Hivi utaratibu wa mtumishi wa umma akiiba au akikosea ahamishiwe sehemu nyengine una maslahi gani kwa taifa?

ZALEMDA

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
1,956
Reaction score
2,225
Msomi akipata shavu la kuajiriwa serikalini, inakuwa raha msarehe. Hatakiwi kuguswa hata akiiba; anahamishiwa sehemu nyingine. Hivi huu utaratibu uko kwetu Tanzania tu au ni duniani kote? Mtu unakula kodi za walalahoi, unaiba, unakosea, halafu eti usisemwe na ikiwezekana uhamishiwe sehemu nyingine uendelee kuiba kule uendako.

Tuna watu wamegraduate tangu 2015 mpaka leo hawana kazi lakini unakuta mtumishi wa umma, jizi tena limekubuhu, linaachwa au linahamishiwa sehemu nyingine. Hivi huyu mtumishi jizi akifukuzwa kazi akaajiriwa mwingine kuna shida gani?

Aisee, mimi nikiwa rais nabadilisha kila kitu. Mswada wa kwanza kupelekwa bungeni utakuwa wa kubadilisha utaratibu huu. Hatuwezi kukaa na wazembe, majizi nk maofisini, halafu eti tutegemee mabadiliko, nchi ipae kiuchumi.
 
Anzisha chama!
 

Umetengeneza wezi sugu wasioogopa chochote ndani ya miundombinu ya umma. Inasikitisha sana kusikia na kuona haya mambo yanavyoenda.

Na naona kama hakuna majawabu ya hilo tatizo. Labda sababu linaanzia pabaya 🀣 🀣 🀣 🀣 🀣
 
Unadhani rahisi hivyo,anyway ukiona mkia umeoza jua kichwa ndio kuzidi.
 
Wizi ni wa mfumo mzima kuanzia juu kushuka chini
 
Sheria ndiyo ilivyo,huku inalinda na huku inaua ndio maana ya msumeno. Nyerere aliweka kifungu hicho kwenye katiba ili kuzuia mtu yeyote kujiamulia kumfukuza kazi mtumishi kwa kutumia tu cheo chake au mabavu.

Ingekuwa yeyote anafukuza kwa Tanzania hii nina hakika watumishi wengi wangekua wanafukuzwa kwa uonevu, sasa sheria hiyo hiyo inayotetea watumishi ndio hiyo hiyo inawapa loophole ya kuhamishwa akijaribu au kusimamishwa tu kupisha uchunguzi na akionekana hana hatia (ambayo ni rahisi tu nchini kwetu) basi anaendelea na kazi ila sehemu nyingine. Kiufupi katiba inasema anaeajiri na kutengua ajira ni Rais.
 
Kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake…
 
Watumishi wa umma wapo wapo tu, hawana "annual targets/KPIs" kitu ambacho huwafanya kuishi kwa mazoea. Aidha wapo katika ajira za kudumu kitu ambacho ni tofauti kabisa na waajiriwa wa sekta binafsi.

Ni wakati sahihi sasa kwa serikali kubadilisha vigezo na masharti ya utumishi wa umma. Ili kuchochea na kuongeza nidhamu, tija na ufanisi katika sekta ya umma, nayo inapaswa kuwa kama ilivyo katika sekta binafsi.
 

Na wanaamini wao wako sahihi na wanaweza kutufanya lolote tukiuliza kulikoni. Wanaweza hata kutuita wahalifu, ili mradi tu wasiguswe, na waendelee na bongo tambarale mpaka mwisho wa dahali πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ .
Ina maana hawaoni kuna shida mahala inataka ufumbuzi? Ina maana kuiba mali ya umma, CAG anatoa uthibitisho na hakuna linalofanywa, sio kosa la jinai? Sasa makosa ya jinai ni yapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…