Hivi Serikali haioni kama Wananchi wanateseka na mfumuko wa Bei, kwanini haiondoi Tozo ili kuwapunguzia mzigo?

Hivi Serikali haioni kama Wananchi wanateseka na mfumuko wa Bei, kwanini haiondoi Tozo ili kuwapunguzia mzigo?

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Hivi jamani hii Serikali ya "Anayeupiga mwingi" haitambui kuwa wananchi wanateseka na hali mbaya ya maisha? mbona hatuoni juhudi za makusudi za kuwapunguzia mzigo mzito wa maisha ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kama chakula na vifaa vya ujenzi?

Badala ya kuwapunguzia wananchi mzigo mzito bado serikali ya CCM imekomalia kukusanya tozo mbalimbali hata kwa masikini hata kama ilisema imepunguza lakini hizo tozo hazimsaidii chochote mwananchi wa kawaida zaidi ya kumuongezea makali ya maisha.

Cha ajabu sasa pamoja na wingi wa matozo ya ajabu ajabu bado serikali yetu inazidi kukopa kila kukicha na fedha zinaenda maeneo ambayo hayana msaada wa moja kwa moja kwa wananchi. Ifike mahali serikali ifute tozo zote ikiwa ni mpango wa kupunguza ugumu wa maisha. Ikumbukwe tayari serikali imeacha kuweka ruzuku ya mafuta na hivyo kufanya bei za mafuta kuendelea kuwa juu.

Serikali iwaonee huruma wananchi wake wanateseka sana huku mataani.
 
Mkopo wa chanjo Trillion 2 tutalipa vipi bila tozo? Kinachoumiza hakuna hata aliyechoma hizo chanjo
 
Hivi jamani hii Serikali ya "Anayeupiga mwingi" haitambui kuwa wananchi wanateseka na hali mbaya ya maisha? mbona hatuoni juhudi za makusudi za kuwapunguzia mzigo mzito wa maisha ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kama chakula na vifaa vya ujenzi?
Jamani si tushakubaliana kwamba mama ni Bora kukiko bwana Yuule.

Mbona mwalalama mnatuchanga bure wenzenu
 
Ulifikiri kuitwa serikali ya CCM itakuonea huruma?
Mnadanganywa serikali ya wanyonge na inawapenda wananchi?
Sasa hivi 10,000 kama buku.
 
Hivi jamani hii Serikali ya "Anayeupiga mwingi" haitambui kuwa wananchi wanateseka na hali mbaya ya maisha? mbona hatuoni juhudi za makusudi za kuwapunguzia mzigo mzito wa maisha ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kama chakula na vifaa vya ujenzi?
Tumuombe mwenyezimungu afanye mambo yake Kwa hii serikali dhaifu atuondolee mmoja mmoja akianza na nape nitashukuru sanaa

Hapa utaongea wee hakuna anaekuskiliza tulirudishe Kwa muumba mwenyew awapige ata Ka Corona Ka Peke Yao Peke Yao tu
 
Hivi jamani hii Serikali ya "Anayeupiga mwingi" haitambui kuwa wananchi wanateseka na hali mbaya ya maisha? mbona hatuoni juhudi za makusudi za kuwapunguzia mzigo mzito wa maisha ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kama chakula na vifaa vya ujenzi?

Badala ya kuwapunguzia wananchi mzigo mzito bado serikali ya CCM imekomalia kukusanya tozo mbalimbali hata kwa masikini hata kama ilisema imepunguza lakini hizo tozo hazimsaidii chochote mwananchi wa kawaida zaidi ya kumuongezea makali ya maisha.

Cha ajabu sasa pamoja na wingi wa matozo ya ajabu ajabu bado serikali yetu inazidi kukopa kila kukicha na fedha zinaenda maeneo ambayo hayana msaada wa moja kwa moja kwa wananchi. Ifike mahali serikali ifute tozo zote ikiwa ni mpango wa kupunguza ugumu wa maisha. Ikumbukwe tayari serikali imeacha kuweka ruzuku ya mafuta na hivyo kufanya bei za mafuta kuendelea kuwa juu.

Serikali iwaonee huruma wananchi wake wanateseka sana huku mataani.

Haiwezi kuona bila sisi kuuvaa ujasiri wa kuionyesha hilo. Mbona tukiamua mambo yanakuwa safi hata kesho tu?
 
Basi mkae kimya watu watengeneza fweza
Unabidi umwambie mwanaccm mwenzako. Maana huko tunakoelekea ataanza kutembea anaongea mwenyewe
Mimi hizo bei nishazoea kwasasa, naona kawaida sana.
Huu muda wa mama, ndiyo wa kupiga hela kama hujui maana unauza kitu kwa bei unayotaka
 
Hivi jamani hii Serikali ya "Anayeupiga mwingi" haitambui kuwa wananchi wanateseka na hali mbaya ya maisha? mbona hatuoni juhudi za makusudi za kuwapunguzia mzigo mzito wa maisha ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa muhimu kama chakula na vifaa vya ujenzi?

Badala ya kuwapunguzia wananchi mzigo mzito bado serikali ya CCM imekomalia kukusanya tozo mbalimbali hata kwa masikini hata kama ilisema imepunguza lakini hizo tozo hazimsaidii chochote mwananchi wa kawaida zaidi ya kumuongezea makali ya maisha.

Cha ajabu sasa pamoja na wingi wa matozo ya ajabu ajabu bado serikali yetu inazidi kukopa kila kukicha na fedha zinaenda maeneo ambayo hayana msaada wa moja kwa moja kwa wananchi. Ifike mahali serikali ifute tozo zote ikiwa ni mpango wa kupunguza ugumu wa maisha. Ikumbukwe tayari serikali imeacha kuweka ruzuku ya mafuta na hivyo kufanya bei za mafuta kuendelea kuwa juu.

Serikali iwaonee huruma wananchi wake wanateseka sana huku mataani.
KWAHIYO MNATAKA MAISHA MAGUMU...YAHAME KUTOKA KWENU YAENDE KWA VIONGOZI...

BILA KODI ZENU WATAKULA NINI WAO?
 
Back
Top Bottom