Hivi ni Kweli Tulihitaji Katiba Mpya au ilikuwa ni katika Njia tu za Kumsumbua Kikwete?


Tena ni wanafiki walikobuhu
 
Kuna Radio ziliwahi fungiwa kwa mijadala ya aina hii, haya tuendelee.
Salary slip hata kama unapinga unaiona ile amshaamsha ya katiba mpya?? unajua katiba mpya imechangia kiasi gani kukuza deni letu la taifa? hivi ni kweli tulihitaji hiyo katiba? au ilikuwa ni uchungu tu wa kushindwa kwa waraka?
 
Ungesikia kelele CHASO, BAVICHA, KANISA LA UFUFUO, sijui kigango gani yaaani ni vurugu mtindo mmoja
 
"Sisi kama CCM, kwa wingi wetu tunashindwa kuishauri Serikali kwa mambo ya ukweli, hatuna sababu ya kubaki kuwa madarakani".

Mhe. Hussein Bashe (MB).

Huyu jamaa nimemvulia kofia natamani CCM ingekuwa na Wabunge wengi na hata Viongozi wa juu wa CCM wenye mtazamo kama wa huyu lakini kwa MACCM wengi chama kwanza na nchi baadaye na hii inaigharimu sana nchi yetu na hivyo kukosa maendeleo ya kweli kwa miaka chungu nzima sasa pamoja na utajiri mkubwa tuliokuwa nao.

 
Nakubaliana na heading "je tulihitaji katiba mpya? " maana ni kweli ukimya umetawala kama hakuna tena haja ya Katiba (japo maelezo ya mtoa uzi na comments zimeuhamisha uzi toka kwenye heading ya msingi).
Ninachokiona wapinzani walitegemea mabadiliko ya Katiba ikiwemo tume huru ya uchaguzi isaidie kuwalinda kwenye uchaguzi mkuu na ndio hasa chanzo cha kuungana na kuunda ukawa. Sasa uchaguzi umeisha hawana tena morali ya kudai katiba.
 
Wewe ni mdini na unasambaza udini.Hivi waliosema JK alikuwa ni chaguo la Mungu walikuwa wa dini gani?Mbona hili hamuhoji?

Ni wale waliotoa Waraka wa kuongoza Waumini kuchagua Mchamungu 2010.

2005 walimwita Chaguo la Mungu kwa Muongozo wa Edward Lowassa aliewarubuni kuwa wakubali tu kwa kuwa Yeye atakuwepo serikalini na atakuwa PM hivyo atamdhibiti wasiwe na hofu kwa kuwa pia Spika wa Bunge litakaloisimamia Serikali pia ameshapangwa kuwa Mzee wa Kanisa Samwel Sitta hivyo hatofurukuta, ndio sababu alipofukuzwa ndio figisu figisu na kejeli na hujuma dhidi ya Rais zikapamba moto ila Watanzania wakasimama Imara na kupuuza hizo hujuma na wengine wakazifichua mmoja wapo akiwa Hayati Baba Askofu Moses Kulola Mkuu wa TAG. JK ule Uanajeshi ulimsaidia kuwa na kifua cha kusitiri Mengi.
 
Hii siyo dalili nzuri hata kidogo. "Imani isiyotakiwa na imani inayotakiwa"
 
Waliokataa katiba ya warioba wote wapo chadema unategemea nini.

Nyumbu kimyaaaaaaaa
 
Je tulihitaji katiba mpya kweli au ilikuwa usumbufu tu kwa jk?
 
Mkuu
Mkuu: nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani lakini nadhani safari hii walikuwa genuine, lakini si kwa kutaka haki-bin-haki bali kutafuta dola kwa mlango wa nyuma. Walitaka serkali 3 walijua watashindwa lakini wakaona si vibaya kutikisa kiberiti. Walitaka Tume Huru ya Uchaguzi hii nayo ilikuwa kutikusa kiberiti kwa sababu Mungu bado hajaanza kutuchagulua tume, bado itabidi wachaguliwe na mtu fulani. Nani kama Rais? Kumbuka Rais ni mchaguliwa wa wananchi wote. Walitaka mgombea huru bila kujua undani wake, wakidhani ni rahisi kugombea binafsi kama una hela. Wisely yalawekwa masharti kuzuia matajiri wa unga kuitenunua nchi kwa kununua kura. Ya mwisho ni Rais kupingwa mahakamani hiyo wamepata kila mtu alitaka. Lakini masharti yametosha kuzuia abuse kwa peoples power kuandamana bila kikomo.
 
There is every possibility kwamba ile ilikuwa dili ya wajanja.Hata hivyo to me kama utekelezaji wa katiba ya 1977 ingeboreshwa na utekelezaji wake ukasimamiwa vizuri,tungepata tija tunayoitegemea.
 
Hata makosa anayofanya Raisi eg kuzuia bunge live au kuzuia sukar wanapewa wengine! La sukar wameangushiwa wafanyabiashara la bunge live ameangushiwa Nape wakati nape ni mtekeleza maagizo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…