Hivi ndivyo wauza magazeti wanavyo wafirisi mawakala wa kuuza magazeti

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
Hii tabia ipo na ni mbaya sana sababu mwisho wa siku mtu anaacha biashara ya kuuza gazeti kwa kupata hasara kumbe muuzaji ndiyo anafirisi.

Tanzania kumeibuka mtindo anayeuza gazeti anakodisha kusoma kwa sh 200 badala ya kuuza.

Mtu anasoma baadaye anarejesha na we boss jioni ukija unaambiwa biashara imekuwa mbaya sana na ukiangalia hesabu ziko sawa, gazeti zimedoda.

Nawashauri mtume watu kupeleleza wakijifanya kutaka kukodisha wasome.

Ukimshika uyo fukuza pia ukiajiri mwingine mtishie utakuwa unaweka watu kupeleleza.

Hii tabia inaua biashara za watu muache mara moja na muwe na huruma pia uchungu
 
WENGINE WANATOA HESHIMA ZA MWISHO NDUKI....
 
Anakodisha anaowafahamu ambao ni wachache sana kuliko unavyofikiria wewe!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…