Hivi mtu kuwa Cream inamaanisha kuwa na First Class au Upper Second?

mtabaki kubishana humu, mwisho wa siku advantages za wenye first na upper, huwezi kuzipinga re:tpdc, ulecturer, uprofesor lazima uwe uliperform ngazi ya degree

Hapo kwenye uprof nakukatalia, wapo maprof ambao hawakupata hizo GPA kama 1st na .2nd upper. Cha msingi ni kwamba wenye pass uwezo wao wa ku deliver ni mdogo compare na wenye GPA kubwa lakini wapo wachache wana uwezo mkubwa tu sema 5% to 10% coz hawakupata hizo GPA kwa kupenda, nadhani hawa wachache ndo mtoa maada anaazungumzia.
 
Kwa maoni yangu kuna wanaofaulu vizuri kwa haki cuz wao wana struggle pia kuna wale wa magumashi. But sio vizuri ku generalize kuwa first class na uppers wote ni hovyo!
Bora uwaambie mkuu, maana wabongo watu wakifaulu wanaongea na wakifeli wanaongea tuache mambo ya kijinga wabongo
 

Ok basi tufanye wenye pass na lower second ndio ma cream.
 
mtabaki kubishana humu, mwisho wa siku advantages za wenye first na upper, huwezi kuzipinga re:tpdc, ulecturer, uprofesor lazima uwe uliperform ngazi ya degree

Lakini mbona utendaji bado ni mbovu huko maofisi na vyuoni licha ya ufaulu wao "uliotukuka"?
 
aliyepata division 1.7 olevel na advance akapata division 1.3 A level lakini chuo akapata lower second huyu utasema sio cream. Kuna vyuo unaenda kuchukua first class na kuna vyuo unaenda kutafuta first class.

Well said brother...!
 

kuna waliopata marks mbaya advance but wakaenda SAUT,SIO kwamba ni wabaya but wengine wanapitia changamoto sana.Mimi kuna mshkaji wangu namkubali ni jembe but aliteleza kidogo A level kapata div 3 akasenda SAUT.
Matokeo sioni kama ni kitu sahihi cha ku judge u cream wa mtu. saa zingine kwenye maisha unahitaji bahati
 
wanafunzi kazaneni kusoma, fanya assignments zote kama individual, shiriki presentations, soma vitabu vingi kwa jinsi ya muda wako, shiriki discussion kidogo. fanya mitihani kwa uaminifu na umakini, hii itakusaidia kua mtaalam wa ulichosomea hata kama u hv a low gpa ( japo haiwezi tokea ktk hali ya kawaida). kua na gpa kubwa ni muhimu sana it makes you more competitive. All the best.
 
Mimi nadhani sasa ifike wakati hawa recruit agency wawe na mtazamo chanya?sasa hawa wenye GPA ndogo waende wapi maana siamini kama hawana skills za kutosha ninanvyojua mimi wapo wenye GPA kubwa halafu hawana skills ofis wao ni kujisikiaa tu wamesoma sana si tunawaona wao ni wameparfom ila perfomance hakuna ni vyeti tu...!
NB:naomba ieleweke huu ni mtazamo tu sio nawahukumu...ila na ww unaweza kutoa mchango wako....!:juggle::juggle:
 
Na hapa ndio wanafunzi wengi wa vyuo mnapojichanganya na kudanganyana eti oooh.. GPA haina maana.. We hebu jiweke kwenye nafasi ya muajiri, umepokea application 100 za watu ambao wote wana degree. Wewe unahitaji watu wawili. Utaangalia kigezo gani kuwachuja? Maana unapozungumzia performance maana yake ni lazma nikuajiri kwanza, nikupe kazi ndio ntajua performance yako!
Wanafunzi wa vyuo msijidanganye GPA ndio kigezo cha kwanza waajiri wengi wanachoangalia kutenganisha mchele na chuya.
 
hizi mada zinakera sana. mfano kwenye sector ya uhasibu kazi ya graduate GPA inahusika sana but ukiwa na CPA na gpa ya kawaida unafikiriwa kwanza. Na kwa kazi zinazohitaji uzoefu GPA na masters havina nafasi,kinachohitajika hapo ni uzoefu.
i am not perfect
 
Sidhan kama kuna jambo la kubishana au kudiscuss apo ili kubadili situation iliyopo...mi naamin yeyote anayetaka kukataa ukweli kwamba mwenye gpa kubwa ndo awe considered first, awe mwajiri yeye halafu aone kama ataweza kumchukua mwenye gpa ndogo na kumuacha mwenye gpa kubwa!! Graduate programs ni wazi waangalie gpa, na management positions/positions zinazohitaji uzoefu waangalie experience na performances. Dogma.
 
Nimeipenda sana hii post.kwanza kabisa GPA ni kigezo cha kwanza kwa employer yeyote ikiwa ni kama kutafuta someone who is qualified for specific job.then hii sio chuo tu ni kwa level zote za elimu kuwa aliyefaulu zaidi ndo mwenye akili zaidi no mattter ali cheat paper or not.kwaiyo hata kujiunga na elimu ya juu TCU huwa wanagrade zao.kwa upande wa waajiri wanaamini GPA kubwa ndo skills nzuri..vipi katika uhalisia.ukweli ni kuwa GPA kubwa sio skills ya kutosha maana wapo wenye ndogo na wanaperform kazi vizri tofauti na wenye GPA kubwa..lastly,ni vyema kupambana na kupata performance nzuri katika academic mana ndo mwanzo mzuri..
 
wanafunzi kazaneni kusoma,
fanya assignments zote kama
individual, shiriki presentations,
soma vitabu vingi kwa jinsi ya
muda wako, shiriki discussion
kidogo. fanya mitihani kwa
uaminifu na umakini, hii
itakusaidia kua mtaalam wa
ulichosomea hata kama u hv a
low gpa ( japo haiwezi tokea ktk
hali ya kawaida). kua na gpa
kubwa ni muhimu sana it makes
you more competitive. All the
best.
 
Basi ili uwe katika safe side, pata GPA kubwa. Kwani kuna tatizo gani ukipata GPA kubwa? Jamani, mbona tunapenda kutetea vitu vya ajabu? Hebu pendekeza sasa, umepewa watu 50 usiowajua, unatakiwa uwapate watu watatu, wewe ungefanyaje? Wakisema kigezo cha uzoefu, mnalalamika eti vijana waliograduate watakosa sifa, wakisema kigezo cha GPA mnalalamika eti GPA kubwa sio uchapakazi, wakisema toeni mawazo yenu kigezo gani kitumike, hamtoi mawazo, mnaishia kulalamika tu! Sasa unalalamika bila kutoa mawazo, huoni wewe hauna mchango wowote katika jamii?
 
GPA sio kigezo kikubwa lakini ni wazi kuwa mtu mwenye GPA kubwa ana advantage zaidi ingawa vigezo vingine vinazingatiwa pia!
 
Mm naamini GPA can or can not be the issue kwani mm nakumbuka nilimaliza chuo na GPA ya kawaida na ninawajua wengi tu walokua na GPA za kawaida they got the job.issue itategemea muajiri anataka nn ajira za ckuhizi ni challenge sana hazitabiriki.soma fanya vizuri kama wajibu lkn isikupe kiburi na uhakika GPA yako
 
Chuoni kuna mijitu huwa inaendekeza discussions..kitu kidogo tu kinasumbua utasikia"twendeni kwenye kimbweta"..ni lini utajifunza to stand on your own?..matokeo yake mtu anashindwa kuja kuwa muamuzi mzuri ata wa masuala ya msingi ya maisha yake...guys, we gotta learn to be independent in some circumstances..thanks!
 

Well said fellow!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…