Hivi ni kipi kilipaswa kujengwa kwanza, ni kuinua daraja la Jangwani au kujenga Daraja jipya la Salenda hadi Coco beach?

Mbona husemi baada ya kuzibomoa hizo nyumba, maji yapite wapi! Juu ama chini ya barabara? Tunaongelea shida inayojirudia ya kukatika mawasiliano pale jangwani kila mvua kubwa inaponyesha!
Dawa si kuinua barabara, dawa ni kuvunja nyumba zilizo bondeni3ili maji yapite

Sent using Redmi Y2
 
Ni kweli mkuu hii barabara ya kutoka kigoma, kibondo mpaka nyakanazi ni shida sana pale, ila ni lazima tuwe na vipaumbele.

Ila vile pesa tunazo, ni sisi tu kuamua pa kuzielekeza, hiyo ya nyakanazi ingeweza kujengwa na jangwani pia n.k.

Bado ni gharama ndogo kuliko miradi inayojengwa na serekali + manunuzi ya ndege, ni utashi tu ndo tumekosa"
Tuache ubinafsi, barabara ya nyakanazi to kigoma ndio muhimu zaidi,,jangwani ni makosa ya kujenga namna ile wakati mto mkubwa unapita pale

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Redmi Y2
 
Tatizo kila mtu leo hii ni mtaalamu wa ujenzi na mazingira. Kweli unaamini mto huo ukichimbwa mafuriko yatakoma? Unauita mto sawa, mi nasema ni bonde linaloanzia Gongo la mboto. Utachimba tangu gongo la mboto hadi Selander? Hiyo idadi ya watu waliovamia bonde hilo uwaweke wapi? Unachimba nini na kimetoka wapi? Vowanda vya tabata unaviweka wapi?

Tusijipe ufahamu wa haraka na kuona ufumbuzi. Ni tatizo gumu kuliko tuonavyo hapo kwenye mafuriko.
 
Tatizo kila mtu leo hii ni mtaalamu wa ujenzi na mazingira.
Hii si sawa kabisa, kuparamia utaalamu wa ujenzi na mazingira, kumradhi kwa hilo. Hata hivyo nimeshangazwa na namna ulivyoshindwa kutumia 'professionalism' kuuliza ni namna gani utekelezaji wa mpango ninaopendekeza utakavyokuwa; kwa kuanza na swali la '.....unaamini mto ukichimbwa mafuriko yatakoma..!?'

Tusijipe ufahamu wa haraka na kuona ufumbuzi. Ni tatizo gumu kuliko tuonavyo hapo kwenye mafuriko.
Lakini si busara pia wataalamu kukaa kimya, mkisubiri sijui amri ya nani, huku mambo yakiharibika. Ndiyo maana sisi ambao siyo wataalamu tunalazimika kuumiza vichwa kuona namna gani tatizo linaweza kuondolewa kwa haraka na kwa faida ya wengi.

Sasa, Mkuu, wewe ambaye ni mbobezi, nguli, mtaalamu aliye makini kabisa kwenye masuala ya mazingira na ujenzi toa ushauri wako wa kitaalamu juu ya namna ya kukabiliana na tatizo na Bonde la mto Jangwani/Msimbazi.

Karibu.
 

mbona Dubai nako Kuna mafuriko nako Ni makonda kayaleta? Mwaka huu Ni wa neema limeni, maji yakija yaacheni yaende baharini yakiisha piteni,
 
Mlalahoi unawahi kwenda wapi? Wacha matajiri wawahi kwenda tra kulipa Kodi ili mlalahoi apate matibabu watoto wasome bure
 
TUJITEGEMEE,
Ushauri wangu wa haraka ni kwamba siyo kila mafuriko yanarekebishwa kwa ujenzi wa madaraja na kuchimba mitaro. Kuna wakati tunayapisha na kuna sehemu duniani zimeachwa na binadamu, kutafuta sehemu zenye amani. Miji huanza na kufa! Using'ang'anie Dar hata kama nature hairuhusu tena!

Dar ni mji ulioanza kama bandari, maji mengi ni sehemu ya sifa za bandari. Kwa nini unalazimisha ufie Dar na kulaumu serikali, ifanyeje?
 
Zygot,
I see Well I! Sina la nyongeza. Nasubiri maoni mengine ya wanaJF
Asante kwa maoni yako.
 
Unacho kinena sahihi kabisa, Kati ya watu na bonde Nani kamfuata mwenzie? Hamieni dodoma yaacheni maji yapite zake kwenda baharini, mnakuwa Kama mumevaa mawigi mnataka kuoga shower bila kulowana kichwa
 
Serikali haikukosea na sipingi ujenzi wa daraja jipya la salenda lenye urefu wa km 1.5 ambalo ni kubwa kuliko lile la nyerere kule kigamboni.
Lakini ujenzi huu umekuja katika wakati ambao kwa maoni yangu sio sahihi ukilinganisha na kero nyingi za wananchi zilizopo kwa Sasa.

Ujenzi huu unagharimu Tsh bil 556.1 huku serikali ikitoa bil 49.5 ikiwa zaidi ya bil 506 zikiwa ni ufadhili kutoka Korea kusini.

