Hivi Ulaya kuna utaratibu wa kuulizwa jina la balozi wa mtaa/mtendaji kata, diwani au mbunge ili kuthibitisha kama ni mkazi wa sehemu husika?

Kwahiyo mtu ukiwa sio mkazi wa sehemu husika ndio unakua mtu mbaya au huruhusiwi kupita sehemu hiyo?
 
Ukifikiria kwa mihemko huwezi kuuona umuhimu wa huo mfumo lakini ni muhimu sana.

Hatuwezi kuishi kama mifugo lazima kuishi kwa utaratibu, watu kama wewe inaonekana wazi pesa ya ulinzi huchangii, pesa ya takataka huchangii pia.

Humjui, mjumbe, hujui Mwenyekiti, hujui Diwani sasa unaishi kama mdudu?

Italy ukienda kwa visiting viza ni lazima ukarepoti police station kwenye eneo utakalofikia wanakuwa wanajuwa wana Mgeni eneo lao.
 
Kuishi kwa utaratibu ni kumjua Mwenyekiti?? Jiji ni tofauti na kijiji kwa number ya watu wanaoingia na kutoka ni kubwa.

Kumjua Mwenyekiti kunatokana na sababu mfano unataka cheti cha kuzaliwa cha watoto, mhuri au mkopo so i guess nikipata reasons za kumtafuta ndio siku nitakayomjua.
 
huko ulaya na america wameendelea sana kila kitu kipo online sura tu ikipigwa picha inatoa taarifa zako zooote..
bado tunasafari ndefu sana kuwakuta...
 
Kama lengo lako ni ligi basi endelea tu na ligi Mimi siwezi.

Ukiishi urban area au town kwenye maapartment huko au prime area kama Masaki huna haja wala sababu ya kuwajuwa hao watu sijui mjumbe wa nyumba kumi wala Mwenyekiti.

Lakini kama unakaa uswahilini hilo ni jambo la lazima kwako, kama huelewi basi endelea kushupaza shingo tu.
 
Ingawa tutaona hao waliomuweka mtu kati tukawaona kama wajinga lakini hili jambo lina umuhimu wake.

Mimi nilikuwa na tabia ya kukaa sehemu hata mtaa siujui unaitwaje, ila kuna siku sikumbuki nilitoka wapi mida ya saa tano usiku uwezi amini nilikuwa nataka bodaboda wa kunipeleka nyumbani ila nikashindwa kujieleza mtaa wote walinikataa wakijua kwamba nitakuwa sio mtu mzuri.

NB:KUNA MAMBO MADOGO SANA UKIYATAZAMA ILA YANAWEZA LETA UGUMU UKIWA NA SHIDA.
 
Kwa kifupi tu kama mfumo huu huuwezi basi hakikisha hukai uswahilini.
 
Yes. Tena ulaya, kuna baadhi ya nchi kama ubelgiji hata ukitaka kujenga jengo kubwa ramani yake lazima ikabandikwe ofisi ya mtaa. Raia wakiona jengo lako lina sura mbaya halitapendezesha mtaa wao wanakataa na utalazimika ubadilishe ramani mpaka waikubali ndipo unapewa kibali cha ujenzi.
 
Kwa kawaida ni lazima raia amfahamu mjumbe wake wa nyumba kumi.

Pili, ni lazima amfahamu mwenyekiti wa serikali ya mtaa na ofisi yake ilipo.

Hiyo ni kwa Tanzania na hizo ni hatua za awali za kutambuliwa endapo utataka kitambulisho cha taifa, kufungua akaunti benki na mambo mengine muhimu.

Kwa ughaibuni huwa wahitaji uwe na kielelezeo cha uthibitisho wa anuani au makazi yako wenyewe huita "Proof of Address" kama barua yoyote yenye kuonyesha jina lako na mtaa unoishi na namba ya nyumba na siku hizi hutumia leseni ya udereva.

Ujerumani hutakiwa kubeba kitambulisho ambacho chaweza kuulizwa wakati wowote na polisi uwapo kitaa au wakiwa na mashaka nawe.

Nchi zingine za Ulaya kama Uingereza na Marekani, polisi wakikusimamisha ama uwe waendesha gari au barabarani kitu cha kwanza kabisa kukuuliza ni ID au leseni ya udereva ambayo itaonyesha anuani au Address ya mahali unapoishi.

Lakini vitu hivi vyote wewe raia huvitoa tu iwapo polisi au askari kanzu kakuzukia na afanya uchunguzi wake au umekuwa suspect.

Ulaya na Marekani raia wa kawaida hana mamlaka ya kudai anuani ya unapoishi wala uraia wako.

Hivyo hao walokusimamisha huko kwenye vichochoro walikuwa na ajenda yao ingine.
 
Acha dharau - lazima uwajue majirani zako. Kwa mila na tamaduni za watanzania jirani ndiye mtu wa kwanza kukusaidia katika shida na raha. Huko Ulaya mtu mweusi anaweza kuuwawa kwa kukosea na kupita mtaa wa wazungu watupu. Jirani yako akiwa na tatizo na wewe, kitu cha kwanza atakupeleka kwa mjumbe wa mtaa, watu wengi hawana vitambulisho kwahiyo kujua majina ya Viongozi wa chini ndiyo suluhu yao.
 
Dharau tena kivipi? Majirani nawajua.
 
Mkuu, si kweli usemayo kwamba wazungu wanaweza kukuua endapo wakosea kupita kwenye kitaa chao kwani mambo hayo yalikuwepo zamani lakini siku hizi yapotea sana.

Isipokuwa ipo mitaa ya wazungu halisi yaani wale wasopenda wageni ambao huwaita "strangers" mingi ina mifumo ya CCTV nje ya nyumba zao na pia kitaa wana mfumo wauita "neighbourhood watch"

Mara nyingi huamua kukufualitia na kupigiana simu kwa kutumia mfumo wa "neighbourhood watch"ili kufahamu ni nyumba ipi waingia.

Wakikuona waishia kwingine hukuacha lakini wakikuona siku ya pili na ya tatu basi hupiga tu simu polisi ambao ndo wenye mamlaka ya kukusimamisha na kuuuliza ID yako na kufahamu una malengo gani na kitaa kile.
 
Muwe mnamiliki hata IST na kuendesha kuepukana na upuuzi kama huu.ī
 
Ulaya ni Ulaya Afrika ni Afrika siyo vyote vya Ulaya vinafaa Afrika na si kila vya Afrika vinafaa Ulaya. Tz jirani akifiwa ni msiba mkubwa wa Mtaa ila Ulaya ni biashara kwa kampuni Ulaya ukifirwa ni jambo la kawaida ila Tz utazomewa kila kichochoro.
Hii Tz utake usitake lazima tukujue kwa undani kwa asili ndipo upelelezi ndipo Ulipozaliwa. Tupo zetu kitaa ikifika usiku huingii mtaani kama hujulikani maana utahojiwa na sungusungu mpaka asili ya ukoo wako wakishindwa kukujua wanaita Njagu .Kwa ufupi ndiyo Usalama wetu
Alijichanganya jamaa mmoja akahamia mtaani akiwa anamiliki shoga yaani Nyumba ilizungukwa na Wanamtaa na kuanza kushambuliwa na mawe Mpaka walipokuja manjagu kuwanusuru.

Hii ndiyo raha ya Tz.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…