Hivi ni kweli kuwa kila Mwana JamiiForums ana degree?

Hivi ni kweli kuwa kila Mwana JamiiForums ana degree?

Shalom wakuu!
Swali hili limekuwa likinitatiza sana tangu miaka 2 iliyopita tangu nilipojiunga na JF,

imekuwa ni kama fashion kwa wanaJF wengi kudeclare elimu zao katika post zao nyingi, ajabu kila mtu anasema sijui alipokuwa chuo mwaka wa pili, mwingine ooh nimejiajiri lakini nina degree yangu, hivi ni kweli wote tumesoma mpaka level hizo? Hakuna hata mwenye diploma au Form4 kabisa? Mbaya zaidi hadi vijana wa BRN wa humu JF naona wameanza taratibu kurithi haka karoho ka kipepo kanakotokana na kutojikubali.

Tubadilike jamani.

Anza Wewe tukusikie!

Kwani mtu akisema mwaka Wa pili chuo ni lazima iwe chuo kikuu?
 
Shalom Baba! Huwezi jua, nimebahatika kukutana na member kazaa, wote wana masters kwenda mbelee.....
 
me darasa la nne ya zamani.. nimesoma chuo cha ufundi wa kushona viatu..
 
Ukizaliwa DSM ni form six.ukisoma mpaka form 4 una degree
 
Back
Top Bottom