Hivi ni akili au matope!

Hivi ni akili au matope!

Da Asha nakuheshimu sana.Usitake heshima yangu ipungue kwa hicho ulichosema hapi juu.Huyo HS naha ustaarabu wowote kufanya hicho anachikifanya kazini kwake! Kijana naye ana kosa kuwasaliti wafadhili wake kwa kumvuruga HG akiwa kazini na kumshauri aache kazi ili asiwe HG tena!

Tausi Mzalendo naomba nishukuru kwa kunijulisha waniheshimu... I am humbled. In blue... bado nasimamia kauli yangu kua; kua house gal haina maana kua feeligs zinakua na utumwa.... Kupenda kuko pale pale bahati mbaya ama nzuri kampenda kijana wa hapo nyumbani kwa huyo kijana. Naweza kubali kua huyo kijana kamvuruga binti sababu tu! Ni mdogo na sidhani kama ana uwezo wa kum support wala kumuoa (kama nilivogusia last para in the first post); kwamba anapomuambia kua aondoke asiwe house gal yeye anampango wa kumsaidia vipi? other wise angekua kijana ana uwezo wa kumlea na kumuoa binti sioni tatizo bado...

Its the principle da Asha ! Ni suala la nidhamu na pia kutokuvunja uaminifu! Kupenda kupo siku zote haijalishi. Lakini huyu mkaka anachanga mapenzi kwenye eneo nyeti - kafadhiliwa.He cannot breach trust! Atafute HG wa jirani ampende kama ni mtaalam wa kudondokea HGs.Usaliti utaenda nje ya mipaka ya familia.Imagine wewe una watoto, umepata HG ukamwamini na akaweza kukufanyia kazi zako ukakaa na amani.Halafu mtu wa ndani anamrubuni ungejisikiaje? Ningemuona wa maana kama baada ya kumpenda HG, angethubutu kumwambia kaka yake kuwa kaka, nimempenda huyu dada wa kazi, nataka kumuoa.Hapa angekuwa ameweka nia wazi na hata kama kuna kukasirika, ingekuwa haina maana na angesamehewa.Hili la kufanya mambo ya aibu kwenye giza ndilo ninalipinga. Mapenzi hayajalishi nampenda nani maana hata HG ni wanawake kama wengine.Wana haki ya kupendwa na kupenda.Hujasikia hata makazini, wale wanaofanya mapenzi kazini kuna suala la kukiuka maadili?.

I do agree with the principle... Ila naomba unijibu maswali haya:-

  1. Kijana angekua na uwezo kabisa wa kumuoa binti (HG) would it have been still wrong kuingia katika dimbwi la Mapenzi sababu anaishi hapo nyumbani?
  2. Nilijibu kwa vigezo ambavo Wali Mweusi alizungumzia... tone, maneno na maelezo yake ni kana kwamba kosa ni kupendana na huyo binti hali anfadhiliwa na kakake ambae ni Boss wa HG - Hivo basi for instance angempenda binti amtongoze kua atamuoa (kwa nia thabiti kabisa) je bado angekua in the wrong?
  3. In red I do support you na reading btn the lines twapishana badogo sababu ya hapo.... But Hio in beige color je utaifafanua vipi kwa wale wanakutana na kutongozana makazini hadi kuonana.... Will it still be called kuvunja maadili?

Hapo bold tuko pamoja sana.Na kama hali ni hii wote HG na kijana ni wajinga wasio na mfano.Ni kama vipofu wawili wanaelekezana njia.Hapo hakuna mwenye mwelekeo wa maisha wa kumsaidia mwingine bali wametawaliwa na tamaa za mwili tu hakuna lolote.


I am glad we do agree on the above Tausie.....
 
Mkuu well said lakini anapokosea huyu mdogo mtu anaesaidiwa ni kumshauri aondoke wakati hawezi kumfanyia msaada wowote. So wenye tabia za ushauri negative kama huu ni vyema wabadilike. Also True love siku zote zinakwenda na kuwa mkweli so ni bora mdogo mtu hapa awa mwazi ili nae mwenzake akajua jins ya kujiandaa na kujipanga kama wana mpango wa kujaishi pamoja


Shine nakubaliana na wewe kabisa.... Na ndio nilivosema katika my last para of my first post katika hili.... Kwamba yupo faster saaana. Na kakurupuka hajafikiria nini hasa hatma ya hayo maamuzi.
 
