Hivi ni ukoo wetu tu tuko hivi au na wengine mna experience upuuzi kama huu?

Mkuu,usiogope fanya vile fikra zako zinavyokutuma lkn usivinje sheria!
 
Mkuu familia zetu ndivyo zilivyo...
Unawajali lkn usiwadikilize sana masna utakuja kuwatenga..
 
njoo unyamwezini uone ungekuwa ushakufa kitambo
Sio vijiji vyote nakataa, kwa Mara ya kwanza nimekwenda Mimi na ndugu zangu msibani ndugu karibu wote walikuwa hawatujui kabisa baada ya mazishi kabla wanakijiji hawajatawanyika kilifanyika kikao cha sisi kutambulishwa pale kijijini na baada ya hapo tuliagana nao na tuliondoka vizuri tu hakuna lolote lililotupata sio njiani wala makwetu nimefupisha. Hivyo mkuu usiseme unyamwezini sema Kijiji X... , ningekubaliana na wewe kama ungesema Kg kule kwa akina Mzito Kabwela
 
Tabora wanaweza kumsaidia mgeni ila sio mwenyeji huwezi kukuta kiongozi wakuchaguliwa mwenyeji wote ni wageni akijaribu mwenyeji hawampi hata kama anaelimu kiasi gani ndo maana maendeleo kwa Tabora sio Leo uswahili umekithiri
 
Daah pole sana mkuu itakuwa ni kwa upande wenu but kwetuu nijuavyo ni ngumuu sn
 
Nilichojifunza kwenye story yako na huenda ndo uhalisia ni kuwa: wazazi wako waliumia unamwaga pesa kwa "watu baki" ilihali wao nyumbani wanashindia dagaa... Yaani huwahudumii wakafurahia jasho LA kujinyima kwao usome au upate nafasi uliyopo.

Tujitoe kwa wazazi wetu jamani, tusiwaone wanazeeka vibaya!! Wanamahitaji mengi muhimu na hawawezi kuwa wanatuambia kila siku tuwatumie hela. Tunahitaji kuwa tunatuma tu bila kuombwa! Siku ikitokea jambo kama hilo la kujitolea kwenye jamii hawatanung'unika, maana watakuwa wameridhika na huduma tunazowapatia.
 
Bora kuishi Na watu baki Tu ndugu Ni masnitch Sana. Hapa nilipo nimezungukwa Na ndugu ugomvi hauishi. Nipo kwenye kampeni nikajenge mbali nimuhamishe na mama.
Mimi ilikuwa ni falsafa yangu, siwezi kuishi ama kufanya kazi nilipozaliwa!!! Kuna majungu na ujinga mwingi sana, huwezi kuendelea.
 
Mambo ya ukoo nlishakataa, I got family.
Ndugu wengine hata ciwajui na cijawahi kuwaona na sihitaji hata kuwaona,
Bora rafiki wa kweli atapenda ufanikiwe kuliko ndugu all tym hawataki maendeleo
 
Haya mambo yapo sana na hali hii inachagizwa pia na wazazi wetu.kwenye vikao vya kifamilia kama baba au mama ameshiriki huwa wakishajua kwamba mtoto wao ni mwenye moyo wa huruma wanajitahidi wakae nae karibu ili wampe ndogo ndogo kwamba asubiri wale wanafamilia wenye uwezo watamke kwanza ahadi zao ndo kisha yeye atamke.

So yule ambaye ni mambo safi sana akishasema na unfortunately akatamka kiasi kidogo itabidi utembee mule mule aliposema tena wanakushurutisha upunguze kiasi na obvious hawa wenye uwezo huwa wanatamka kiwango kidogo ili{kwa akili zao}ili kuepuka virungu vya wanafamilia kuwalilia shida hili likishapita.

Kwa siye tuliotoka vijijini,Kaskazini mwa nchi huwa tunakuwa na umoja wa ukoo ulio na katiba na sheria kamili wakati huo huo wazee pia vijijini huko wanakuwa na vikao vyao na katiba yao inayowaongoza.likija tatizo tunakaa vikao sisi kama vijana linawekwa mezani linajadiliwa kama ni lakutekelezwa kwa umoja{yaani papo kwa papo kwamba kila mwanaukoo atoe tuseme Tsh20,000/=}tunafanya hivyo laah halitekelezeki basi tutachangishana na kiasi kitachopungua kitatoka kwenye hazina ya ukoo inayotokana na michango yetu ya kila mwezi tuliyopangiana kutoa.

Matatizo huwa hayana hodi,matatizo sio harusi maana harusi hata ukiahidi miezi minne mbele hapana shaka yoyote shida ni pale utakapomshuhudia ndugu yako ktk kitanda cha mauti kwa kukosa japo 1mill kama familia ya kumfanyia kipimo fulani cha dharura ili doctor ajue amwandikie dawa ya aina gani,i swear to God hii picha itakusumbua maishani mwako maana unakuta huku unaogopa kutoa ili kuiridhisha jamii fulani huku ukitaka kutoa umuokoe nduguyo sasa muda wote huu unaoutumia kujitafakari Mungu nae anafanya yake.

Haya mambo huwa yanaandaliwa,cha kufanya wote kwenye koo zetu tuhamasishane tukutane kwa vikao japo mwezi mara moja kwa tunaokaa mji mmoja au hata miji mingine maana siku hizi huduma za SimuPesa zimerahisisha sana kufikisha amana kwenye mambo kama haya.tuwekeane kiwango kidogo tu cha ada kwa mwezi japo Tsh10,000= mkiwa 20 au hata kumi ndani ya mwaka mmoja mna bei gani?ikitokea tatizo la kutaka million 1 hakuna tena kutegeana yule aseme kwanza ndo mi niseme.

Yangu ni hayo wakuu......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…