Hivi tunahitaji Katiba Mpya au Mjadala juu ya Katiba Mpya?

Hivi tunahitaji Katiba Mpya au Mjadala juu ya Katiba Mpya?

ChiefmTz

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2008
Posts
2,937
Reaction score
942
Wana jf, hivi kwa sasa tunahitaji Katiba mpya kwanza au tunahitaji kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba mpya. Nimeulilza hivi kwa sababu kuna watu wanataka tudai Katiba Mpya bila ya kujali kuwa hakujawahi kuwepo kwa mjadala rasmi juu ya Katiba mpya. Tusipoiona haja ya kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba, watatokea wajanja ambao watapeleka Mswada Bungeni wa kutaka Katiba mpya na ukakubaliwa na ikaundwa Katiba nyingine hata kama ni kwa jina tu. Lakini tukidai mjadala rasmi, sio rahisi kuchezewa shele. Nawasilisha
 
Wana jf, hivi kwa sasa tunahitaji Katiba mpya kwanza au tunahitaji kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba mpya. Nimeulilza hivi kwa sababu kuna watu wanataka tudai Katiba Mpya bila ya kujali kuwa hakujawahi kuwepo kwa mjadala rasmi juu ya Katiba mpya. Tusipoiona haja ya kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba, watatokea wajanja ambao watapeleka Mswada Bungeni wa kutaka Katiba mpya na ukakubaliwa na ikaundwa Katiba nyingine hata kama ni kwa jina tu. Lakini tukidai mjadala rasmi, sio rahisi kuchezewa shele. Nawasilisha

Tufafanulie juu ya huo "mjadala rasmi" ukoje ili nikujibu swali lako!
 
Tufafanulie juu ya huo "mjadala rasmi" ukoje ili nikujibu swali lako!

Labda anataka tujihakikishie contents za katiba mpya zitakua nini ili tusije andika kijarida badala ya Katiba. Maana mawazo na madai ya katiba mpya kwa wakati huu ni kuitoa CCM madarakani. supposed imewezekana than what next? na walioshindwa wadai katiba mpya ya kukiondoa hicho chama kingine madarakani? Katiba iwe futuristic with long lasting ideas!
 
Kwa maoni yangu ni wananchi ndio wana final say juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa katiba mpya.kufikia huko ni lazima kuwe na mjadala rasmi utakaohusisha pande mbalimbali.
Serikali itakapokubali kujadili suala hili ndipo tutakapoita 'mjadala rasmi'
 
Jiulize utapataje Katiba mpya bila mjadala? Mchakato lazima uanze na mjadala. Hivyo upatikanaji wa Katiba unamaanisha mjadala ulikuwepo!
 
Labda anataka tujihakikishie contents za katiba mpya zitakua nini ili tusije andika kijarida badala ya Katiba. Maana mawazo na madai ya katiba mpya kwa wakati huu ni kuitoa CCM madarakani. supposed imewezekana than what next? na walioshindwa wadai katiba mpya ya kukiondoa hicho chama kingine madarakani? Katiba iwe futuristic with long lasting ideas!
Lakini pia itatusaidia kukubaliana mambo ya msingi.
 
Kwa maoni yangu ni wananchi ndio wana final say juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa katiba mpya.kufikia huko ni lazima kuwe na mjadala rasmi utakaohusisha pande mbalimbali. Serikali itakapokubali kujadili suala hili ndipo tutakapoita 'mjadala rasmi'
Ahsante Mkuu kwa kutokuwa Kipofu wa kuona ukweli. Jambo la msingi ni kuishinikiza gvt kuandaa na kuruhusu vikao kwa ajili ya kujadili Katiba.
 
Wana jf, hivi kwa sasa tunahitaji Katiba mpya kwanza au tunahitaji kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba mpya. Nimeulilza hivi kwa sababu kuna watu wanataka tudai Katiba Mpya bila ya kujali kuwa hakujawahi kuwepo kwa mjadala rasmi juu ya Katiba mpya. Tusipoiona haja ya kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba, watatokea wajanja ambao watapeleka Mswada Bungeni wa kutaka Katiba mpya na ukakubaliwa na ikaundwa Katiba nyingine hata kama ni kwa jina tu. Lakini tukidai mjadala rasmi, sio rahisi kuchezewa shele. Nawasilisha

mkuu... kuna mjadala mwingine tena zaidi ya huu tunaoufanya hapa JF na huko mitaani....... kitakacho fuata ni mchakato wa upataji wa katiba mpya.....
 
mkuu... kuna mjadala mwingine tena zaidi ya huu tunaoufanya hapa JF na huko mitaani....... kitakacho fuata ni mchakato wa upataji wa katiba mpya.....
Mjadala tunaofanya sio rasmi na hauna hata muhtasari ambao tunaweza kuutumia kama reference.
 
Mjadala tunaofanya sio rasmi na hauna hata muhtasari ambao tunaweza kuutumia kama reference.

mkuu i agree... but what is more important are the contents and then all of that procedures can follow smooth..... suppose the contents for the need of a new draft constitution are not sufficient and healthier enough to pave way for the drafting a new constitution; we need to brainstorm and not neccessarily formal..... but also we need oral discussions and measure the pro's and con's
 
From my understanding I think we need both 2 steps,na tayari moja wananchi wameanza ambayo inangojewa sasa kuwa rasmi kwa kupokelewa na mamlaka then tuendelee
 
Back
Top Bottom