Housegirl na kijana mdogo mtu wanapaswa kufunzwa kuhusu kujitambua. Hawaelewi maisha bado, wafundishwe kwamba kufanya ngono kabla ya muda muafaka kuna madhara yake, na wafundishwe kufanya ngono salama, housegirl afundishwe kutambua kuwa wakati wa kazi ni kazi na wakati wa mapenzi ni mapenzi, kijana wa shule aelimishwe kutambua kuwa anatakiwa kujiandaa kwanza kimaisha na kujitegemea sio kupenda vya bure (HG) kwa kaka yake. Hakuna mtu anayeweza kuwazuia watu kufanya mapenzi ila anatakiwa kuwapa elimu ya ngono na kujitambua. Nakumbuka nyumbani HG akija tu Mama alikuwa anamwambia waziwazi tukisikia, ukipata mimba tu unakwenda kwenu sio hapa na hatutajuana tena.
 
Nadhani umeeleza vizuri, ingawa nia yangu sio kuunga mkono uhusiano wa namna hiyo. Wao kama binadamu pia wanaweza kupendana, upendo kama mjuavyo huwa unawafanya watu wawe vipofu, ndio maana unaona wanafanyana humo ndani ya nyumba, halafu hata hivyo unategemea waende wapi?, Guest? Hawawezi kumudu. Siungi mkono mapenzi yasiyo ya ndoa, lakini ninachotaka kusema ni kwamba mtoa mada ulitakiwa ukae nao uzungumze, uwaelimishe na kuwaonya kwa upendo kuhusu hizo tabia na madhara yake. Kwa rika lao hilo ni mambo ambayo unaweza kutarajia.



Simplicity... hapo ni blue hata mimi nimekataa na kusema kijana anakurupuka.....

Nakubaliana na wewe kabisa in red.
 
dada asha tuko pamoja ila ambako sijapendezewa ni kijana kumwambia binti aondoke,sababu naona kama kuna uwezekano wa kijana kumyumbisha huyu binti sbb kijana angekua na kazi ya kumwezesha kwenda kumpangishia binti mahala ili asiwe housegirl hapo ningemuelewa lkn kijana mwenyewe kula yake ya kusaidiwa,pili sijafurahi kumwambia binti aondoke ilhali kijana anajua fika kwamba binti ndiye msaada mkubwa hapo home na akiondoka shemeji yake atapata shida ukichukulia siku hiz ni shida kuwapata hawa mabinti.Tatu kwa nin hapend kuona binti akiwa hapo kama housegirl wkt uhousegirl si kosa la jinai wala dhambi kwa kauli hiyo inaonesha kijana anamdharau binti kwa kuona uhousegirl ni kitu cha aibu.Yeye kijana na huyo binti kupendana ndani ya nyumba ya kaka wa kijana sion tatizo juu ya hiyo,hata kama kijana bado analelewa bado ana haki ya kupenda ila tu anapodanganya yuko chuo kikuu ilhal anareseat form four na anavyomwambia binti aondoke inanitia mashaka kuwa anataka binti aondoke labda kisha amtose maana labda kijana anaona binti akiendelea kuishi hapo anaweza siku moja kugundua kuwa si kweli kuwa anasom chuo kikuu.



Nakubaliana na wewe Cheusie.... Umeongea kweli kabisa.....
 
Tausi Mzalendo naomba nishukuru kwa kunijulisha waniheshimu... I am humbled. In blue... bado nasimamia kauli yangu kua; kua house gal haina maana kua feeligs zinakua na utumwa.... Kupenda kuko pale pale
Bado tuko pamoja dia ADii!

bahati mbaya ama nzuri kampenda kijana wa hapo nyumbani kwa huyo kijana. Naweza kubali kua huyo kijana kamvuruga binti sababu tu! Ni mdogo na sidhani kama ana uwezo wa kum support wala kumuoa (kama nilivogusia last para in the first post); kwamba anapomuambia kua aondoke asiwe house gal yeye anampango wa kumsaidia vipi? other wise angekua kijana ana uwezo wa kumlea na kumuoa binti sioni tatizo bado...

Hii para nzima inabeba uzito wa tatizo
Unampenda binti wa kazi anayetegemewa na wafadhili wanaokupatia uwezesho wa kupata fursa kurudia mitihani.Huyo mkaka angekuwa anajiweza, hajawategemea, nadhani ulinisoma nikasema situation isingekuwa sa bad though bado ni mbaya.



I do agree with the principle... Ila naomba unijibu maswali haya:-

  1. Kijana angekua na uwezo kabisa wa kumuoa binti (HG) would it have been still wrong kuingia katika dimbwi la Mapenzi sababu anaishi hapo nyumbani?

