Hivi ushawahi kukutana na hii?

Hivi ushawahi kukutana na hii?

Leejay49

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2023
Posts
16,388
Reaction score
51,970
Hope Jumapili iko njema kwa wote,. Kwa ambao hamko sawa nawaombea mrejee kwenye hali zenu za kawaida..

Iko hivi, imi hua nakutana na hii kitu sijui niiwekaje,. Yaani unakuta maybe mtu ana shida na kitu fulani labda kuelekezwa au kumpatia namna ya kukipata au kukijua. Na ninao uwezo labda wa kumwelekeza na kitu nakijua vizuri kabisa ila nakua naogopa je nitaonekanaje au atanifikiriaje baada ya kumwambia maana vitu vingine unakuta nimevijua kwa namna za ajabu sana. Nitaweka mifano kadhaa.

1. Kuna siku mzee (baba yangu) nilikua namsikia anaongea na watu tofauti tofauti kwenye simu almost kama saa zima, anaulizia kama kuna mtu ana namba ya mtu fulani ambaye ni kiongozi mkubwa tu kwa nafasi yake. Alimuuliza hadi mama na marafiki zake wote hakuna aliyekua nayo. To be honest, namba nilikuwa nayo na nilitoka kuongea nae hata siku mbili hazijaisha lakini sasa nikawaza nikisema nimpe enhe nikiulizwa ilikuwaje nikapata namba yake na hua naongea nae nini, maana kama urafiki ni suala lisilowezekana ni mtu mzima,. Kwakweli sikumpa nilimwacha tu ahangaike maana sikua na maelezo endapo ningeulizwa maswali kama hayo🌚

2. Kuna siku dada yangu alikua na shughuli (send off) na kuna marafiki zake wa kutoka mbali walikua wanakuja ilibidi awatafutie hotel maana nyumbani kulikua na watu wengi sana, na kwa status yao kufikia lodge au guest ilikua haipendezi. Sasa kwenye ile conversation walikua wanaulizana na mama ni hotel gani nzuri na gharama zake na vitu kama hivyo,. Walikua wanaulizia kama kuna mtu ana mawasiliano yao ya uhakika waulize vitu kama hivyo maana kutoka nyumbani mpaka zilipo kuna kaumbali kidogo halafu ukizingatia ni usiku,. Walihangaika wee hawakufanikiwa.

Ila kwakweli hizo taarifa zote nilikua nazo yaani hizo hotel walizotaja nilikua najua gharama zao zote za accomodation, mazingira, hadhi zao hata wangetaka picha ningewapa. Kuna baadhi ya wahudumu nilikua nafahamiana nao, yaani kiufupi details zote nilikua nazo hadi menu lists zao ila sasa naanzaje kusema😃. Nikiulizwa nimejuaje yote hayo na nilikua naenda lini na nani kufanya nini? Kwakweli majibu nilikua sina Maana sijawahi kuaga nyumbani naenda sehemu kama hizo, na mda wote wanajua niko kazini kama sio kanisani au nyumbani,. Kwakweli niliwaacha tubwahangaike hadi asubuhi wakaenda wenyewe,.

3. Hii hapa kuna siku nilikua niko na Jamaa (mpenzi wangu) kuna mahali nilimsindikiza kwenye kikao wakati wa kurudi tukapitia mahali kula,. Asa eneo tulilopark gari ni eneo ambalo nalifaham vizuri tu na kuna magari kama matatu hivi Alphard yalikua yamepakiwa kwa pembeni na wenye hayo nawafahamu vizuri tu, si nikaropoka bhana “Haya magari haya yamepark hapa saizi lazima tu kuna watu wananjunjana“ akastuka mmmh, akaanza kunihoji umejuaje wewe na haya magari yana tinted nikabaki kujiuma uma tu nikapotezea mada. Kiukweli najua sana na ushahidi ninao lakini sasa namna niliyojua jua inatatanisha kiasi kwamba nilionekana sina maana siku ile🥹😔 lakini tu najua ila sijui.

Matukio ni mengi jamani mikono imechoka kuandika. Tuambie na wewe kama inakukutaga hii tusimulie sisi hatukufaham hutapata shida😬
 
Hope Jumapili iko njema kwa wote,. Kwa ambao hamko sawa nawaombea mrejee kwenye hali zenu za kawaida..

