Hivi ndivyo tunavocheat, palipo na viatu vya muwewe kuna ndala zangu

Hivi ndivyo tunavocheat, palipo na viatu vya muwewe kuna ndala zangu

Salaam wadau,


Maisha yanatupa zoefu nyingi sana, zenye matokeo chanya na wakati mwingine zinaweza kukuachia alama ya uchungu isiyosahaulika. Mara nyingi sio kwa kupenda au kuridhia maisha automatically yanakupa darasa. Hiki ni kisa Cha ukweli.

Nitajaribu kuweka wazi mambo magumu ili upate picha japo kwa kusoma. Nikusihi tu soma na chukua machache kwajili ya kuboresha mahusiano Yako. Wala usinijaji kwa yaliotokea maana huko nilishatoka 6 years back na sijutii. Toba ilishamaliza kila kitu. Twende kazi.

Miezi miwili tu baada ya kumaliza elimu ya juu nipo home mark timing ndio nakutana na aliyefanya niandike huu Uzi. Tulikutana dukani mtaa Mmoja, wakati Mimi nafika yeye alikua akisubiri chenji/chenchi yake. Muuzaji alitoka kidogo ikabidi nimuulize yeye sasa. "Habari Yako, huyu yupo wapi ?". Akanijibu. " ametoka kidogo kufata chenchi anarudi sasahivi". Hili duka lilikua ndani ya mji wa mtu, unaelewa sikuhizi unajenga nyumba Yako na frame kadhaa mbele yake. Ndivo ilivokua.

Mimi sikuona Haya kuanzisha stori nae ili kubuy time. Mimi " sorry wewe ni mwenyeji huu mtaa ?" Huyu dada naomba tumuite Recho. Akanijibu "Ndio mi nikaa hapo tu jirani, na wewe ?". Mimi "Me pia nyumba ya tatu kutoka hapa". Recho " ooh! Kumbe tupo jirani... sasa mbona Mimi sijawahi kukuona na kwangu we ni mgeni kabisa". Nikamjibu Hilo swali kuwa na Mimi nilitaka nimuulize nivile tu kaniwai. Huku ukweli nikwamba ni kweli sio mkaaji sababu ya shule. Basi muuzaji alirudi na akampa chenchi yule dada akarudia nyuma kunipa nafasi nihudumiwe lakini hakuondoka nikama alikua akisoma sms kwenye simu yake.


Wadau mwanamke udhaifu wake upo masikioni. Maana yake ni unaweza athiri namna yake ya kufikiri kwa kupenyeza maneno matamu kwenye sikio lake. Lakini kwetu wanaume Macho ndio weakpoint. Kutaamani kunaanzia kwenye kuona. Binafsi nilimtamani yule dada. Why ? alikua amevaa tight ndefu ya grey, t-shirt ambayo kwake ni oversize chini kabisa kaua na kikuku Cha chain mguu mmoja. Shape na muonekano mzima of course alinivutia japo sijamuelezea kwa 100% maana sio dhima yangu ya msingi ingawa kama ungeiona picha yake insta naamini ungegusa kwenye kuview profile.

Bila kujua au kujali sikumpa tena attention kwani niliamini anaondoka lakini nilishangazwa na kitu. Nilisikia... " jirani me naondoka", nikama 30sec zilikatika toka anipishe nipate hudumu. Nikageuka chap naona ni kweli anashuka ngazi. Nikamwambia " sawa jirani tutaonana tena". Nilichonotice ni kama Recho alitarajia ninge endeleza maongezi sorts of maswali na hatimaye tubadilishane namba. Ukweli ni alikua sahihi lakini nilikaza tu maksudi maana niliamini kama ni jirani kweli na anakaa pale aliponionesha kwa kidole basi tungekutana mara nyingi zaidi maana nipo home sasa.

Kimsingi nilikua nimefunga zipu yangu kwa miezi kama mitatu hivi au ziaid hivyo nilikua hyper flani hivi. Hapa niweke kitu clear. Notion iliojengeka kichwani mwangu ni, mwanamke ambaye Anableach...anavaa vikuku...anatattoo. Iwe ni ana kimoja kati ya hivyo au vyote kwa pamoja ni Wanawake ambao wapo beyond the limits. Yaani kama kaolewa au anamtu kucheat sio issue na mambo ya bata hasa sex ndio issue zinawapa fantasy sana. Na hio Haina uhusiano na elimu yake . Super woman chukua hioo itakuaaidia. So niliamini tu hapa nitapiga hata iweje. Niliweka nia lazima nitamtafuta tu.

