Hivi ni kipi kilipaswa kujengwa kwanza, ni kuinua daraja la Jangwani au kujenga Daraja jipya la Salenda hadi Coco beach?

Hivi ni kipi kilipaswa kujengwa kwanza, ni kuinua daraja la Jangwani au kujenga Daraja jipya la Salenda hadi Coco beach?

Hahaha no mtawala gani anatumia hilo daraja?! Kwenda wapi?!
 
Naingalia Jangwani kwa huruma. Bonde linaendelea kujifukia bila hata mipango yoyote kuhimili hali hiyo. Miaka ijayo maji yatafika magomeni. Tangu enzi ya waziri Tibaijuka, kulikuwa na mipango ya kisanii, eti ijengwe bustani ya kupumzikia, wapi! Mipango ni mibovu.

Napendekeza; kuliko kupoteza pesa kwa ujenzi wa daraja la Selander, eti linapita baharini, jengeni daraja la jangwani. NI barabara muhimu kuliko barabara zote za dar. Ndo pekee iliyo na mizunguko mingi ya watu
 
Mvua zikiisha nyinyi nyote mnao lalama mtaungana na serikali kusahau daraja la jangwani! Mtaanza tena kipindi cha masika. Mtasahau tena baada ya masika kwisha. Hivyo hivyo mpaka mnazeeka. Au mnahamia chama tawala na kufumbuka macho.
... kama mwanamke mjamzito pindi uchungu umjiapo. Akishazaa papo hapo anasahau na "kumpa tena mumewe" hivyo hivyo hadi anazeeka.
 
Ni kweli hili daraja ni la miaka mingi sana na halikuwahi kuleta kero kama hizi hapo kabla.

Vipi hizi kero zije baada ya kujenga mwendo kasi na ofisi zake pale?

Kilichofanyika, walipoongeza barabara ya mwendo kasi na kujenga ofisi kuna mkondo umefinywa pale, matokeo yake kutapika kule na si swala la mazingira Boss!
Nashukuru lakini usisahau uchafu unaotupwa mto wa msimbazi na uchimbaji michanga ambapo kunakuwa na mmomonyoko wa mchanga unaoziba.
 
Bu'yaka,
Unastahili sifa kwa kuifahamu Dar vizuri kuliko wengine. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba eneo la Magomeni linajikata, halitapitika tena kuingia kati ya jiji. Hiyo haihitaji kujua kona hii na ile au kitongoji hiki na kile. Ni ubabaishaji tu!
 
Mystery,
Ukitaka kutatua tatizo lazima ujue tatizo. Nawe una tatizo la kutojua tatizo ni nini! Unamlaumu rais na kumuita misifa kwani hapo Jangwani matatizo yameanza leo? yalianza zamani, je, wakati rais Kikwete anabariki mradi wa daraja la Selader hakujua tatizo la jangwani? Kwa nini unamuita rais wa sasa misifa? Kuna wakati mtu una tatizo, jingine lakini unaamua kulilia sababu nyengine.

Halafu sasa, wewe umegeuka kuwa injinia kwa kuomba daraja liinuliwe. Nani amekuonesha kwamba likiinuliwa ndo ufumbuzi. Toa kilio chako uwaachie wataalamu watatue. Siyo kuomba liinuliwe, kwenda wapi? Msimbazi haihitaji ufumbuzi rahisi kiasi hicho. Lazima vichwa vya maana vikae na kuamua. Daraja lilishainuliwa tangu mwaka 1982 mbona leo limefunikwa.
 
Hii ni Aibu iliyo kuu kwa Wahandisi wa jiji hili. Nilishasema, hakuna siku hata moja ya kuzuia mafuriko kwa kutanua kingo za mto! Kinachotakiwa hapo ni hiyo mito ichimbwe iwe na kina ijengewe kwenye floor na pembezoni kama ulivyokuwa mto unaopeleka maji ziwani jiji la Mwanza!
 