  1. Nimeshatoa msimamo wangu hapo juu na post yangu ya awali


    [*]Nilijibu kwa vigezo ambavo Wali Mweusi alizungumzia... tone, maneno na maelezo yake ni kana kwamba kosa ni kupendana na huyo binti hali anfadhiliwa na kakake ambae ni Boss wa HG - Hivo basi for instance angempenda binti amtongoze kua atamuoa (kwa nia thabiti kabisa) je bado angekua in the wrong?

    Hapo ndio mzizi wa fitna ulipojikita.Kosa siyo mapenzi per se.

  1. In red I do support you na reading btn the lines twapishana badogo sababu ya hapo.... But Hio in beige color je utaifafanua vipi kwa wale wanakutana na kutongozana makazini hadi kuonana.... Will it still be called kuvunja maadili?
Kama mapenzi yao hayaingilii utendaji kikazi its fine.Ndiyo maana watu wengi hukutana makazini wakapendana na wengine hadi kuoana. Ila kama mapenzi yataathiri kazi basi itakuwa kukosa maadili.Mfano Mtunza fedha anapendana na binti halafu mapenzi yake yanapelekea kuvuruga mahesabu, au Boss anapendana na sekretari na kufanya mapenzi ofisini hadi inaleta kero, huwezi kusema that is just love.
[/QUOTE]
I am glad we do agree on the above Tausie.....[/QUOTE]
asante

Wewe kijana wa kiume ambaye umeonewa huruma na kakako, na kuchukua zigo la kukusomesha unaanzisha mahusiano ya kimapenzi ndani ya nyumba ya kakako na house girl.
ADII, Naomba usome tena hii

Ni adabu kweli kugeuza nyumba ya kaka yako guest house, sometimes mchana wapo kazini nyie mnafanya starehe zenu?
Kwa wale wote wenye tabia hii nawaomba muache.:hatari:

Huu ni utovu wa adabu kabisa na ukosefu wa shukrani.Hivi, huyo HG akiondoka, yeye ndio ataangalia nyumba na watoto?
 
Dogo hana akili, alitakiwa afanye heshima kwenye nyumba ya kaka yake.

Msimfukuze mpeni lecture, asikimbilie kucheza na kitabu cha house maid, wakati cha form four kimemshinda.
 
Inaelekea mkuu unaumizwa na nduguyo kuwa na dada wa kazi, kwani wewe una hisia/uhusiano na huyo dada???! mimi sioni tatizo kwamba anakula dada msaidizi,!! angekuwa anatafuna mkeo hapo tungesema toto halina shukrani ya kulipiwa ada!! Kisha wewe jiulize kama unaheshima kwa huyo dada kwa kumpa majina mengine zaidi ya cheo alichonacho cha kumsaidia mkeo!!! Tunawaita Mabeki sawa! lakini unafikiri wao wangependa kudharauliwa kwa namna hiyo?!?! Kwa jinsi unavyoandika hapa ni kwamba huyo dada hana future! usijidanganye na kumdharau kwani aliyekupa wewe ndiye anaye mpatia riziki yeye. Mimi nina heshima sana kwa dada/kaka zetu wanaofanya shughuli hizo kuliko hao wanaoamua kuuza sura na miili yao kwa sababu maisha magumu. Ulichotakiwa kufanya ni kuongea nao na kuwaambia kuwa jinsi gani ungependa nyumba yako mambo yaende na sio kuwaleta humu na kumwaga chumvi baharini. Hapa bado hatujasikiza their side of the story! inawezekana wewe ndiye usiye mstaarabu!! Inama mkuu ufikiri. Jamaa kachagua dada wa kazi na sio mkeo
 
NB: Kichwa cha habari kimenileta humu nilifikiri pacha wangu Matope kaonekana ;-)
 
Kuwa house girl ni jina tu. Lakini ubinadamu uko pale pale yeye ni mtu na ni mwanamke kama wanawake wengine ana haki yakupendwa na kupenda maana mapenzi ni kitu cha muhimu na cha msingi kwa mtu mzima, mleta maada usichanganye status na basic needs. Love and seX ni basic need ya kila kiumbe kilicho hai , haijalisha mnafanyia kwa kaka au nani tulieni msiwe vipingamizi kwenye mahitaji ya msingi ya kila mtu
 
Kuwa house girl ni jina tu. Lakini ubinadamu uko pale pale yeye ni mtu na ni mwanamke kama wanawake wengine ana haki yakupendwa na kupenda maana mapenzi ni kitu cha muhimu na cha msingi kwa mtu mzima, mleta maada usichanganye status na basic needs. Love and seX ni basic need ya kila kiumbe kilicho hai , haijalisha mnafanyia kwa kaka au nani tulieni msiwe vipingamizi kwenye mahitaji ya msingi ya kila mtu
Naona wengi wanachangia hii mada kwa jazba.Hakuna aliyekataa kuwa huo ni ubinadamu.
Mwanzisha mada anachosema ni ile hali ya kijana ambaye hajajitegemea, anayetegemea wengine, kujiingiza kuharibu taratibu za nyumba ya mfadhili wake. Angeendelea na mapenzi yake kimya kimya bila kuharibu utaratibu isingekuwa ishu.Hivi ungekuwa na mtoto/watoto wadogo halafu siku moja ukute mlezi wao katoroka na kuwatelekeza halafu ugundue nduguyo uneyemfadhili ndiye kafanya hivyo bado ungesema "love na sex ni basic needs"?

Tukiendekeza sana huu ubinadamu katika mjadala huu, tukaacha kuona ishu pana tutajipotosha.
 
Kuwa house girl ni jina tu. Lakini ubinadamu uko pale pale yeye ni mtu na ni mwanamke kama wanawake wengine ana haki yakupendwa na kupenda maana mapenzi ni kitu cha muhimu na cha msingi kwa mtu mzima, mleta maada usichanganye status na basic needs. Love and seX ni basic need ya kila kiumbe kilicho hai , haijalisha mnafanyia kwa kaka au nani tulieni msiwe vipingamizi kwenye mahitaji ya msingi ya kila mtu

Akimtundika mimba anaweza kumtunza au utafurahi kuona kichanga kimetupwa??
 
Inakuwaje wewe kijana wa kiume unaishi kwa kakayako, naye ana mke. Wewe uko pale kwa vile umeshindwa shule, sasa unafanya kuungaunga walau upate pa kujishikiza. Kaka yako na mtoto mdogo, akaamua atafute house girl wa kumsaidia mkewe hasa awapo kazini. House girl ni mchapa kazi sana na anamheshimu kakao na mkewe. Wewe kijana wa kiume ambaye umeonewa huruma na kakako, na kuchukua zigo la kukusomesha unaanzisha mahusiano ya kimapenzi ndani ya nyumba ya kakako na house girl.

Kwa vile huwa unaenda shule, wamdanganya mtoto wa watu kuwa unasoma chuo kikuu kumbe unareseat mitihani ya form foru. Halafu kibaya zaidi mnafanya mapenzi humo humo ndani kwa kaka yako, usiku wakati wao wamelala. Kibaya zaidi unamshauri huyo demu aondoke coz hujisikii vizuri kumuona akiwa house girl (mbaya zaidi ze comedy wanapowaitaga ma beki tatu).

House girl anataka kuondoka ghafla tu na hali shemeji yako yupo kazini na hategemei kupata likizo. Jamani, hivi ndugu zetu nyie tuache kuwasaidia?Huko mnakosoma na kuzurura hamkuwaona wadada tena warembo kuliko housegirls?Ni adabu kweli kugeuza nyumba ya kaka yako guest house, sometimes mchana wapo kazini nyie mnafanya starehe zenu?

Kwa wale wote wenye tabia hii nawaomba muache.:hatari:
Nijuavyo hakuna sehemu permanent ya kumpata mwenzi hata we kumbuka wapi ulikutana na huyo mme/mkeo so dogo si ndo kampenda huyo binti no matter ni house girl kwa dogo ndo kafika cha msingi wape semina wote kwa pamoja juu ya madhara yanayoweza kutokea kwa sababu ya kufanya ngono zembe then wache wale mema ya dunia.
 
Niutoto tuu wakikia wataacha tabia hiyo wala usijali....

mtu keshabalehe yuko form four ni mtoto? Ni waharibifu sana hawa! Inatakiwa ukishagundua nyendo zake za kunyatia hosegirl mtimue hapo nyumbani! Rafiki yangu alishafanya hivyo ingawa alikutana na vpingamizi kwa wazazi wake lakini alijieleza kwa undani sana wakamwelewa.Kijana mharibifu aliomba kuishi mahali pengine kwa marafiki, akapata kibarua maisha yakaendelea. Ila kwa kweli vijana aina hii wanaong'ata mikono inayowalisha wapo wengi
 
Kusema kweli sijaona kundondokeana kimapenzi inaingiliana vipi na mmoja wao kua house gal na mwingine kua mzigoa kwa kakake (as you call it) Hebu iangalie kwa upande huu....

House gal ni binti mzuri na mastaarabu na katulia, na ni binti ambae kama mabinti wengine once in a while fall in Love... Anachapa kazi, ana adabu (as per your say); Huyo kijana anakosa gani kumpenda huyo binti? Kwamba sababu ni binti wa kazi hana feelings za mapenzi ama hastahili kupendwa?

Haya basi yaelekea kijana kweli kampenda binti kwa dhati.... Na twaelewa kua a true man always wants what is best for her lady... Wee mwenyewe hapo wasema mahouse gal wanajina lingine (obviously intended at mocking) la beck tatu.... Je kuna mwanaume ambae anampenda kweli mwanamke wake atataka awe house gal?

IMO makosa ambayo naona anayo kijana ni haraka yake.... Kama kweli awategemea kaka na shemejie na ndio anarudia form four; yupo faster saana... Anamshauri huyo binti aondoke aende wapi na atamsaidia vipi? Hata hivo huo ni mtazamo wangu tu....

Sikatai kuwa house girl anazo hisia za kimapenzi, ila kwa nini wanafanya mambo yao hadharani kabisa!Mbona hata sie tulipokuwa kwa wazazi wetu tulikuwa na girlfriends na kwa kweli hayakuwa mambo ya kuwaonesha wazazi, kwa nini ye anioneshe live?Haitoshi wawe na mahusiano, anamshawishi house girl aondoke then what will happen at home?Tunaenda job me na wife, mtoto atabaki na nani?
In short mi naamini kama upo kwa ndugu yako tafuta chako, I mean soma upate kujitegemea, upange gheto lako hapo utakuwa huru kuingiza umtakaye. Ukiwa kwa ndugu yako kuwa na adabu.
After all nshamtimua.
 
]Inaelekea mkuu unaumizwa na nduguyo kuwa na dada wa kazi, kwani wewe una hisia/uhusiano na huyo dada???! mimi sioni tatizo kwamba anakula dada msaidizi,!! angekuwa anatafuna mkeo hapo tungesema toto halina shukrani ya kulipiwa ada!![/B] Kisha wewe jiulize kama unaheshima kwa huyo dada kwa kumpa majina mengine zaidi ya cheo alichonacho cha kumsaidia mkeo!!! Tunawaita Mabeki sawa! lakini unafikiri wao wangependa kudharauliwa kwa namna hiyo?!?! Kwa jinsi unavyoandika hapa ni kwamba huyo dada hana future! usijidanganye na kumdharau kwani aliyekupa wewe ndiye anaye mpatia riziki yeye. Mimi nina heshima sana kwa dada/kaka zetu wanaofanya shughuli hizo kuliko hao wanaoamua kuuza sura na miili yao kwa sababu maisha magumu. Ulichotakiwa kufanya ni kuongea nao na kuwaambia kuwa jinsi gani ungependa nyumba yako mambo yaende na sio kuwaleta humu na kumwaga chumvi baharini. Hapa bado hatujasikiza their side of the story! inawezekana wewe ndiye usiye mstaarabu!! Inama mkuu ufikiri. Jamaa kachagua dada wa kazi na sio mkeo


Hapo kwenye bold,mimi sina any interest with that girl najiheshimu sana isipokuwa sipendezwi na matendo wanayoyafanya. Can you imagine usiku tumelala wanatoka sitting room kufanya sex?Wapo pia ndugu wengine, sometimes wazazi wantutembelea, do you think its pleasant kweli?

Mkuu, nawaheshimu sana wasaidizi wa nyumbani, kwa sababu kubwa moja!WANAWATUNZA WATOTO WETU TUWAPO MAKAZINI! Hilo jina la Beki tatu nilitoa tu mfano kuwa Comedy hupenda kuwaita hivyo, also to me its not good, ila mimi sikufurahishwa na hilo jambo coz dogo namjua tabia zake, yule dada anamchezea tu isitoshe anao wadem kibao. Mbaya zaidi huyu dada ni yatima, alikuwa anaishi na dadake huko Mkoani. Sijapenda hiyo tabia coz najua 100% anamdanganya mtoto wa watu, na ikitokea dada ana ujauzito we unadhani nani atabeba huo mzigo?

Wakati tukiwa home, alikuwepo house girl, you cant imagine tulikuwa wanaume watano and no one touched her. Tulimheshimu as our own sister na aliolewa na mtu mwingine tena kwa heshima kubwa. Kama we ni baba wa familia hutokivumilia hiki kitu, na kama si baba wa familia na wewe unaishi kwa kakako utaona kama nawaonea. Kiukweli HATA WATOTO WANGU SITOWARUHUSU KUFANYA HUU MCHEZO NDANI KWANGU!Nadhani huu ni mtazamo wangu mimi.
 
Back
Top Bottom