Hivi tumeshindwa kumbaini aliyepandikiza magugu ziwa Viktoria ayaondoe Kwa gharama zake?

Magugu maji hutokea kutokana na kuzidi Kwa virutubisho vya nitrogen na phosphorus ndani ya maji (eutrophication), chanzo Cha virutubisho hivi ni kutokana na vinyesi vya wanyama (akiwemo binadamu) kuingizwa majini (Sewage system directed into water bodies).

Ukiangalia Kwa upande wa ziwa Victoria, makazi kuzunguka ziwa Hilo hayana mfumo mzuri wa vyoo. Hivyo wakati wa mvua inasemekana flushing hufanyika kuelekezwa ziwani. Hivyo kuongeza virutubisho (nutrients content), na kupelekea magugu maji ndani ya maji.

Faida za magugumaji Kwa samaki.
1.Husaidia kujificha Kwa baadhi ya samaki pindi wanapowindwa
2.Hutoa kivuli na sehemu za kupumzika Kwa samaki.
3.Baadhi ya samaki(Egg beater) hutumia magugumaji kutengeneza viota vya kutagia mayai.
4.Ni sehemu mhimu ya kukuzia vitoto vya samaki (Nursery grounds)

Hasara za magugumaji.
1.Hupelekea upungufu wa oksijeni (Hypoxic and anoxic condition) kutokana na ushindani wa matumizi,
2.Hupunguza uangavu wa maji(water clarity) na kupelekea kupungua kiwango Cha mwanga jua kufikia viumbe maji.
3.Hupunguza uzuri wa mazingira ya majini na huduma zingine (water beauty and amenity)
 
Miaka ya 90 mwishoni yaliibuka kwa wingi sana ikawa habari kubwa ziwa Victoria. yameota tena. Kumbuka kila mmea una mbegu yake inayoweza kusambazwa na ndege upepo, mkondo wa maji n.k.
Ndege atoke Amerika ya kusaini atuletee magugu maji?
 
Magugu maji yameharibu sana mwonekano wa ziwa nyanza.

Hii ya kusema, chanzo Cha magugu ni maji tiririka Toka vyooni, umeitoa wapi?
 
Mkuu, unafahamu kuwa kuna mienendo ya ndege, kuwa wakati wa baridi kali ulaya wanahamia bara la Africa?
Mfano ndege yupi aliyetoka America ya kusinni akafika ziwa nyanza?
 
Ndivyo ilivyo mkuu,
Ziwa Nyasa na Tanganyika hamna vitu kama hivyo, kutokana na mazingira kuzunguka maziwa hayo.
Nyasa na Tanganyika hakuna vyoo na kemikali zinazotiririka ziwani?

Tutafiti zaidi, nadhani Kuna zaidi ya hapo!!
 
Wewe ni MPUMBAVU, unapewa majibu sahihi kuhusu chanzo cha magugu maji wewe umekazania kuwa yamepandikizwa na watu.
Nenda mto Kagera uone ulivyozungukwa na magugu maji kwenye kingo zake.Ziwa Victoria magugu maji yamekuwepo tangu miaka na miaka na sio jambo jipya kama unavyotaka kuaminisha watu hapa.
Nimezaliwa na kukulia kwenye visiwa vya ziwa Victoria so najua ninachokisema.
 
Una Elimu ya darasani kiwango kipi?

Samahani lakini!!
 
Project za watu hizo.
 
Mimi nilijua magugu maji ndio kuongeza kasi ya kuzaliana samaki.
Ok, hiyo ni nature msimtafute mchawi
 
Jadili mada uliyoileta.Huu upumbavu wa kukwepesha mada wafanyie wapumbavu wenzio.
Ni vizuri nikajua kiwango Cha Elimu Yako,

Kuishi karibu na ziwa, Si kujua Kila kitu,

Inawezekana umezaliwa na kuwakuta sangara ziwani, lakini ukiambiwa kuwa zamani hapakuwapo na sangara ziwa NYANZA, walipandikizwa, unaweza kubisha.

Jitahidi kusoma comment za Walio kutangulia Ili uwe kwenye position nzuri ya Kutoa mchango uliosheheni.

Karibu🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…