Hivi mtu anaweza kumwaga rough floor pasipo kuezeka?

Ndio Inawezekana, .., Mimi NILIFANYA HIVYO kabla sijaezeka kwa lengo la kupambana na mvua zitakazo sababisha Msingi kutitia..
HIVYO kwangu Mimi naona ni maamuzi sahihi Sana.
Mkuu una maana gani kupambana na mvua zinazosababisha msingi kutitia. Yaani, connection ya kuweka rough gloor na hilo ni ipi
 
Unaweza kumwaga Zege la Nchi 2 baada ya kushindilia vizuri, then baadaye ukaezeka...!

Ukija kupata pesa, huna haja ya rough floor, unaweka Tiles straight kutokea kwenye Floor yako ya Zege...!

Nimekushauri sio kama JF member tu, ila mimi ni Fundi.
 
Ndio hata mi najua hivi. Hao wanaomwaga jamvi soon after msingi nadhani ni wale wako na budget ya kutosha kujenga. Tunaojenga kidogo kidogo Jamvi huja baadae sana.

Kukujibu swali lako vipi ukichongesha hata madirisha labda? Au tafuta mahali wanapowekeza iwe kama umelipa advance ya bati.
 
Zege mbichi ikipigwa na jua kali inatengeneza nyufa kwa wingi kutokana na kupoteza maji mengi (volumentric ahrinkage)..ndio maana site huwa tunatumia magunia kufunika zege ili lisipoteze maji (angalau kupunguza hiyo effect)
 
Floor hutengenezwa kabla ya ukuta kuanza kujengwa
 
Wewe nawe jitafakali uliona mtoto anatembea bila kutambaaa? Unataka kuvuka step au??
 
Wewe nawe jitafakali uliona mtoto anatembea bila kutambaaa? Unataka kuvuka step au??
yah kuna watoto hawatambai wanatembea tu. Nimeuliza kwa sababu kuna nyumba zinapigwa rough floor zikiwa msingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…