ibanezafrica
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,261
- 6,553
Hivi punde nimesikia kutoka radio moja kipindi cha michezo kuwa Simba imekuwa ikifanya vibaya katika michezo yake hasa ile ya kimataifa moja ya sababu eti ni vile hawana kocha msaidizi, sasa wamepanga na wameshamalizana na kocha wa KMC wanamchukua wao
Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo hapa Mbeya City walikuja vizuri sana katika soka watu tukafurahi kwa timu hii ya mkoani kuzipa challenge kubwa timu kubwa, kilichofuatia Yanga wakamchukua kocha wao! Timu ikapotea hadi leo
Hivyo hivyo tumeshuhudia wachezaji wengi wazuri wanaoibukia timu changa na kuzisaidia wanarubuniwa kuja kuzichezea hizi timu za Simba na Yanga na mwisho wengi wao wanapotea. Tushukuru tu akina Samatta na Ulimwengu hawakua na muda sana ndani ya timu hizi vinginevyo ndio ingekua basi
Kiukweli timu hizi hazina jipya na kuendelea kwake ni ndoto, kwanza hazina weledi wa kutafuta wachezaji wenye viwango ndio maana wana ng'ang'ania wachezaji wazee walio expire miaka mingi. Vipi unategemea wachezaji kama Okwi, Ngasa, Boban?
Kikubwa serikali izifute klabu hizi mbili zipo hapo kwa manufaa ya baadhi ya watu kujaza matumbo na kuua kiwango cha soka nchini timu hazina vision ya kwenda mbali kimataifa,serikali tuondoleni timu hizi kabisa zifutwe,iwekwe mikakati ya kutengeneza kizazi kipya tutafika mbali hakika.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo hapa Mbeya City walikuja vizuri sana katika soka watu tukafurahi kwa timu hii ya mkoani kuzipa challenge kubwa timu kubwa, kilichofuatia Yanga wakamchukua kocha wao! Timu ikapotea hadi leo
Hivyo hivyo tumeshuhudia wachezaji wengi wazuri wanaoibukia timu changa na kuzisaidia wanarubuniwa kuja kuzichezea hizi timu za Simba na Yanga na mwisho wengi wao wanapotea. Tushukuru tu akina Samatta na Ulimwengu hawakua na muda sana ndani ya timu hizi vinginevyo ndio ingekua basi
Kiukweli timu hizi hazina jipya na kuendelea kwake ni ndoto, kwanza hazina weledi wa kutafuta wachezaji wenye viwango ndio maana wana ng'ang'ania wachezaji wazee walio expire miaka mingi. Vipi unategemea wachezaji kama Okwi, Ngasa, Boban?
Kikubwa serikali izifute klabu hizi mbili zipo hapo kwa manufaa ya baadhi ya watu kujaza matumbo na kuua kiwango cha soka nchini timu hazina vision ya kwenda mbali kimataifa,serikali tuondoleni timu hizi kabisa zifutwe,iwekwe mikakati ya kutengeneza kizazi kipya tutafika mbali hakika.
Sent using Jamii Forums mobile app