Hivi vitambulisho vya mjasiriamali mdogo vina maana gani hasa? Pesa inayokusanywa ni ya nani na inakwenda wapi?

Hivi vitambulisho vya mjasiriamali mdogo vina maana gani hasa? Pesa inayokusanywa ni ya nani na inakwenda wapi?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
7,951
Reaction score
12,541
WanaJF, habari zenu wote!!

Hebu tulijadili tena hili. Mwaka huu 2020 limekuja kiaina na kivingine kabisa. Limeniacha na maswali yasiyo na majibu. Labda wenye majibu watatushirikisha...

Ni kuhusu hii kitu iliyopewa jina la "KITAMBULISHO CHA MJASIRIAMALI MDOGO". Mimi naona kama ni usanii na ufisadi uleule wa ki -CCM wa miaka yote

ID yenyewe ya mwaka huu 2020 ni hii hapa katika picha (mbele na nyuma). Itazame na tujiulize maswali kadhaa tunapojadili;

IMG_20200707_122637.jpg
IMG_20200707_122848.jpg


Ukiitazama vizuri EXPIRED DATE ya ID za mwaka huu, vimeandikwa ni December 31, 2020....

Maswali ya kujiuliza ni haya;

1. Wote tunajua kwa utaratibu mzunguko wa mwaka wa fedha huanza July 1 - Juni 31 kila mwaka. Ni kwanini ID za mwaka zimeanza kugawiwa July na muda wake uishe Dec. 31,2020 nusu mwaka?

2. Nini hasa lengo la ID hizi? Ni hilihili lililosemwa awali lililoanzisha kodi hii kwa tamko la jukwaani la Rais Magufuli?

3. Fedha Tshs. 20,000 kwa kila ID inayouzwa na maDC kupitia watendaji wa kata na vijiji zinaenda wapi?

4. Ni kweli fedha inayotokana na mauzo ya ID hizi inaingia kwenye mfuko wa serikali kama kodi ama huu ni mradi wa maCCM kujipatia fedha za uchaguzi tu?

5. Ni kwanini safari hii ID ziwe na EXPIRED DATE ya Dec. 31, 2020 pungufu ya miezi 6 ktk mwaka huu wa fedha 2020/2021?. Tukumbuke kuwa ID za mwaka wa fedha 2019/2020 muda wake (expired date) ilikuwa Juni 31, 2020. Hivi vipya vimeanza kutolewa trh 1/7/2020.

6. Amenusa nini huyu Magufuli hata kufupisha muda wa maisha (expired date) wa ID hizi kuwa Dec. 31, 2020 badala viende hadi Juni 31, 2021?? Kuna nini hapa? Je, ina maana kuanzia January 1,2021 tutalipa Tshs. 20,000 tena kupata vingine vipya?
 
Tunawarahisishia bado mnalalamika, tukipeleka mambo ki tra tra si mnajua mtiti wake.
 
Nilivyoelewa Mimi, hiki ni chanzo cha mapato ya Serikali ambayo awali yalikusanwa na Serikali za Mitaa/vijiji. Mapato haya hukusanywa kule kwenye jungu kuu HAZINA. Serikali unatumia fedha hizi kuleta HUDUMA na uchumi kwa Jamii. AIDHA, Serikali za Mitaa kupata ruzuku iitwayo GPG Fidia kwa vyanzo vilivyofutwa hamishwa ili kuziwezesha kutekeleza majukumu yake.

Huo muda uliowekwa sio issue. Hapa uwe nacho halafu unatoboa HD juni km vile kilichoisha muda wake.
 
Sio lazima kujua kila jambo.wewe kama machinga ukishatoa buku twenty na kitamburisho umepewa basi chapa kazi mwanangu.mambo mengine hayamuhusu kila mtu.
 
Back
Top Bottom