sajo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 3,474
- 6,195
Kinachofanya ukopwe fedha nyingi au chache (kulingana na mtu unavyoona kuwa ni nyingi au chache) ni kiwango cha mshahara unaochukua kwenda nacho nyumbani (net salary) na sio kiwango cha mafao yako, mikopo ya watumishi dhamana ni mshahara, pensheni ni moja ya sehemu tu lakini mfuko wa jamii kama haukushirikishwa katika mapatano ya huo mkopo wenu unaweza kukataa kumpa mdai sehemu ya fedha za mtumishi kwa kuwa mahusiano ni kati ya mfuko na mtumishi na sio watu wengine, labda kama watakuja na amri ya mahakamaMkuu kuna vigezo vya kupewa ndio maana wanaomba barua ya kuthibitishwa kazini ,miaka uliyofanya kazi na kiwango chako cha mshahara kwa mwezi kifupi huwezi pata mkopo unaozidi mafao yako