Pamoja na kuwa mradi huu umekuja kwa lengo la kupunguza adha ya foleni katika eneo hili lakini kuna maeneo muhimu zaidi katika mkoa wa Dar es salaam ambayo yalitakiwa kupewa nafasi ya kwanza kwenye ujenzi.

1. Daraja la Jangwani
Daraja hili ni kiuongo muhimu Sana hapa jijini, ikumbukwe kuwa shughuli nyingi za wana dar hutegemea sehemu hii kuunganisha wilaya kinondoni na Ilala kupitia fire na magomeni.
Mara nyingi daraja hili limekuwa likikumbwa na adha ya mafuriko na kufunikwa na maji hivyo kukwamisha shughuli nyingi kwa masaa mengi Sana. Hii ni kero kubwa na niaibu kwa jiji letu hili bora kabisa Afrika mashariki.
Badala ya daraja la salenda serikali ingeanza na hili kwanza.

2. daraja la mto msimbazi katika eneo la Kigogo njia panda
Hapa napo ni sehemu korofi sana lakini ina umuhimu mkubwa kwa wakazi wa jiji la Dar Kama ilivyo kwa eneo la Jangwani hapa napo tatizo ni lile lile, serikali isifumbue macho eneo hili, kila siku Makonda anakuja hapa kujifanya kuangalia athari za mafuriko bila kuchukua hatua yoyote ile, hapana tumechoka Sasa.
Badala kujenga daraja la salenda mngeanza hapa kwanza.

Na sio kujenga daraja tu bali mje na
mpango mkakati wajinsi ya kutanua mto msimbazi kupunguza athari za mafuriko kwa wakazi hawa.

Nasisitiza kusema ujenzi wa daraja la salenda serikali yangu imekurupuka mlitakiwa kuangalia ni eneo gani linagusa watu zaidi Kama kweli hii ni serikali ya wanyonge.

Achaneni na miradi inayolenga tu kupendezesha jiji huku wananchi wanalia.
Mh Rais wangu mpendwa naomba liangalie hili utakuja kuwaambia nini Wana Dar es salaam wakati wa kampeni??
Umejenga mfugale na ubungo ujenzi unaendelea hatupingi kabisa lakini hao watu wanao tokea kimara kupita ubungo kwenye flyover kuja kariakoo watapita wapi wakati Jangwani daraja linajaa maji MH RAIS?

Mh Makonda unayaona haya?
Wananchi wamechoka kukuona unakuja na macamera kupiga picha za daraja kufunikwa na maji watu wanashindwa kuendelea na shughuli za kila siku we kazi unakuja kupiga picha au mnaona kuwa hili ni kivutio cha utalii?

Tumechoka!!.
 
Flyover ya kwanza tanzania ilipaswa kuanzia magomeni ikatue fire mengine ndio yaendelee, au tuuze dege moja nn 2fanye ye2
 
Dam55,
Mkuu Dam55 umeunena ukweli mtupu kwa asilimia 100, Mwenye masikio na asikiye na mwenye kuona na zone

Unajua shida ya nchi hii kwa watawala wetu kupenda misifa.
Wanaona vyema kutoa kipaumbele kwa miradi hiyo mikubwa mikubwa
 
Foleni Salender ni kila siku. Mafuriko ni mara 5 kwa mwaka . Sasa jipe jibu mwenyewe
 
Mystery,
WAHENGA WALISEMA....... "WAPISHI WENGI HUHARIBU PISHI". Si kila wazo lako linafaa kutekelezwa, nchi hii inashida nyingi saana toka inapata Uhuru, Raisi Magufuli si Mungu aliye kuja kuzitatua shida zetu zote, ila tu baadhi na yeye kama kiongozi lazima awe na mapendekezo na inapobidi awe na kauli. Hivyo yeye kama kiongozi Mkuu Wa nchi anayafanya hayo, si kama usemavyo anafanya ONE MAN SHOW........ ACHA MAZOEA. Yaliyopita kwa awamu zilizopita siyo lazima uyaone kwenye awamu hii. Tuache kumkatisha tamaa Mh Raisi hata yeye ni binadamu mwenye moyo anahitaji kutiwa moyo na kupongezwa kwa kazi nzuri anayoifanya
 
Mystery,
Unapita kwenye barabara za juu ubungo ukifika jangwani gari linazama kunatatizo la huko gorofani kwa viongozi wetu namaanisha upstairs
 
Hizo porojo za kajima tunazifahamu. Ila kabla ya ujenzi huu wa BRT maji yalikuwa hayapandi juu ya daraja. Maji yameanza kupanda juu ya daraja baada ya huu ujenzi kwa kuwa wameyang'anya maji sehemu ya kutulia bahari inapokuwa imejaa.

Kumbuka wakati huu ujenzi unaanza vifusi vyote walivyokuwa wanafukua barabara ya zamani walikuwa wanavileta hapa jangwani wakawa wanasawazisha mpaka wakapa_level na kujenga karakana moja iliyokuwa na mabomba mengi sana pale nje. Ile karakana baadae walikuja kuiondoa lakini damage ilikuwa imeshafanyika kwani lile bonde lilikuwa limeshaminywa na kupunguza uwezo wake wa kuhifadhi maji. Ndio maana tangu hapo hili tatizoo limeanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…