Zygot, Vichwa gani wa maana haooo
Au Hao wenye matumbo makubwa wanakaa ofisini
Shida yenu nyiee hamna long term plan
Nyie ni wazee Jenga Leo kesho mnabomoa

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kwanza Tumalize project za kuijenga cattle

Mkinichagua tena awamu ya pili ...Basi ni tawafikiria dhidi ya hapo Jangwani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
January Makamba alishaandaa na kuanza kutekeleza mpango wa bonde la msimbazi na mito yake. Wafadhili walitoa hela. Baada ya figisu za kisiasa wahisani walikata hela...mpango huu ulihusisha ujenzi wa barabara ya juu toka fire hadi magomeni, uhamishaji wa wananchi, kubadili matumizi ya bonde n.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata wewe inaonekana kabisa tatizo hujalielewa! Haijalishi yalianza lini na nani aliaababisha! Mimi na wengine tumeshuhudia haya matatizo ya jangwani miaka na miaka!
Ni kwa nn hii serekali iliopo wakati huu na ikifanya miradi mingi na mikubwa ya ujenzi kimfano daraja la baharini, ukilinganisha na kero inayotokea jangwani kila mvua zikinyesha, pesa tunazo ndo mana tunajenga! Tatizo ni nn??

Kuna mdau hapo juu yeye alisema daraja la jangwani wanapita walala hoi na daraja la baharini wanapita wenye hela zao!

Na mi naunga mkono hoja hii.
Ukitaka kutatua tatizo lazima ujue tatizo. Nawe una tatizo la kutojua tatizo ni nini! Unamlaumu rais na kumuita misifa kwani hapo Jangwani matatizo yameanza leo? yalianza zamani, je, wakati rais Kikwete anabariki mradi wa daraja la Selader hakujua tatizo la jangwani? Kwa nini unamuita rais wa sasa misifa? Kuna wakati mtu una tatizo, jingine lakini unaamua kulilia sababu nyengine.

Halafu sasa, wewe umegeuka kuwa injinia kwa kuomba daraja liinuliwe. Nani amekuonesha kwamba likiinuliwa ndo ufumbuzi. Toa kilio chako uwaachie wataalamu watatue. Siyo kuomba liinuliwe, kwenda wapi? Msimbazi haihitaji ufumbuzi rahisi kiasi hicho. Lazima vichwa vya maana vikae na kuamua. Daraja lilishainuliwa tangu mwaka 1982 mbona leo limefunikwa.

Sent using Redmi Y2
 
TUJITEGEMEE,
Mapendekezo yenyewe haya hapa chini. Niliyaweka hapa 17July,2018 kwenye uzi wa Mbu wa Muhimbili
TUJITEGEMEE,
 
Mystery,
Dawa si kuinua barabara, dawa ni kuvunja nyumba zilizo bondeni3ili maji yapite
 
Baada ya kuona haya mateso makubwa wanayopata wanabchi kwa kufunga barabara inayounganisha jijini Dar na Magomeni ikijirudia Mara kwa Mara kutokana na mvua kunyesha, nimekuwa nikijiuliza hivi hawa watawala wetu walitumia busara kweli kuamua kujenga daraja la kuunganisha coco beach na selander, badala ya kutoa kipaumbele cha kuliinua daraja la Jangwani?

Imekuwa ni kawaida sana kwa siku za karibuni kila mvua inaponyesha, hata kama ni ndogo, tunaambiwa kuwa barabara ya Morogoro, inayounganisha Magomeni na jijini Dar imefungwa

Hebu tujaribu ku-imagine ni madhara kiasi gani yanayopatikana kiuchumi kila barabara hiyo inapofungwa?

Hebu pia tujaribu ku-imagine ni wakazi wangapi wanapata usumbufu wa kutokwenda kutibiwa kwenye hospitali ya Muhimbili au kwenda waona wapendwa wao waliolazwa katika hospitali hiyo kubwa hapa nchini kutokana na kadhia hiyo?

Lakini kwa kuwa nchi hii hivi sasa tunajua kuwa inaendeshwa kwa "misifa" ya ONE MAN SHOW, kila alitakalo bwana yule ni lazima litekelezwe, bila kwanza kuangalia ni kitu gani cha kutoa kipaumbele kwa muda tulionao

Nina hakika watu maelfu kwa maelfu, wanaathirika sana na hii barabara ya Morogoro ya kipande cha daraja la Jangwani kinachounganisha Magomeni na jijini Dar
Tuache ubinafsi, barabara ya nyakanazi to kigoma ndio muhimu zaidi,,jangwani ni makosa ya kujenga namna ile wakati mto mkubwa unapita pale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom