Hivi Rais kutotoka nje ya nchi ndiyo Uzalendo? Hatukusema usitoke kabisa bali tulichukia safari zisizo na tija

Hivi Rais kutotoka nje ya nchi ndiyo Uzalendo? Hatukusema usitoke kabisa bali tulichukia safari zisizo na tija

CreativityCode

Senior Member
Joined
Aug 8, 2020
Posts
158
Reaction score
653
Mgombea wa CCM John Magufuli amenukuliwa siku za hivi karibuni kwenye kampeni zake kuwa alipoapishwa kuwa Rais wa Tano wa Tanzania moja ya mambo aliyoyafanya ni kutotoka nje ya nchi na hasa kutokwenda nchi za Ulaya na Marekani.

Sababu za kutokwenda Ulaya na Marekani ni kuwa yeye ni mzalendo na alitaka kuchapa kazi na kubana matumizi.

Hoja zake zote hazina mashiko na inaonesha ni kwa kiwango gani haelewi kabisa kuhusu uhusiano wa biashara ya kimataifa na diplomasia.

Kuna faida kubwa rais wa nchi kukutana na viongozi wenzake huko duniani kuliko kujifungia ndani, nitaorodhesha hapa chini.
  1. Angelipata uelewa mpana wa dunia kuhusu ushindani wa biashara na namna ya kufaidika nao. Sio porojo eti tuko kwenye vita ya kiuchumi, nani awe na vita na Tanzania kwenye vita ya kiuchumi. Vita ijulikanayo ya kiuchumi ni kati ya China na USA (Mashariki dhidi ya Magharibi), sisi wengine hatugombani na mtu bali tunagombaniwa. Angelielewa hili angejua namna ya kufaidika na pande zote mbili.
  2. Angeweza kushinda dili kubwa za kijamii na kiuchumi kwa kushikana mkono tu na viongozi mbalimbali, mfano kukutana tu na rais wa Marekani kungeweza kuishawishi marekani kuongeza fursa za watanzania wanaoenda Marekani kimasomo, hivyo hivyo kwa nchi za Ulaya.
  3. Hoja kwamba anabana matumizi ni propaganda na uongo wa wazi, kwani tunashuhudia jinsi ziara zake za ndani na hata wakati huu wa kampeni zinavyotumia rasilimali za umma kwa ajili ya ulinzi wake na kuwalipa kundi kubwa la watu anaotembea nao.
  4. Kazi ya urais ni kutoa dira na siyo kazi ya utendaji, hivyo haina ulazima eti lazima uwe ndani ya nchi 27/7, anayoyafanya John Magufuli ni working hard but not smart.
  5. Kwa kumalizia kutokuwa na exposure ya masuala ya dunia kwa John Magufuli kumelifanya Taifa kufikiri kijima, yaani ni kama tuko kwenye kupigania uhuru, si ajabu majina kama mabeberu na mengine mengi ya kibaguzi anapenda kuyatumia, akidhani bado anapigania uhuru. Dunia ya leo huwezi kufanikiwa ikiwa bado unaendekeza sera za aina ya Magufuli ambazo zinashabihiana kabisa na zile za Julius Malema wa Afrika ya Kusini ama hayati Robert Mugabe ambaye aliiharibu nchi iliyokuwa inaheshimika kiuchumi kusini mwa jangwa la Sahara.
TUNDU LISSU PEKEE NDIYE ANAYEWEZA KUIMARISHA UCHUMI WA TANZANIA HUKU AKIREJESHA DIPLOMASIA YA NCHI, TAREHE 28 OCTOBER 2020 MPIGIE KURA ILI AWE RAIS WA SITA WA NCHI YETU.

Enjoy your lunch if you can access any maana najua wengine humu hata chakula cha mchana leo hampati hii ni kutokana na Serikali ya CCM kubana kila kona si Sekta Binafsi ama ya Umma.
 
Mwambieni lissu atoke aende akansalimie robertison wa Amsterdam [emoji3]
 
Atoke nje kwani na yeye ana beberu wake huko kama alivyo mwenzie ambae ana yule amasterdam?

Kwanza atike njee kwani waziri wa mambo ya nje ana kazi gani?

Si nyie mlikuwa mna sema jk anakesha angani?
 
As if alienda sababu anapenda baada ya kupata matatizo?
 
As if alienda sababu anapenda baada ya kupata matatizo?
Kilichompata wote tunakilaani, na wote tunajua alienda kwa matatizo, lakini kitendo chake cha kurudi na beberu ndio tunachopinga.
 
Ukishaona hivyo juu huyo mtu akili ishaenda kutokana na yale aliyomfanyia mwenzake damuuuu damuuuu haijawahi mwacha mtu
 
Inawezekana huyu anadhani mwisho wa dunia utamkuta akiwa hai kwahiyo anadhani kutokwenda nchi za wenzako kujifunza ni ufahari.Aya hajaenda je kuna jipya lipi sasa latofauti ambalo wengine wanaoenda wameshindwa kulifanya.

Halafu mtu anasema kutokwenda nje ndo uzalendo wakati ukifwatilia unakuta zaidi ya asilimia 80 ya vitu anavyotumia vyote vimetoka uko nje ya nchi.Hii tafsiri ya uzalendo inapaswa kuangaliwa upya.
 
Huyu jamaa yetu ana phobia na lugha ya kiingereza.

Nina hakika washauri wamejaribu lakini imeshindikana.

Nakubaliana na hoja yako kwamba tunahitaji Rais atakayerudisha heshima ya Tz kimataifa.

Huyu wa sasa hivi hana uwezo wa kuwasiliana, na pia ana kauli ambazo zinaweza kuliaibisha taifa huko nje.

Hebu chukulia mfano aende huko nje halafu aanze kuongelea matiti ya kinamama kama alivyozungumza akiwa Singida. mnafikiri akifanya hivyo ktk kikao cha UN, au Davos, wenzake watamuelewa vipi na watatuchukuliaje waTz?
 
Kilichompata wote tunakilaani, na wote tunajua alienda kwa matatizo, lakini kitendo chake cha kurudi na beberu ndio tunachopinga.
Karudi na beberu yupi? Alipokelewa mwenyewe pale uwanja wa ndege akiwa mwenyewe.
Huyu beberu unaye mzungumzia alitokea wapi?
 
Back
Top Bottom