Kesho yake mida ya saa 5 asubuhi nilipita jirani kabisa na Ile nyumba na ilikuwa na fence. Kichwani nikawaza nigonge geti au nikaushe naona shetani akawini. Nikagonga geti, baada ya muda kidogo likafunguliwa. Aisee ni yeye Recho kafungua. " Jamani jirani umepajuaje hapa. Heeh! Karibu kumbe kweli wewe ni mwenyeji". Mimi " Jana baada ya kunionesha tayari nikajua ni nyumba gani haswaa" mara kidogo nyuma yake akafata mtoto mdogo wa kiume kama miake 4+. Sikuuliza lakini alinambia "Oh! Mwanangu huyu jirani, haya karibu basi ndani."

Kaka mkubwa niliingia Ndani, Moja kati ya very high risks nimewahi kufanya ni hii. Kuingia ndani ya mji wa mtu pasina kujua kaolewa au lah na kama kaolewa mwenye mke yupo ndani, katoka au utarudi muda gani... Leo tuishie hapa then kesho tujue yalionikuta, inshallah tunaendelea.
malizia
 
Salaam wadau,

Tuendelee na EP 03

Saa 3 usiku nipo getini kwake tayari nasubiri kufunguliwa. Haikuchua muda akafika maana nilimjulisha nipo nje. Zana niliiweka mfuko wa nyuma wa suruali yangu ya cadet, hakika nilidhamiria kumlala Recho. " Karibu! Huogopi usiku huu kulivotulia na kiza hiki". Alinipokea kwa Hilo swali. Mimi " Kwasababu Yako tu sijajali kama ni usiku au lah!..nilikuahidi ningekuja kukuona kabla hujalala. Ndio hivi nimetimiza." Recho " mnh! Jamani.. haya ahsante kwa kujali jirani."
Tuliingia sitting room na kweli mezani pale nilikuta mzinga wa konyagi ndogo, krest na glass mbili. Moja ikiwa robo na Ile ya pili tupu. Recho "Karibu, kwanza umeshakula...hio glass hapo ni kwajili yako au Z wewe si mnywaji?".
Sasa ukweli Mimi si mnywaji kabisa, hapa nilitafuta namna ya kupapatua ili nisiharibu flow. Mimi " Leo alcohol hapana nimemalizia dozi ya vitonda vya tumbo ulcers leo mchana..ila kama kuna Sprite naomba".


Recho hakuwa kalewa ingawa ule mzinga ulikua unakaribia nusu ya ujazo. Nafikiri alikua anachanganya ki' cocktails flani hivi. Mimi nikaanza na Sprite yangu pale kisha stori zikaanza. Tuliongea kanakwamba tunafahamiana miaka kadhaa nyuma. Hapo ndio akanifahamisha ana jamaa na yupo kwenye ndoa halali, mwaka wa nne na kwa wakati ule mkuu wa kaya alikua nje ya bara la Africa kimasomo.

Sasa inaenda saa 5 kasoro usiku, na ukumbuke nina condom mfuko wa nyuma na mbaya zaidi nimeshadhamiria kumla. Hio haitoshi nimeshathibitishiwa usalama wangu kuwa mwenye mali hayupo, hapo nikarelax kabisa.


Recho "Nahisi joto nisubiri nikaoge... kwani unawahi home?". Mimi "hapana leo nipo lonely tu ... hakuna mtu home". Recho "Ooh! basi ngoja nikafunge na geti ulale tu hapa... Kuna chumba cha wageni". Nikajifanya nafikiria kitu kwa sekunde kadhaa kisha nikamjibu, " Ok poa ila nafikiri pia nikaoge nipumzike tu".
Mpaka hapo tayari niliona nipo kwenye nafasi nzuri. Recho alitoka nje kufunga geti na wakati huo nawaza nalalaje chumba cha wageni pekeyangu.


Alivorudi ndani wakati anafunga mlango kuingia sitting room nikasema liwalo na liwe. Nilienda mpaka pale kwake akiwa wima huku kanipa mgongo kisha nikapitisha mikono yangu usawa wa nyonga zake. Recho huku akigeuka " Ushhh! Z acha...umenistua . Mimi "relax, sitaki u feel upweke tena." Palepale breki zikafeli tukaanza kulana mate. Lakini Kuna jambo aliniuliza katika hali ya mshtuko kidogo. " Una condom?". Chap nikamjibu, "Ndio..ninazo".

