Hivi VAT huwa inakatwa kwenye mauzo au kwenye faida?

shukrani sana. nimekupata vyema.
 
Mkuu na ukiclaim refund wanakurudishia kwa mtindo gani?
 
Check na hii mkuu
vat=out put tax-input tax, output tax=120000*18%=21,600 yaan sales*18%. input tax=purchase*18%, 100000*18%=18000. Vat=21600-18000=3600.
kumbuka anaeweza kucharge VAT ni yule tu aliesajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani. kama mfanyabiashara hajasajiliwa ataongeza tu faida yake ya kawaida hatacharge VAT.
 
input itakuwa 18000 na output 21600. kwa hiyo ntalipa 3,600? ni ikitokea nimeuza kwa hasara labda 90,000 na VAT ikawa 16200 inabidi niende TRA kudai (16200-18000) 1,800?. nafikiri nimekupata.
Kwa hiyo tra watakupa pesa hiyo kweli?
 
Lakini hiyo in put unaipata kwenye manunuzi na out put kwenye mauzo swali langu je nisipopeleka output nikapeleka in put peke yake je ni kigezo gani wanachokitumia kukadiria VAT?
 
Kwa kifupi uza bidhaa kwa Tzs 100,000/- hiyo ni pamoja na faida yako, then add 18% VAT jumla yake mtoze mlaji.
 
huja soma.Sheria
 
Biashara sio duka tu. Mfano una garage VAT registered, mara nyingi unanunua parts in retail kutokana na demand ya siku hio. Obviously utanunua kwa retailer ambao wengi sio vat registered.

Muuzaji asiyesajiliwa VAT hulipa kodi gani mbadala wa VAT?
 
Muuzaji asiyesajiliwa VAT hulipa kodi gani mbadala wa VAT?
Nyinginezo kasoro VAT. Mfano mapato,corparate tax,withholding tax etc. Wenye maduka wanakadiriwa kodi ya mwaka.
 
[QUOTE="Willy Johnson, post: 19263620, member: 383977"]Lakini hiyo in put unaipata kwenye manunuzi na out put kwenye mauzo swali langu je nisipopeleka output nikapeleka in put peke yake je ni kigezo gani wanachokitumia kukadiria VAT?[/QUOTE]

ndugu willy kama hujafanya mauzo inamaana output tax itakuwa sifuri. hapa ndo unaweza kukuta output tax n ndogo kuliko input tax. Ambapo hapa mfanyabiashara anaweza kuomba refund TRA.
Kodi hii hulipwa na final consumer, ndo maana wafanya biashara wanavyosema hawatoi risisti ya mashine maana inakata VAT sio sawa hata kidogo.
Ikumbukwe pia sio watu wote wenye mashine wanaoweza kucharge VAT, ni wale tu waliosajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani. wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa na VAT (yaani mauzo ghafi hayafiki m100 au m50 kwa miezi 6)hawapaswi kutoza VAT hata kama wana mashine za efd.
wao wanapaswa kuweka tu faida yao na sio vinginevyo


naomba kuwasilisha.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…