Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Duh kaka umepania😂 ,hadi na kapicha kake kabisafanya kweli na kapicha kake
Nimepania kaka, kama ni kanda ya ziwa itapendeza..Duh kaka umepania😂 ,hadi na kapicha kake kabisa
Ama kweli uandishi ni kipaji,ni kitu gani umeandika hapa mkuu maana hakuna lolote la msingi zaidi ya muuza maziwa mara cherehani 🤣Kuna uzi humu niliwahi eleza kisa chote nimesahau heading ilikuwa inasomekaje.
Yule demu alikuwa muuza maziwa pia alikuwa msabato. Hapo kitaa wahuni walikuwa wamejaribu kila njia lkn akawachomolea iwe hela bado kwao ilikuwa ngumu sana.
Baada ya muda nikaweka uteja kupitia mama yake na wamama wengine wauza maziwa sikuwa na mazoea na binti yyte pale.
lengo lilikuwa kumnasa yule binti.kwanza alikuwa mzuri sana na amepanda juu yaani tunalingana urefu futi5 cm kadhaa....
Nikabahatika kumteka mama yake kiheshima huku yeye ni salam tu na alikuwa na nidhamu kubwa sana.
Mama yake alipojaa kwenye mfumo basi siku mama asipokuwepo nitajifanya kusitikika kabisa.
kufupisha.....baada ya siku kadhaa nikaanza kumwingia kuwa anipelekee maziwa geto yaani awe ananiletea hata kama sipo anaweka tu getoikawa hivyo yeye hata mama yake .
Nilikuwa wakala kipindi hicho wa bank kadhaa hivyo nilikuwa na kawaida ya kuomba note za buku kiasi hata cha laki2 mpya. nikamuonyesha kuwa hela yako uwe unachukua hpa hapaswi kupajua mtu mwingine tofauti nawewe akakubali.
pia nikamwambia issue yoyote ya hela inayomuhusu awe anachukua hata bila kuomba ukumbuke hakuwa na simu. Mara kladhaa alikuwa anatumia ya mama yake.
Siku zikaenda mazoea yalishakorea sasa na nilikuwa hadi namsindikiza kwenda kwao hata mama pia.
kuna siku mama yake alileta maziwa geto siku hiyo alipofika mvua kubwa ikaanza nyesha mle geto hapakuwa hata na kiti nikamuomba ake kwa godoro akagoma badae akakubali mimi nkakalia ndoo. badae maza ake alienda mida kama ya saa2 hivi usiku biashara ishadoda.
Siku moja demu huyu alikuja nikamshawishi anipikie ukumbuke kule maziwa kaachia watu tu kumshikia wanauza ya kwao tu hadi saa2 mzigo uko vilevile . tukapita hoteli moja nilikuwa napenda kula pale hata mama nilikuwa nampeleka kula hapo nikawaambia leo biashara imegoma naomba nikuuzie haya maziwa kwa sababu wewe una firiji nakuuzia kwa bei ya ofaa akakubali tukauuza halafu helailiyopelea nikafidia.
hapo sijawahi mwambia nampenda wala nini hata hela aliwahi chukukua3000 tu.Mama yake alinikubali hadi akawa ananiletea nyama ama kuku wa kuchinja muda mwingine mahindi mabichi nachemsha kuchoma.
Baada ya kumuweka kiganjani mama yake hofu kubwa ikaja iwapo mama atajua hii ya mwanae ataniona wa ovyo sana.Siku moja nilijifanya naumwa ili aje tu kweli akaja ilikuwa siku ya sabato akaaga anenda kusali kanisa jirani walikuwa sijui na kusanyiko sijui wanafunga makambi whatever. siku hiyo ndo nikashinda nae alivaa nguo zangu kwa kuniomba nimpishe abadiri nikakataa sana badae nikakubali akavaa alifua hadi boxer mashuka nakupika nk.
Siku hiyo ndo nilimwambia kuwa namuhitaji akaniambia niende kwao hapohapo akasema ameshachumbiwa na wazazi hawatakubali niolewe mara2 iliniuma sana nikakumbuka hela zangu muda wa kumpeleka kwao kumbe ananichora tu.