Iko hivi,. Mimi hua nakutana na hii kitu sijui niiwekaje,. Yaani unakuta maybe mtu ana shida na kitu fulani labda kuelekezwa au kumpatia namna ya kukipata au kukijua,. Na ninao uwezo labda wa kumwelekeza na kitu nakijua vizuri kabisa ila nakua naogopa je nitaonekanaje au atanifikiriaje baada ya kumwambia maana vitu vingine unakuta nimevijua kwa namna za ajabu sana,.. Nitaweka mifano kadhaa

1.. Kuna siku mzee( baba yangu ) nilikua namsikia anaongea na watu tofauti tofauti kwenye simu almost kama saa zima,. Anaulizia kama kuna mtu ana namba ya mtu fulani ambaye ni kiongozi mkubwa tu kwa nafasi yake,. Alimuuliza hadi mama na marafiki zake wote hakuna aliyekua nayo,. To be honest namba nilikuwa nayo na nilitoka kuongea nae hata siku mbili hazijaisha lakini sasa nikawaza nikisema nimpe enhe nikiulizwa ilikuwaje nikapata namba yake na hua naongea nae nini,. Maana kama urafiki ni suala lisilowezekana ni mtu mzima,. Kwakweli sikumpa nilimwacha tu ahangaike maana sikua na maelezo endapo ningeulizwa maswali kama hayo🌚

2. Kuna siku dada yangu alikua na shughuli ( send off ) na kuna marafiki zake wa kutoka mbali walikua wanakuja ilibidi awatafutie hotel maana nyumbani kulikua na watu wengi sana,. Na kwa status yao kufikia lodge au guest ilikua haipendezi,. Sasa kwenye ile conversation walikua wanaulizana na mama ni hotel gani nzuri na gharama zake na vitu kama hivyo,. Walikua wanaulizia kama kuna mtu ana mawasiliano yao ya uhakika waulize vitu kama hivyo maana kutoka nyumbani mpaka zilipo kuna kaumbali kidogo halafu ukizingatia ni usiku,. Walihangaika wee hawakufanikiwa,.
Ila kwakweli hizo taarifa zote nilikua nazo yaani hizo hotel walizotaja nilikua najua gharama zao zote za accomodation,,. Mazingira, hadhi zao hata wangetaka picha ningewapa,. Kuna baadhi ya wahudumu nilikua nafahamiana nao,. Yaani kiufupi details zote nilikua nazo hadi menu lists zao na bei za vyakula vyao vyotee. ila sasa naanzaje kusema😃,. Nikiulizwa nimejuaje yote hayo na nilikua naenda lini na nani kufanya nini? Kwakweli majibu nilikua sina Maana sijawahi kuaga nyumbani naenda sehemu kama hizo, na mda wote wanajua niko kazini kama sio kanisani au nyumbani,. Kwakweli niliwaacha tu wahangaike hadi asubuhi wakaenda wenyewe,.

3. Hii hapa kuna siku nilikua niko na Jamaa ( mpenzi wangu )kuna mahali nilimsindikiza kwenye kikao wakati wa kurudi tukapitia mahali kula,. Asa eneo tulilopark gari ni eneo ambalo nalifaham vizuri tu na kuna magari kama matatu hivi Alphard yalikua yamepakiwa kwa pembeni na wenye hayo magari nawafahamu vizuri tu ,. Si nikaropoka bhana “ Haya magari haya yamepark hapa saizi lazima tu kuna watu wananjunjana “ akastuka mmmh,. Akaanza kunihoji umejuaje wewe na haya magari yana tinted nikabaki kujiuma uma tu nikapotezea mada.. Kiukweli najua sana na ushahidi ninao lakini sasa namna niliyojua jua inatatanisha kiasi kwamba nilionekana sina maana sikuile🥹😔,. Lakini tu najua ila sijui

Matukio ni mengi jamani mikono imechoka kuandika,. Tuambie na wewe kama inakukutaga hii tusimulie sisi hatukufaham hutapata shida😬
Basi ulisha kunjwa kwenye hizo alphard
NAENDELEA KUWAKUMBUSHA WANAUME WENZANGU : KAMA SIO BIKRA USIOE!! DON'T BE A "NICE" MAN
 
Back
Top Bottom