Hivi Rama Dee aliwakosea nini watanzania

Huyo ni msanii ambaye hajielewi au kwa kifupi unaweza kusema ni Nyumbu.Amejiingiza kwenye beef za kijinga na Media halafu anajikomba komba kwa Jide.Sasa Mwenzao Jide kaomba radhi ( Nadhani ni baada kuwa chini ya mchagaa Mosha anaejua namana kupata pesa )

- Sasa wale nyumbuwote waliokuwa na Jide nao wataomba msamaha au watakaza

- Watu wana vichwa vyao sijui kwanini hawavitumii, yaleyale ya kina Sugu - Ant Virus na Clouds.Sugu karudi Clouds Nyumbu wameshindwa wafanye nini.

- Ukiona mtu ana beef kuwa makini ,huwa ni suala la maslahi yake siku akiyapata utabaki kuonekana uliekuw unamuunga mkono ni bonge la mnafiki.
 
Tatizo jamaa ana mambo ya kike na ndio yamesababisha apotee kwenye game,aliingilia ugomvi wa Ruge na sugu sasa walivyo kuja kupatana yeye akabaki yupo yupo na ngoma zake cloud hawazigongi!
Ndio matatizo ya kuwa Nyumbu,unajiingiza kwenye beef bila kujua kilichofanya hao unaowatetea wakosane.Leo kina Sugu na Jide wameelewana na Clouds umebaki zoba hujui cha kufanya.Mungu alimuumba binadamu kila mtu na kichwa chake- hata kama utashauriwa na magwiji wa ushauri 99999999999999999999999999, bado unatakiwa kukaa chini kutmiakichwa chako kuamua maamuzi yako.Hizi tabia za kukabidhi kichwa kwa mtu ni tabia za ajabu sana hususani kwa mwanaume.
 
Mara ya kwanza kumsikia jamaa ni kwenye kibao chake cha Sio waoaji hao apo ndo nilipata kumsikia na kumfahamu jamaa anjua sio siri basi tuu wabongo hatuja pata kumuelewa labda kwa kua anaimba rnb soft sana kama zile za kina Joe tom akina Mario vasquez

Kipenda roho ndo best kwangu mimi kwa miondoka ya taratibu sioni kibao/track ya kibongo inacho kikaribia iyo ngoma kwa kweli..
 
Kikao cha family je
 
Aende label ya WCB, pale pana wasanii tu ila wanaonekana wanamuziki
 
Huyu jamaa anatabia za kijinga sana,ukiachilia mbali vita ya Ruge,na mpaka hivi juzi Ruge alisema kabisa kwenye XXL ya clouds kwamba Clouds hawawezi kamwe kucheza nyimbo za Ramadee!

Pia Ramadee ameingilia bifu la Diamond na Kiba hapo katikati,akaona haitoshi akaingilia siasa kati ya Chadema na CCM,kwa mkorogo huu ni lazima tu Jamaa apotezwe![emoji38]
 
jamaa anajua lakn kiukweli mi cjawah bahatika kuona nguvu zake katka kupromote kazizake, cjawai sikia redioni kwny tv akipromote kaz zake, hilo nalo ni tatizo, nyimbo zake ni nzuri lakn maranying tunaziskia kimizuka mizuka kama hv mtu kaleta uzi, bs ndo watu tunafunga safar mpaka youtube kuuangalia.
 
Kama muziki sauti Wema Sepetu angekuwa musician[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kiukweli jamaa anajua sana kuimba na tungo zake zimesimama vibaya sana...ila nadhan ana ulimbukeni wa kuleta harakati kwenye muziki...

in short, ana kipaji ila hana akili ya kutoka kimuziki na kimasoko...sijui kakulia bush gani huyu jamaa.
 
Unamuuliza msanii ambaye sijawai kuichukia Nyimbo yake
1: siyo waoaji hao
2: usiofie colour
3: Sarah
4: kama Huwezi
5: kipenda Roho
na nyinginezo dah huyu ni mwanamuziki
 
naamini tanzania kuna vituo vingi za radio na rulinga lakn why vinazidiwa na clouds msanii kma ana bifu na clouds bas kaz yko haitapata air tym xna coz ndo radio ina mashabiki wengi hasa vijana na age fulan hapa kat rama dee hana mahusiono mazur na clouds
 
Jamaa anajua sana mziki ....kuna ngoma yake moja inaitwa Siyo waoaji hao...bonge moja la wimbo ila sijajua nini kinasababisha jamaa asisikike kabisa
 
Kosa lake jingine ambalo linamuangamiza ni kuamini, ndoa yake na mzungu ndio kila kitu katika maisha yake huku anasahau kuendeleza kipaji chake. Sijajua kwa nn vijana wanaona deal kuoa wazungu eti kwa sababu ya kupata makaratasi ya kuishi ulaya huku wakisahau kupigania vipaji vyao, siku wakipigwa chini na hao wazungu sijui itakuwaje.
Kosa lake la pili ni kuingilia ugomvi usiowahusu (ugomvi wa sugu na ruge).Ukiangalia ugomvi wa sugu na ruge haukuwa kwa ajili ya kutetea maslai (walidhulumiana ela za wafadhili katika mradi wa marelia) ya mziki na wasanii, bali ulikuwa wa kutetea maslai yake mwenyewe sugu kwa kuwatumia wasanii wabongo fleva ili apate support, kwa kuanzisha anti-virus movement. Haya leo hii sugu na ruge wamepatana na uswahiba wao unazidi kuimarika, je wasanii bado hawanyonywi?,je wasanii hao walioanzisha hiyo movement wanapata airtime na show za kutosha?, jibu ni hapana mimi paka sasa nikiangalia mziki huu wa bongo fleva sijaiona effect yoyote ya anti-virus movement. Wasanii wote waliomsapoti sugu walitakiwa wajiulize, je hii vita tunaipigana kwa maslai ya nani, sisi pamoja na industry ya bongo fleva tutapata nini? Sasa hivi angalia mtu kama Rama dee mm mwenyewe namkubali sana na nyimbo ninayoikubali ni Ile aliyofanya na jide lkn haikupata airtime ya kutosha. Njoo kwa mapacha wako hoi wamezidiwa na msanii waliomkaribisha dar Joh makini wame kaa nae ghetto moja lkn leo wana wanalalamika njaa huku Joh anazidi kutusua. Ujue siku zote unapoingia ktk vita yoyote jiulize hii vita na pigana kwa maslai ya nani?
 
Uongoz mbovu wa mwanamzik ndo tatzo i mean management yake inashndwa mtangaza msanii wao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…