Hapo hapo mambo yakabadilika. Recho akatoka kwa jazba flani kuelekea sitting room kisha akakaa. Na pupa zangu nikamfata nyuma harakaharaka walau nijue nini mbaya.


"Kwahio umekuja kwangu ili unit*mbe...mpaka condom umekuja nazo kweli Z kweliii unaona ni sawa?" Alitamka hayo maneno katika hali ya ukali. Kwanza kidogo nicheke ila nikakaza tu. " Hapana, sio kama ulivotafsiri...Sina maana mbaya kabisa." Nikaendelea huku nikisogea pale alipokaa na kushika nywele zake. " Mimi ni mwanaume, ni utaratibu tu nimejiwekea wa kuwa na protection popote ninapo kuwa...sina maana mbaya Recho".


Alionesha kushawishika na jibu langu lakini hakujibu kitu zaidi ya kuondoka kuelekea vyumbani. Nilibaki sitting room nashushia Sprite na baada ya dakika kama 15 au 20 ikaingia meseji. "Njoo chumba kinachowaka taa". Nilisimama kwa uharaka nikafata maelekezo. Hapo sasa dula chini huku nikama akastuka kutoka usingizini.

Nimezama ndani nikarudishia mlango, macho yangu mbele namuona Recho yu bed pekeyake akiwa kavaa pajama la kulalia. Nikamuliza dogo yupo wapi, akajibu hua alilinaye ana chumba chacke.

Kufupisha habari, nilifanikisha nia yangu ovu. Sio uongo ule usiku ulikua wa pambano zito. Nina miezi 3 kavuu, Recho sijui lakini kwa ushirikiano nilioupata nidhahiri Recho alikua na njaa zaidi yangu. Ajabu ni, zana ilitumika round ya kwanza pekee. Round zilizofata hata Mimi ukiniuliza ilikuaje for sure Sina majibu.

Tulichokifanya huu usiku naweza kusema ndio chanzo Cha yote yalioendelea. Na kwanzia hapo rasmi tukawa wapenzi, ingawa ulikua ni wizi/cheating lakini hakuna aliyejali hilo.

Nilijifunza kitu hapa, mwanamke akikuvulia nguo deliberately/kwa kuridhia basi amini tayari umechukua nafasi kwenye moyo wake au tuseme maisha yake hata pasipo yeye kutamka wazi. Rudia hapo kwa kuridhia na sio kwa kumbaka au kutumia madawa ya kumlevya. Haijalishi ni mara Moja au mbili then akakata mawasiliano. Ukikaza kumtafuta basi kumla kwa mara nyingine ni rahisi sana.

Hapa nakubaliana na wanaosema mpenzi wako akicheat basi likehood ya kukucheat tena ni kubwa hasa na yule yule mwamba. Na hii ndio maana nyuma ya jina la Uzi PALIPO NA VIATU VYA MUMEWE KUNA NDALA ZANGU yaani tofauti yangu na bwana mkubwa ni uwezo kimaisha na umri tu lakini kuhusu mwanamke tunateleza sehemu moja.


Kumepambazuka. Nashtuka nawai simu kucheck muda ni saa 12 lakini nipo mwenyewe kitandani. Recho yupo wapi ?
 
Karibu sana.
Mkuu naona kupitia hii story yako umetilia mkazo swala la kuoa bikra na kutoa straight red card (Without VAR consideration) kwa mwanamke aki cheat

Me naendelea kujifunza mkuu
Kaka tusiwe waumini sana wa kuacha wapenzi simply kacheat. Utaacha wangapi kaka maana Kwa uzoefu mdogo tu nilioupata kucheat ni inevitable kwa jinsi zote. Kikubwa muueleze ukweli mwanamke wako juu ya athari za kucheat walau aone haya kufanya hivo. Wakati huohuo nawewe punguza au achakabisa kucheat.
 
Karibu sana.

Kaka tusiwe waumini sana wa kuacha wapenzi simply kacheat. Utaacha wangapi kaka maana Kwa uzoefu mdogo tu nilioupata kucheat ni inevitable kwa jinsi zote. Kikubwa muueleze ukweli mwanamke wako juu ya athari za kucheat walau aone haya kufanya hivo. Wakati huohuo nawewe punguza au achakabisa kucheat.
Duh,bro una moyo mgumu sana
 
Back
Top Bottom