Aisee japo yeye hakuona reaction yangu nikamwambia nami najua mzuri kama wewe huwezi baki bila kuwa na mme ama mahusiano. Basi katika story akaniambia hajawahi kusex kabisa....siku hiyo alienda .....
Dada yake aliuguliwa katoto akalazwa na akaombwa aende kwa dadake.Hivyo mama yake ndo alikuwa anakuja kuuza maziwa sisi tunapeleka chakula jioni hospital baada ya mimi kutoka job. hakuna aliyejua na dada yake alijua mi ni Dr Tu maana nilikuwa na koti lasuti jeupe na miwani ya kuzugia nilikuwa nikiingi wodini. nasalimia karibia kila mgonjwa (mtoto).
Hivyo dadake hakuhisi kitu chochote hata kujua tu tunafahamiana na mdogo wake.
Mama yake kuna siku alinambia nimtafutie sehemu ya kushona cherehani hii ilikuwa oda kutoka kwa jamaa na mama alinambia ndo nikajua kweli kaolewa kumbe......
Uzuri jirani ya ofisi yangu ya uwakala alikuwepo dada mmoja alikuwa anashona na anavitambaa nilimwambia akakubali mama nikamwambia aje kwanza apaone na amjue yule dada kabla ya kuja kuanza kazi ikawa hivyo...
Jamaa alimuuliza demu anapenda nn ili akija home amfungulie demu akasema kushona ndo akatoa go ahead hii..
Nilibahtika kumla huyu demu na kweli alikuwa silidi. Penzi likakolea sasa kuna siku sasa akaja akalala kabisa maana nilimuhakikisha nitamuoa yeye aangalie uwezekano wa kumuacha jamaa tu.
Sasa nahisi hata mama alihisi kitu lakini kwa nidhamu yangu hakuhofu. ilifikia hatua nikampa ufuguo wa geto maana kushona akawa hataki tena hivyo akifika ananiaga tu kuwa akija dada(mama ) fundi cherehani nimwambie anaumwa amerudi nyumbani. ukumbuke simu ya mama yake anayo kwahiyo akifika geto anapika anadeki na nilikuwa xmart tecno nikampa hivyo kazi yangu nikumuunga bando na kumwambia ingia youtube search vichekesho nk basi kazi nilimaliza kabisa.
Siku moja wazee wake wakaenda msibani lengo ilikuwa wakalale huko msibani ....yeye akaenda kwa dadake by saa11 akaja geto nikawa naye by saa3 mzee akapiga nikaiwahi maana ilikuwa vibration nayeye yuko busy na vichekesho. nikaacha hadi ikakata then nika weka kidenge yeye hakujua kitu akasema baba huwa anapiga kila usiku kuuliza kama tumelala vipi hajapiga tu nikamwambuia hajapiga.
Kumbe walirud bana na baada ya kumkuta hayupo wakapiga simu japo wenzake walisema alienda kwa dada na wakaamini.kesho yake tukaamka saa1 kumaliza kujiandaa saa2 hii hapa.Akaniambi my mi naenda home chap nikacheki halafu narudi kulala umenichosha sana. Huo ndo ulikuwa mwisho wa kumuona asee.....
Baada ya kufika kwao si akamkuta mzee wake na mama yake wakauliza mbona umetoka kwa dadako mapema hivi hata vyombo hujaosha wewe.Mzee wake akapiga simu kwa dada yake bahati nzuri haikupolewa na muda tu mzee akatoka akaenda kutembea hukohuko dada akamurudia mzee wake baada ya kuona alitafutwa mzee aliuliza rachel alilala huko? dada yake hapana alirudi mbona.
Mzee akamrudia mama yake muda huo anajiandaa aje kushona mzee akatoa amri rachel asitoke getini maana hajalala hata kwa dadake....hapohapo jamaa aliyechumbia akapigiwa simu aje achukue mke wake. huku akipewa maneno makali sana na mzee huyu rachel hasa laana iwapo hata sikia maneno yake.
kwa kifupi mkuu hii ni shot story tu na nimeruka vipengele na kuchnganya story utafute ule uzi ukiupata ndo utaelewa zaidi. Ukweli niliumia mno asee lakini nilijipa moyo konde. demu baada ya kwenda kwa jamaa kesho yake tu akanipigia simu ndo akanipa full strory kuhusu kwao tena ananiraumu kwanini sikwenda na ananimbia atoroke nikamfiche kijijni kwetu hata miezi3
Muda ananiambia hela anayo ya nauli kama mimi sina nafasi niwaambie tu nyumbani kuwa kuna mgeni anakuja wampokee atokomee na anasisitiza kuwa ukikubali tu mi naanza kwenda sasahivi.
lakini nilipiga chini kwa maumivu makali mno nikakataa.nilimblok kama mara3 nikachoka sasa maana alikuwa anabdiri no mara achukue kwa majirani zake tu badae akanipa masufuria ya kuanzia maisha ninayo hadi leo
Kabisa. Karibu sana mzeeNdio zao wake za watu hasa wenye familia zilizo na kauwezo kidogo kanakozidi uwezo wako mwanaume. Mwanamke wa familia za hivyo huwa muda wowote anabadilika na kukaliwa kimia ikiwrmo hizo blocks.
Nikuhakikishie ungekuwa na hela nyingi kuliko mme wake hata kama simu yake itapasuliwa utatafutwa na kuombwa msamaha.
Okay...!Tuendelee EPISODE 10B
Lile penzi la jana likafufua hisia zilizokuwa zimeanza kupoteza uhai. Nikajikuta wazo la kubutua ya mwisho niondoke linakosa nafasi. Miezi mitatu ikakatika nikiwa nimekutana na Recho kwa wastana wa mara moja kila mwezi.
Mkeka wa tatu ukaitika, hii sasa ni ajira rasmi ya kudumu. Kituo cha kazi si tu ni mkoa mwingine bali ni kanda nyingine kabisa. Kabla ya kumjuza Recho nilijiuliza maswali machache ikiwemo. Mosi, Mimi nipo na Recho katika mahusiano, je malengo yetu ni nini. Pili, kama kaweza kumcheat mumewe kwa sababu ya umbali vipi kwangu 'mpango wa kando'. Majibu yangu yote yalionesha hapa sina tena changu.
Kama ilivoada, binadamu tumeumbwa kuzoea/ adapt mabadiliko fulani katika kipindi fulani. Ndivyo ilivokua kwangu. Nilizoea kutafutwa mara moja kwa wiki, au hata wiki kukatika bila kutafutwa na hii iliiandaa akili yangu kuwa tayari kupokea taarifa yoyote mathalani kuachana na Recho rasmi. Majira ya kuondoka kwajili ya kazi yalipo karibia nikamjulisha Recho kwa njia yetu ileile.
Mimi " Recho nina habari njema". "Habari gani?" Akajibu. Kwa kuchat hutanielewa, ukipata nafasi nipigie". Akanipigia na nikamwambia nimebahatika kupata kazi mkoa X na Nina week tu kureport. "Dah! jamani kweli Mungu anajibu maombi. Hongera!!". Mimi " Ahsante sana... umenisapoti sana". Akacheka kisha "So waenda lini, Fanya basi uje tuagane nikutakie na safari njema". Mimi " Unadhani naweza kuondoka bila kumuaga mama la mama".
Tulipanga tuonane na hii ilikua nje na kwake. Naweza sema hii ndio ilikua our first date. Sijui alidanganya nini kwa jamaa yake, aliomba nichukue na chumba ili tusiongee kwa kujibana badala yake tuwe 'free' tuagane vizuri.
Ndani ya chumba chenye hadhi ya wastani nipo na Recho. Nikamuonesha vithibiti vya uhalali wa kazi. Recho " Babaa sasa umepata kazi ambayo siku zote tumekua tunamuomba Mungu...nenda ukafanye kazi". Akaendelea " Mimi usiniwaze kabisaa et uko mbali tutaishije.... umepata nafasi usiichezee, Mungu atampa mtu mwingine". "Unanisikia babaa.." nikaulizwa mwanaume .
Mimi "Yep yep.. ila kukuacha hivi inanipa mawazo". Recho kwa sura ya upole na sauti ya kuombea hela ya sadaka akaendelea, " Z mimi sio binti mdogo kwamba nitaanzisha mahusiano mengine...we Nenda kapambanie ndoto yako". Hakuishia hapo akaendelea, "Ukipata likizo utakuja, mbona tumeonana zaidi ya mara tatu toka jamaa kaja!!... itawezekana tu!".
