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2013
- 13,481
- 28,116
Bajeti iliyojenga barabara ya kwa msuguli -malamba mawili ndio hiyo hiyo ilikua ifike mpaka kwembe,king'azi,kifuru hadi kisarawe,ila jiwe alipokufa tu ile bajeti na yenyewe ikaenda mifukoni mwa wajanja,jiwe alikua mtu sana sema vzr avidumuKuna barabara waliweka hadi kibao cha kuanza ujenzi, lile bango limeshaanguka tayari. Serikali imejaa uhuni sana.
Sasa wewe ndio unaoajua vizuri mkuu, ni aibu mitaa hiyo.Hiyo ni kwembe,king'azi,malamba mawili,kibamba ni aibu maeneo hayo na serikali hauna hata habari,inafikiria kuomgeza v8 za ma rc!!
Tmk ilijiwahi kipindi cha jiwe,kama utakumbuka siku anazindua magu bus terminal aliongelea ujenzi wa barabara za wilaya ya ubungo na majimbo yake ubungo na kibamba,baada ya pale akuonekana tena hadharani hadi umauti wake,hawa waliokuwepo sasa hivi hawana time na maendeleo ya wananchiKitu ambachi sielewi why Temeke imefanikiwa kuwa na Lami vichochoroni. Ubungo Moja ya manispaa yenye ukwasi mkubwa imeshindwa wapi!?
Ipo pale pale mpigi magoe mwisho standard.Mpiji magoe Hospital gan au ile ya wilaya kule mabwepande?
Sisi tulishawahi tumewekeza biashara zetu vzr. Na maji yapo tumepata kutoka tanki la Tegeta A. Mtoa huu uzi aache kukatisha watu tamaa yeye akajenge Sinza au Kinondoni atuachie Msumi yetu. Maana hata Goba miaka ya 2012 ilikuwa worse no maji no umeme no barabara. New Msumi is coming!Kwa watu wanaojua nini wanafanya hawawezi ongea mambo ya kijinga kama discussion zilizomo humu ndani.
Vijana wengi wa kileo huwa wanafuata umeme na maji na barabara. Then wanaenda kuweka makazi kwenye 20×20 . Huu ni ujinga kwa watu wanaojielewa.
Watu wengi waliowahi maeneo msumi wamejenga kwenye maeneo yenye ukubwa wa sqm 2500. Manake nini, ardhi ya DSM inapanda thamani kila siku. SLOGAN ni hamia sehemu mji ndo ukufuate.
Usifuate mji. Wajanja wamenunua maeneo wamejenga hardware viwanda vya tofali nk. We kaanzishe kiwanda cha tofali sinza.
Kwa hizi akili za kufuata lami na maji ya bomba sijui kwenye suala la ardhi tutawaachia nini watoto wetu.
Kumbuka tabata ilikuwa pori na wengine waliogopa kununua kwani waliamini yalikuwa makazi ya wanyama wakali kama simba. Kunawazee wakikumbuka ujinga waliofanya wanalia machozi.
Uzi huu utunzwe vizuri kunawatu baada ya miaka 10 tu watalia machozi. Nami ngoja nikatafute eneo msumi litanifaa baadae
Waambie waelewe. Sehemu niliyowekeza mimi kuna maji kutoka Tegeta A. Upande uliobaki Maji yatafika na fomu walishajaza. Maendeleo yanakuja .Wakazi wa Msumi tujuane tafadhali!
Nimeishi huko mwaka wa 6 Sasa sijawahi jutia,..!!
Hivi mlitegemea serikali iweke maji kwenye ngedere,ijenge Barabara pasi watu kuwepo?
Punguzeni kukatisha Tamaa watu,Kuna jambo ukiliongelea watu tunajiuliza uwezo wako wa kufikiri.
Nimezaliwa kimara,hapakuwa na maji Wala Barabara baada ya muda tukapata.
Vivyo hivyo,sinza k/Koo,tabata,ubungo nk.
Hatuwezi kulala na kuamka kukuta Kila eneo Lina maji na Barabara bila kusahau umeme,MAENDELEO HATA YA NYUMBANI KWAKO HAYAJI KWA SIKU MOJA!
Sijui ni mtaa upi huo usio na mpangilio unaozungumzia.Hakuna mpangilio wa kimakazi
Huko na hiyo inacsababihwa
Na watu wenyewe
Ova
Mpiji magoe ni km 25 kutoka mbez Magufuli terminal to bunju B.
Asije akawa anatutega humoHatuna uhakika ni nini....ila baadhi ya maeneo kaweka uzio na wanyama.
Uvumilivu ni nguzo ya Kila kituKuna siku nipo pale Mbezi nikamsikia jamaa wa Bajaj anaitia ”Msumi na Bajaj buku nne” nikamwangaliaaa nikamuona hivi huyu anadhani hela watu wanaenda kuokota?nikaishia kumtukana kimoyo moyo.
Sema mkuu Msumi hata kama mateso yakizidi wokovu unakaribia ila nyie mnapata shida aisee,mtu anasubiri Eicher au DCM kwa dakika 45 inakuja anapanda halafu inaenda kuzimikia pale Mazulu au au njia panda Goba na hapo limekata spring au limetumbuka clutch na ni wazi kuendelea na safari itakuwa kesho lakini mnaendelea kuvumilia.
Hatari sana.
ShukranStand ya daladala mbezi mwisho ...ulizia magari ya Msumi.
Msumi iko Dar imepakana na Goba pamoja na Madale.Msumi ni Kibaha, Pwani.
Barabara ya mpiji magohe serikali inashughulika na kibamba mpiji magohe mpka iishe inajengwa kwa awamu. Mbezi mpiji magohe bado Sana maana kipande hiki kinahitaji fidia kubwa kwa wananchi katika kupanua barabara pia kipande hiki kinahitaji Madarajq zaidi ya matano hivyo inahitajika bajeti ya kutoshaBraba
Ya Mpigi magohe itajengwa pia kwenye huo mradi ?!