Hivi ni kwamba bidhaa za mbao hazina thamani tena siku hizi?

Aah! Zile fenicha bandarini ni mbao au?
 
Kweli wanajifariji, kuna radio miaka 1979 ,Mimi hapo nikiwa na miaka tisa zilikuwa za mbao (super muninga) National, naziona vijijini hadi leo zipo halafu watu wanazungumza kuziponda.
 
Vitu vya mbao ni ghali sana. Ukiwa na 250000 unapata kabati simple la kichina kwenye mbao sasa ni shida.
 
Vitu vya mbao ni ghali sana. Ukiwa na 250000 unapata kabati simple la kichina kwenye mbao sasa ni shida.
Hilo kabati la kichina utadumu nalo miaka mingapi? Tena kama ndio mtu wa kuhama nyumba kila baada ya miezi sita isitegemee litakaa hata miaka mitatu.
 

Nilitaka nimpe mfani wa mlango wa mbao ya mninga wa 900x 2100 ni tsh 600,000 (frame plus mlango)
 
"Wasingekuwa" kina nani hao!?
Ukileta Siasa katika mambo ya msingi kama haya ambayo yanapaswa kujadiliwa kwa hoja nitakuona mngese wa kiwango cha SGR. Otherwise ungeweka hili bandiko lako katika jukwaa la Siasa kuna baadhi ya watu tungepita kimya.
matusi tena mr ya nini? nimesema sisi watumiaji wa ndani wa mazao ya misitu hatuwezi kumaliza msitu uliopo nyakati hizi. ila kwa sababu walikuwepo watu waliokua wakipeleka magogo nje basi miti ingeisha mapema ndio ilikua maana yangyu mkuu.
 
Reactions: etb
pole sana, ni aina ya mbao tu haikua rafiki na mazingira yenu ndio maana ilishambuliwa na mchwa
 
na ambayo pia ni imara mkuu
 
nakushushukuru mkuu kwa kuliona hilo, lakini huko vijijini kunakotoka mbao garama yake ni chini mno! ila serikali ndio ilaleta ugumu.
 
sio hazina thamani laa! bali hazithaminiki tena na wateje siku hizi japo zina ubora wa hali ya juu kuliko chuma alunium plastic nk
 
hilo kweli mkuu kosa hilo tumelifanya sana lakini sio kwa sasa au kwa wengi wetu.
 
Wewe ni kichwa maji ujui jamaa kaongea point ya msingi kuliko zote bei ya mbao imepandishwa na wahuni ili kuuza nje ya nchi wahuni wamechukua tenda na kudhibiti mbao toka mapolini ili kuuza magogo nje ya nchi

Sent using Jamii Forums mobile app
asante sana mr ndio ilikua maana yangu haswa.
 
Nyumba za zamani zilikuwa zinatumia madirisha ya mbao, sasa hivi watu wamegeukia Aluminium. Makabati ya mchina yapo tele. Makochi sasa hivi ni mwedo wa sofa. Vitanda hadi vya chuma vipo. So fani ya useremala lazima iathirike. Lakini ufundi ni ku migrate. Fundi seremala akienda semina kidogo tu, anaweza kutumia ujuzi ule ule kutengeneza dirisha la Aluminum...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…