Hii siku nilipewa mawaidha ya kutosha na Recho. Kubwa alilosisitiza zaidi ni Mimi kujishikilia. Nitangulize kazi mbele mapenzi yafate. Alikuwa sahihi sana, nafikiri aliweza kuona udhaifu niliyokuwa nao juu yake.
Moyoni nilijisemea " walahi huyu mwanamke angekua ndio mke wangu, kwa umri wangu huu kimaisha ningekua mbali sana" . Tuliongea mengi na baada ya hapo tukaziruhusu sehemu zinazotofautisha jinsi zetu nazo zipeane mawaidha.
Recho aliondoka mishale ya saa nne usiku kurejea kwake. Nilala pale huku nikiwa natafakari maisha mapya mbali na mwanamke ninayempenda yatakuaje.
Msomaji wangu, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hakika pamoja na ukosefu wa uadilifu katika ndoa yake, Recho alinisaidia kupiga hatua kimaisha mchepuko wake.
Pamoja na kwamba ni kweli nimeonekana kumkatia tamaa kimapenzi lakini bado yeye alionesha yupo ndani ya maisha yangu. Aliniuliza kila hatua niliopitia kwanzia safari kuelekea mkoani mpaka mapokezi kazini. Kwakweli aliweza kuniteka. Nilikuwa najisikia huzuni pale wazo la lini nitamuona tena Recho likiniijia.
Wiki ya kwanza ikaisha, mwezi ukapindika ndani ya makao mapya. Mimi na Recho bado tunawasiliana japo ni kwa style yetu ambayo ni limited. Wiki ya kwanza ya mwezi uliofata Recho ghafla akaacha kujibu status zangu na alikua anaziona, nilipojaribu kupiga simu yake muda wote ilikua busy, Yani nimekua 'blocked.
Ikanistua sana kuna nini kinachoendelea. Nikavunga kwa hio wiki niki 'assume' huenda yupo mazingira magumu kuwasiliana na mchepuko wake. Wiki iliofata hakuna madiliko. Tayari red light kichwani, nikasajili namba mpya na kumpigia nijue changamoto nini.
Simu ikaita kwa muda na haikupokelewa. Nilijaribu tena bila mafanikio. Hofu sasa ikanijaa kwani Recho kapatwa na nini.
Mida ya saa Moja kasoro akanipigia kwa namba yangu mpya " Hello". Nikaitikia "Yes Hello!". Recho "nimekuta umenipigia, sorry nani?". Mimi "Hata sauti hujaijua....ok Z hapa". Baada ya kujitambulisha vile Recho akakaa kimya kwa sekunde kadhaa nikamstua.
"Hello Recho.... ni mimi Z naona umeniblock na hata WhatsApp sikupati, tatizo nini niambie tafadhali". Recho pasipo kuongea lolote alikata simu. Sikuamini kile kitendo na nikivojaribu kupiga tena tayari alikwisha block hio namba yangu.
Maadamu niliweka reserve wazo la siku moja nitaachwa, sio kuachana na Recho kutokana na umbali nikajisemea hii Ndio tayari byebye. Kumbe Haikua hivyo. . . . .
Naomba niishie hapa lakini kesho tutamaliza kisa hiki, niombe radhi kwa ufupi wa kipande cha Leo. Ni muda wangu kwa leo si rafiki
sana. Ahsante!
Niko poa kabisa, bahati mbaya si huko japo ni majirani kimtindoNimepania kaka, kama ni kanda ya ziwa itapendeza..
vp umeamka salama lakini?
Dodoma? Singida? basi toa code tumalize kaziNiko poa kabisa, bahati mbaya si huko japo ni majirani kimtindo
Tabora mkuu 😎, japo makuzi yake hayakuwa hukoDodoma? Singida? basi toa code tumalize kazi
Watu kama hawa....
Nyamwezi? au sukuma?Tabora mkuu 😎, japo makuzi yake hayakuwa huko
Mkuu, tupatie kipandeKaribu sana. Nijuze Episode yako pendwa. Lily Tony
🙏Karibu sana. Naweka mambo sawa.