Hivi ndivyo hela zilivyopigwa kwenye Bohari ya Madawa

Hivi ndivyo hela zilivyopigwa kwenye Bohari ya Madawa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ni kwa Mujibu wa CAG

Screenshot_2024-04-17-00-21-56-1.png

"Nilibaini kuwa Bohari Kuu ya Dawa ilinunua mashine 10 za kuondoa maumivu, ukakamavu na mkazo wa misuli (Diathermy) kwa bei ya shilingi milioni 136.7 na kuacha kununua vifaa hivi kwa mzabuni aliyebainika kuwa na bei ndogo wakati wa ushindani ya shilingi milioni 103.2 hivyo kupelekea gharama za ziada ambazo zingeweza kuepukika za kiasi cha shilingi milioni 33.5" -Kichere

"Vilevile nilibaini ununuzi wa vifaatiba kwa wazabuni 32 waliopewa zabuni zenye thamani ya shilingi bilioni 4.14 bila kufanyiwa uchambuzi wa awali na kuidhinishwa na bodi ya zabuni, pia vifaatiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 13.37 ambavyo ununuzi wake haukuwa umeanza.

Pia nilibaini uchelewaji wa ununuzi na usambazaji wa vifaatiba katika vituo vya afya kwa siku zinazoanzia 23 hadi 1,458 tangu fedha zilipopokelewa na Bohari Kuu ya Dawa hadi vifaatiba vilipofika kwenye vituo vya afya, pia vituo 21 vya afya vilipokea vifaa vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.68 ambavyo vilikuwa havijaanza kutumika" -Kichere

CAG Charles Kichere amezungumza hayo alipokutana na wanahabari Aprili 15.2024
 
Hii ni kwa Mujibu wa CAG

View attachment 2965842
"Nilibaini kuwa Bohari Kuu ya Dawa ilinunua mashine 10 za kuondoa maumivu, ukakamavu na mkazo wa misuli (Diathermy)

Bil 20 mbona ndogo. Yale mashangingi ya Bil 190 vipi

Kuna ipigagi pia, na yale mandege ya JPM na samia vipi !

Ofisi ya CAG nayo inatumia hela sana kufanya ukaguzi usio na tija wala impact kwenye jamii. CAG imekuwa ni chombo cha habari, yeye anakaguliwa na nani ? Kuna matumizi makubwa ya hela kwenye kukamilisha kaguzi zake
 
Bil 20 mbona ndogo. Yale mashangingi ya Bil 190 vipi

Kuna ipigagi pia, na yale mandege ya JPM na samia vipi !

Ofisi ya CAG nayo inatumia hela sana kufanya ukaguzi usio na tija wala impact kwenye jamii. CAG imekuwa ni chombo cha habari, yeye anakaguliwa na nani ? Kuna matumizi makubwa ya hela kwenye kukamilisha kaguzi zake
Hoja yako ni ipi , waendelee kula au asikague ?
 
Kilichoandikwa kwenye heading ni Billion.

Ukisoma taarifa yenyewe ni Millioni, kipi ni sahihi wewe mleta mada.

Kaguzi za namna hii hazina Tija hata kidogo, sheria ya manunuzi ndio shida, wasilaumu hao MSD.
 
Hao wanaokula mapesa hayo ndio wanasifia sifia na kumshukuru rais kwa sababu wanaweza kuiba pesa na wasichukuliwe hatua.
 
Hoja yako ni ipi , waendelee kula au asikague ?

Anapoteza muda. Kuna mtu yoyote umesikia amewahi kuchukuliwa hatua ?

Na yeye pia tujue anakaguliwa na nani, kuna matumizi makubwa sana ya pesa kwenye ofisi ya CAG na ikulu. Ni Nani anaehusika kukagua huko

It is for public interest iwekwe wazi, ofisi ya Rais na Mkaguzi wote ni watumishi

Je sheria ya uhakiki wa Mali za umma una maeneo hawatakiwi kugusa?

Nyuzi kama hizi ni kufutilia mbali, hazina tija

Sitak kusikua ishu yoyote ya CAG , yale mandege ya JPM na Samia, ni another failure kwenye Taifa hilo la Tanzania, na hakuna waliowajibishwa, DP world ni another failure kwenye taifa, mnatafuta viofisi kama MSD visivyokuwa na mbele wala nyuma kuwashushia mzigo
 
Bil 20 mbona ndogo. Yale mashangingi ya Bil 190 vipi

Kuna ipigagi pia, na yale mandege ya JPM na samia vipi !

Ofisi ya CAG nayo inatumia hela sana kufanya ukaguzi usio na tija wala impact kwenye jamii. CAG imekuwa ni chombo cha habari, yeye anakaguliwa na nani ? Kuna matumizi makubwa ya hela kwenye kukamilisha kaguzi zake
Kazi yake ni kuimba ngonjera kila mwaka,mafisadi wapo juu ya sheria
 
Anapoteza muda. Kuna mtu yoyote umesikia amewahi kuchukuliwa hatua ?

Na yeye pia tujue anakaguliwa na nani, kuna matumizi makubwa sana ya pesa kwenye ofisi ya CAG na ikulu. Ni Nani anaehusika kukagua huko

It is for public interest iwekwe wazi, ofisi ya Rais na Mkaguzi wote ni watumishi

Je sheria ya uhakiki wa Mali za umma una maeneo hawatakiwi kugusa?

Nyuzi kama hizi ni kufutilia mbali, hazina tija

Sitak kusikua ishu yoyote ya CAG , yale mandege ya JPM na Samia, ni another failure kwenye Taifa hilo la Tanzania, na hakuna waliowajibishwa, DP world ni another failure kwenye taifa, mnatafuta viofisi kama MSD visivyokuwa na mbele wala nyuma kuwashushia mzigo
Usikate tamaa
 
Back
Top Bottom