Hivi ndivyo mmoja kati ya wanafunzi wa kidato cha 4 alivyojibu mtihan wake wa kiswahili.

Hivi ndivyo mmoja kati ya wanafunzi wa kidato cha 4 alivyojibu mtihan wake wa kiswahili.

Huyo mwl. mnae mlaumu kua amefelisha mnataka afanyaje kama anapokea mwanafunzi alie maliza drs la7 kwa kuanza kidato cha kwanza akiwa hajui kusoma wala kuandika. Mwl. huyo afanye kazi ngapi?
Shule za msingi walifuta baadhi ya masomo nakuanzisha somo jipya la TEHAMA, walimu wakufundisha somo hilo hawakuweko unategemea nin hapo?
 
'Ukigombana na mpishi lazima utakula chakula kibichi.' Ni matokea ya kutoelewana baina ya mwl. na siri_kali
 
'Ukigombana na mpishi lazima utakula chakula kibichi.'
Ni matokea ya kutoelewana baina ya mwl. na siri_kali
 
mimi nafikiri ya kuwa huyu kijana anajua kuwa mdahalo katika lugha ya kwao ni dawa fulani ya kienyeji na ndio maana aliezea hatua za kuandaa kwa stahili hiyo
 
mimi nafikiri ya kuwa huyu kijana anajua kuwa mdahalo katika lugha ya kwao ni dawa fulani ya kienyeji na ndio maana aliezea hatua za kuandaa kwa stahili hiyo

Kwa stahili hii inabidi pepa zikisaishwa warudishiwe wazaz wa wanafunzi
 
lakini kama alikuwa haelewi au hajui hata huo mdahalo wenyewe ni nini kosa ni la nani?? pengine yeye hajawahi hata kusikia mdahalo ni kitu gani na kwa akili yake ya haraka haraka (unajua tena ukiwa kwenye pepa) na jinsi swali lilivyoulizwa (hatua za KUANDAA mdahalo) akajua pengine ni kitu kama chakula hivi...mi kwa upande mwingine simlaumu..inawezekana hakuwahi kabisa kufundshwa/kusikia kitu kinaitwa mdahalo! kuongea kiswahili si kujua kiswahili mkuu!!

Huenda huko kwao kuna chakula kinaitwa mdahalo
 
mkuu sidhani kama mwalimu anapaswa kubeba lawana kutokana na huyu mwanafunzi alivyojibu,tatizo la wanafunzi wa siku hizi wanakariri sana kiasi kwamba wakibadilishia kitu kidogo tu kwenye swali alilowahi kulisolve unakuwa umempoteza kabisa,pia siku chache kabla ya mitihani hulishana sana matango pori


Umenena sawa mkuu
 
SWALI:- Eleza hatua za kuandaa MDAHALO.
Akiwa hajui maana ya mdahalo akajibu hivi-

KWANZA; unachukua mdahalo wako unauosha vizuri.

PILI; hakikisha mdahalo wako haujakomaa sana.

TATU ; bandika sufuria yako jikoni mkali kiasi.

NNE ; weka mdahalo wako jikoni kisha uache uchemke kwa dakika kumi hadi kumi tano .

TANO; mdahalo wako ukiwa tayari uepue.

SITA; mdahalo huu unaweza kunywa na kinywaji chochote...

@copy&paste#..

Huyu inaonesha ni msikilizaji mzuri wa vipindi vya maakuli vya Radio Free Afrika vinavyoendeshwa na Glory Robinson.Staili aliyoitumia ni hiyo hiyo.
 
mimi nafikiri ya kuwa huyu
kijana anajua kuwa mdahalo katika lugha ya kwao ni dawa fulani ya
kienyeji na ndio maana aliezea hatua za kuandaa kwa stahili hiyo

Yaweza kuwa hvyo mkuu,kwani hata alivyoelezea ha2a za kuuandaa had ukamilike amejitahd,labda angetafutwa aulizwe alielewaje swali.
 
kajitahidi sana maana kajibu kama alivoelewa swali unaandaaje mdahalo hili lazima litakuwa neno kwa kilugha ni msosi si bure..
 
lakini kama alikuwa haelewi au hajui hata huo mdahalo wenyewe ni nini kosa ni la nani?? pengine yeye hajawahi hata kusikia mdahalo ni kitu gani na kwa akili yake ya haraka haraka (unajua tena ukiwa kwenye pepa) na jinsi swali lilivyoulizwa (hatua za KUANDAA mdahalo) akajua pengine ni kitu kama chakula hivi...mi kwa upande mwingine simlaumu..inawezekana hakuwahi kabisa kufundshwa/kusikia kitu kinaitwa mdahalo! kuongea kiswahili si kujua kiswahili mkuu!!
huwezi ukafundishwa kilakitu na hapo ndo juhudi binafsi na akili ya kujiongeza inapotakiwa.

Kwa jinsi alivyojibu UWEZO ANAO!
tatizo ni kwamba hakufundishwa!
Hajui nini maana ya mdahalo!
Lawama zinawaendea waliopewa dhamana ya kumfundisha!
 
huwezi ukafundishwa kilakitu na hapo ndo juhudi binafsi na akili ya kujiongeza inapotakiwa.
ila kumbuka juhudi binafsi na akili zinategemea sana mazingira aliyonayo mwanafunzi shuleni, na kuna vitu vingine hata uwe geneus kias gani huwezi vijua kama hujawahi sikia, soma au kufundishwa mahali flani..huviwezi kuja tu automatically la sivyo hawa wanaoitwa ma geneous wangekuwa hawaendi darasani kabisaaa!!
 
huwezi ukafundishwa kilakitu na hapo ndo juhudi binafsi na akili ya kujiongeza inapotakiwa.

Wanafundishwa wanaokaa darasani tu!
Mtu chimbo,shule anaonekana kwa nadra,akishindwa kuandaa mdahalo alaumiwe mwl!
 
Huyu inaonesha ni msikilizaji mzuri wa vipindi vya maakuli vya Radio Free Afrika vinavyoendeshwa na Glory Robinson.Staili aliyoitumia ni hiyo hiyo.

Itabidi serikali itafute masomo mengine yafundishwe na radio kama wanaelewa zaidi wakazisikiliza.
 
Mh!Jamani ifike wakati NECTA wasahihishe kulingana na mawazo ya mutu.Pengine huyo binti yuko sahihi kwa mawazo yake
 
Back
Top Bottom