Hivi shilingi 5, 10 na 20 zimefutwa kwenye matumizi?

Half Genious

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2017
Posts
491
Reaction score
784
Habari wadau nimejiuliza sana hivi shilingi 5,10 na 20 kupotea mataan nina weza kusema nina miaka kama mitatu sijaziona hela hizo na sijaona tangazo la serikali au BOT kuziondoa kwenye matumizi hela hizo naambiwa hata madukan hazikubaliki tena....sasa najiuliza zimefutwa au hazina thaman tena ya kufanya manunuzi...na pia kiuchumi hili limekaaje ikiwa america had leo wana Sent...vip sisi tunao anzia sh 50 tena hapo unanunua pipi tu.!

Karibuni
 
Jibu ni ndiyo mkuu hazina thamani..utanunua nini kwa shilingi 5, 10 au 20 sasa hivi?
 
Uzazi ukifika mwisho mbegu huonyesha huhitaji kwenda kupima hospitali au kusubiri tamko la mke wako.
 
Kwa hiyo tuna hali mbaya kwenye shilingi yetu au ni sawa hapa tulipo.!?
 
Jibu ni ndiyo mkuu hazina thamani..utanunua nini kwa shilingi 5, 10 au 20 sasa hivi?
Mnaposema hela hizo haziwezi nunua kitu mnamaana gani? Ikiwa sh 100 unapewa pipi tano maana yake pipi moja ni sh 20. Au kiberiti sh 50 maana yake ni 20+20+10, ambayo ni sawa na mtu atumie sh 2000+2000+1000 kununua shati la sh 5000.

Bado vipo vitu unaweza nunua kwa kutumia hiyo sh 20 pekee. Mfano bomba la kijiji fulani huko Mpanda ndoo moja ya maji ni sh 20 ila watu hulazimika kununua ndoo 5 na kulipa sh 100.

Labda sababu watu twaona shida kubeba mzigo wa "vichele"

Kama BOT hawajaongea lolote hizo bado ni hela halali
HAZIJAFUTWA MKUU ILA HAKUNA CHA KUNUNUA
 
Japo Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya uchumi lakini nafikiri kupotea kwa hizi sarafu ndogo hasa sh 5, 20 ni matokeo ya fedha yetu kuzidi kushuka thamani. Siku hizi hata elfu kumi ukichange inathamani ndogo sana
 
Toka uhuru hakuna pesa iliyofutwa hata sasa. Mpaka thumni unaweza kuitumia kwa sasa.

Kama unahitaji kitu cha shilingi 100, na huku una sarafu za shilingi ishirini tano, basi unaweza kuzitumia zote hizo kununua unachokitaka.

Hii nilimsikia ofisa mmoja wa BOT akifafanua hili hapo nyuma.
 
Mleta mada atakua mtu wa dodoma huyu,
Manake huko chechi ya buku 5 tu hadi benki[emoji3]
 
ndio ni halali natambua mkuu
 
Mpaka centi tano inatumika ile ya samaki jelly fish ila watu wanaona in mzigo kubeba mzigo wa sarafu hizo.
Fikiria unaenda benki kudraw laki mbili halafu upewew mzigo wa shs tanotano, achilia mbali uzito wake, hata kuzihesabu tu ni shida.
Mimi nikichukua milioni mbili tu akinipa note ya alfualfu huwa napata taabu sana, sembuse senti hamsini za kasungura.
Zipo zinatumika ila ziko kwenye mahesabu tu.

Rejea bajeti za serikali utakuta vijisenti vipo tu
 
Swala langu ni kupotea sarafu hizo kama bado zipo kwenye matumiz nimi chanzo kupotea kwa sarafu hizo ma wafanya biashara hawazitaki...tunajua kwenye sarafu ya mia kuna 20 tan na 10 kumi lakin hata kwenye not ya elfu ya moja kuna 100 kumi lakin sh 100 na sh 1000 zote zipo kwenye mzuguko so swala la hoja ya kusema zipo ila zinajumishwa kwenye sarafu kunwa sion kama ina mshiko.!.. Kuna mtu kasema ndo ya maji Rukwa ni sh 20 lakin ukitaka maji unatoa.100 ili upate ndoo tano je kama nataka ndoo mbili ntapata wapi chenj yangu.!
 
Hizi sarafu sh 5, 10 na 20, ( pia sh 50) zinapoteza thamani kwa sababu in one way or other mamlaka za kusimamia bei za bidhaa hazitimizi wajibu.
Wafanyabiashara wanajipangia bei watakavyo na raia wakilalamika hakuna mamlaka inayochukua hatua! Mfano ni hivi, bidhaa inayotakiwa kuuzwa kihalali Tsh 40, muuzaji atalazimisha iwe sh 50 ili asisumbuke kurudisha chenji ya sh 10 (ambapo sarafu za sh 10 zinapatikana bank ila wauzaji wa retail hawapendi kwenda kuziomba kwa hiyo zinaadimika mtaani)
Kadhalika nauli ya daladala halali ikiwa sh 450, kondakta atalazimisha iwe Tsh 500 kwa kisingizio cha kukosa change!
Hivi sasa, bidhaa ya sh 900, usishangae ukalazimishwa kulipa 1000! Au ile ya 1400 ukalazimika kulipa 1500! Kisingizio sh 100 ya kukurudishia hamna. Na kwa kuwa waTz ni wapole sana basi very soon itakuwa ni kawaida, na hatimaye sarafu za 100 nazo zitaadimika kama zile za 5, 10, 20, (na 50 baadhi ya maeneo)
 
Bado zinafanya kaz; angalia bei hizi:

Printing
Mabibo Hostel sh.70@page

Copy sh.20@page
 

Hiyo maaana yako haina maana japo inamaana...nenda sasa ivi dukani kanunue kitu cha thamani ya tshs 20 toa tshs 50 iliurudishiwe tshs 30...kwa umoja wa kitu hicho hakuna japo kwa wingi wake utapata ivory 5 au bublish kwa tsh 100...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…