Hivi unaweza kuwa na akili timamu ukakubali baba yako mzazi auze samaki akiwa na umri wa miaka 92 na ukakubali alalie mkeka?

Utalalia mkeka na kuuza samaki hata ukiwa na miaka 200, kama kazi yako itakua kuzalisha wanawake na kuwatelekeza halafu kutwa kupiga domo mtandaoni kuwatukana single maza.
Jukumu la kuwa na maisha mazuri ni wewe mwenyewe mzazi (baba). Huwezi kuwalaumu watoto wakujengee nyumba na kukupa maisha mazuri wakati wewe kipindi cha ujana wako ulishindwa kutengeneza maisha mazuri. Kuwa na watoto siyo kigezo cha mwanaume kuwa masikini (tengeneza kipato)
Watu hasa sisi wanaume tukiwa kwenye ujana tunaendekeza, pombe, wanawake na anasa zisizo na maana. Mimi kama mwanaume siwezi kuwategemea watoto wanipe maisha mazuri hilo ni jukumu langu
 
Ndo maana mungu anakubariki kila Leo hongera
 
Hii nimeiona pia katika upande wa Mama ujombani .

Babu yangu ulikuwa ukienda kumtembelea unamkuta anaishi maisha magumu Sana.

Na uwezo wa kumsapoti walikuwa nao huwa sielewi baadhi ya familia zina nini.


Mimi mzee wangu siwezi kukubali afike hiyo hatua achilia Mbali kukaa Nyumba Kama hiyo.

Itakuwa aina maana ya sisi kufanya Kazi.
 
Tatizo wazee wanazalisha tu,mtu amezaa watoto 18 mama tofauti tofauti kuwalea changamoto, watoto wanaishia kujilea hawamjui baba wala mama,Mungu akijaalia watoto wakifananikiwa ndio unakuta Wazazi wanajitokeza kusiko julikana
Ipo sana kanda ya ziwa hii tabia
 

Ni Laana hizo.
Ukisikia Laana ndio hizo Sasa
 
Ni Laana hizo.
Ukisikia Laana ndio hizo Sasa

Laana ya aina gani na inaitwaje ?

Maana I remember Bibi yangu mzaa Baba mpaka anakufa alikuwa akiisafiri dunia na kula bata kwa pesa. Za watoto wake. Ila kwa upande wa Mama ujombani wazazi wao wanakula msoto mkali Sana , kitu ambacho huwa nikifirikia naona something is wrong.

Mtu kutonsapoti mzazi inafikirisha.

So what the kind of curse?
 
Wewe mzee wako hakukutelekeza ndiyo maana ulikuwa na roho hiyo(hukumuona ujana wake alikuwaje)
Ni kweli hakunitelekeza kabisa Ila sasa mbona hata kaka zangu na wao walilelewa vizuri tu tena wao walilelewa na Mzee enzi ambazo Mzee alikuwa na nguvu lakini hawajamsaidia.
Watoto wengine ni majanga tu ndugu zangu tuombe Mungu atupe watoto wema
 

Moja ya dalili ya kuwa mtu analaana ni kushindwa kusapoti au Kusaidia watu wake, wa nyumbani kwake yaani Wazazi, watoto wakati anauwezo wa kufanya hivyo.

Laana zipo za aina nyingi.
Kuna Laana za umri, yaani watu Kufa kabla ya kuzeeka. Na zina Sababu.
Kuna Laana za mahusiano ya Familia. Yaani mtu kuoa au Kuolewa lakini kuachwa au kuacha. Ndoa kutokuwa na Amani. Hizo ni Laana zote.

Mtu kuwa na hasira za Baba au mama yake, au watoto kuwa na hasira na wewe mzazi. Hizo ni Laana.

Unaweza ukafanikiwa kuwa tajiri lakini Moja Kwa Moja ukajiona unalaana maana maisha yako unayaona hayana furaha. Mtu wa kuhangaika, kutangatanga, kugombana gombana na ndugu, jamaa na marafiki
Hizo ni Laana zote

Huwezi kuwa na furaha wakati mzazi wako aliyekuzaa, watoto wako uliowazaa, au ndugu zako wanahitaji msaada wako alafu wewe kwa makusudi huwapi huo msaada. Hiyo ni Laana.
 
Wengine huwa wanapitia kipindi cha Masahihishi kwa yaliyoyafanya au kuwafanyia watu enzi za ujana wao.
Ila sijasemea ndio huyu Mzee ila wengine huwa n kipindi chao cha masahihisho
 
🙏🏽🙏🏽🙏🏽 I learn barikiwa
 
🙏🏽🙏🏽🙏🏽 I learn barikiwa

Kuna watu hawa wakukosee vipi lazima uwasamehe.
Msamaha ni Moja ya Njia kuu za kufuta Laana.

Mzazi
Mtoto
Ndugu
Mke(kama hajafanya kosa la ku-cheat)
Hao lazima usamehe ili kuondoa Laana kwenye Familia.

1. Kisa cha Rejea
Yusufu alipotaka kuuawa, kisha kuuzwa na ndugu zake.
Mwisho wa siku alifanikiwa, akasamehe ndugu zake ingawaje hakuwaweka karibu Sana, aliwatafutia eneo zuri la malisho, huko Gosheni. Ili wakafuge mifugo na kulima huko. Huku yeye akibaki IKULU.

Ile ndio ilikuwa Nafasi nzuri ya yeye kulipa Kisasi lakini hakufanya hivyo.
Laana ya kuuzana ndani ya Israel ilikomeshwa na Yusufu.

Kama Yusufu angebaki na Kinyongo Mpake Leo Wayahudi wangekuwa wanasalitiana wao kwa Watu wengine(mataifa mengine)
Lakini Hilo kwa sasa hakipo.
Wayahudi wanasalitiana wao kwa wao au kugombana wao kwa wao lakini kuuzana au kujiunga na mmataifa ili amuuze mwenzake Hilo utasubiri Sana.

Rejea Kwa Musa alipozaliwa na kukulia jumbo la kifalme la Wamisri lakini hakuwasaliti ndugu zake.
Rejea Kisa cha Malkia Esther


Lakini Mtu ametelekezwa na Baba yake au Mama yake hakuwa Responsible Sana kwake. Mtoto akishafanikiwa badala amsamehe mzazi wake hata asipomuweka karibu lakini kumsaidia na kumpa Ile hadhi yake hataki, anataka kumkomesha.
Hiyo Laana inatembea kizazi hata kizazi.

Watu wasameheane
 
Hao watoto live live bila kumung’unya maneno wana laana siyo bure.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…