Hivi VAT huwa inakatwa kwenye mauzo au kwenye faida?

Hivi VAT huwa inakatwa kwenye mauzo au kwenye faida?

Hiyo bidhaa ya TZS 100,000 kama umenunua kwa mfanyabiashara aliyesajiliwa tayari ndani yake kuna VAT TZS 15,254.

Endapo umeuza TZS 120,000 ikijumuisha VAT, VAT hapo ni TZS 18,305.

Utakacholipa TRA ni TZS 3,051 hii ndio kodi ya Ongezeko la thamani kati ya bei uliyouzia na ile uliyonunulia.

Ugumu kwenye VAT unakuja pale unaponunua kwa mtu ambaye hakusajiliwa VAT wakati wewe umesajiliwa VAT. Ili usipate shinda kwenye sheria ya VAT, kama wewe umesajiliwa VAT nunua bidhaa zako kwa mtu aliyesajiliwa VAT kwani ile VAT unayolipa kwenye manunuzi si gharama ya biashara yako, utajirudisha kwa kupunguza kwenye VAT uliyowatoza wateja wako.
shukrani sana. nimekupata vyema.
 
Mfano upo hivi
(1)Umenunua bidhaa 100,000
Jumlisha Vat 18%=18,000
Kwa hiyo jumla bidhaa umeinunua kwa 118,000
(2) Bidhaa unaiuza kwa 150,000 vat exclusive
Jumlisha vat 18%=27000
Kwa hiyo bei ya bidhaa itakuwa sh.177,000 vat inclusive
Ukicheki hiyo mifano miwili hapo juu;
Vat ilichajiwa mfano A ni Input tax (vat on purchase)
Vat iliyochajiwa mfano B ni Output tax(vat on sales)
Sasa ikitokea Output tax ni kubwa kuliko input tax tofauti unaenda kulipa Tra
Mfano:27,000-18,000=9,000

Na ikitokea Input tax ni kubwa kuliko Output tax tofauti ni refund/claim (Tra wanapaswa kukurudishia)
Mkuu na ukiclaim refund wanakurudishia kwa mtindo gani?
 
Check na hii mkuu
vat=out put tax-input tax, output tax=120000*18%=21,600 yaan sales*18%. input tax=purchase*18%, 100000*18%=18000. Vat=21600-18000=3600.
kumbuka anaeweza kucharge VAT ni yule tu aliesajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani. kama mfanyabiashara hajasajiliwa ataongeza tu faida yake ya kawaida hatacharge VAT.
 
input itakuwa 18000 na output 21600. kwa hiyo ntalipa 3,600? ni ikitokea nimeuza kwa hasara labda 90,000 na VAT ikawa 16200 inabidi niende TRA kudai (16200-18000) 1,800?. nafikiri nimekupata.
Kwa hiyo tra watakupa pesa hiyo kweli?
 
Lakini hiyo in put unaipata kwenye manunuzi na out put kwenye mauzo swali langu je nisipopeleka output nikapeleka in put peke yake je ni kigezo gani wanachokitumia kukadiria VAT?
 
Kwa kifupi uza bidhaa kwa Tzs 100,000/- hiyo ni pamoja na faida yako, then add 18% VAT jumla yake mtoze mlaji.
 
Mfano nimenunua bidhaa 100,000, nikiweka gharama zingine inafika 103,000 na nimeuza bidhaa hiyo 120,000 na kupata faida 17,000.

Je, VAT itakuwa 18% ya 120,000, yaani 21,600?.

Au itakuwa 18% ya 17,000 yaani 3,060?

Sheria ya kodi ya nchi inasemaje kuhusu VAT?

Nchi zingine zinafanyaje?

Naomba kujuzwa.
huja soma.Sheria
 
Biashara sio duka tu. Mfano una garage VAT registered, mara nyingi unanunua parts in retail kutokana na demand ya siku hio. Obviously utanunua kwa retailer ambao wengi sio vat registered.

Muuzaji asiyesajiliwa VAT hulipa kodi gani mbadala wa VAT?
 
Muuzaji asiyesajiliwa VAT hulipa kodi gani mbadala wa VAT?
Nyinginezo kasoro VAT. Mfano mapato,corparate tax,withholding tax etc. Wenye maduka wanakadiriwa kodi ya mwaka.
 
[QUOTE="Willy Johnson, post: 19263620, member: 383977"]Lakini hiyo in put unaipata kwenye manunuzi na out put kwenye mauzo swali langu je nisipopeleka output nikapeleka in put peke yake je ni kigezo gani wanachokitumia kukadiria VAT?[/QUOTE]

ndugu willy kama hujafanya mauzo inamaana output tax itakuwa sifuri. hapa ndo unaweza kukuta output tax n ndogo kuliko input tax. Ambapo hapa mfanyabiashara anaweza kuomba refund TRA.
Kodi hii hulipwa na final consumer, ndo maana wafanya biashara wanavyosema hawatoi risisti ya mashine maana inakata VAT sio sawa hata kidogo.
Ikumbukwe pia sio watu wote wenye mashine wanaoweza kucharge VAT, ni wale tu waliosajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani. wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT (yaani mauzo ghafi hayafiki m100 au m50 kwa miezi 6)hawapaswi kutoza VAT hata kama wana mashine za efd.
wao wanapaswa kuweka tu faida yao na sio vinginevyo


naomba kuwasilisha.

 
Back
Top Bottom