Waafrika wenzetu tena jirani zetu wa Uganda wamezindua mabasi yanayotengenezwa nchini mwao tena na waganda wenyewe. Hivyo badala ya kutoka mabilioni ya pesa nje ya nchi kwa ajili ya kununulia mabasi pesa zote zinabaki ndani ya nchi, pamoja na kuongeza mapato ya fedha za kigeni pale nchi nyingine zinaponunua mabasi kutoka kwao. Kwa kufanya hivyo pamoja na miradi mingine, uchumi wa Uganda utakua kwa kasi zaidi.
Je, sisi tunashindwa nini kutengeneza mabasi, zana na mashine za kilimo, au kutengeneza magari kama wenzetu Kenya na Rwanda?
Maana uagizaji wa magari, zana za kilimo na mashine zingine unatupotezea pesa nyingi na kuathiri mzunguko wa pesa ndani ya nchi, kuchangia ukosefu wa ajira na kuathirika kwa kasi ya ukuaji wa uchumi.
Je sisi hatulioni hilo? Au hatuwezi? Au muda wetu wa kuamua bado?
Sent using Jamii Forums mobile app
Je, sisi tunashindwa nini kutengeneza mabasi, zana na mashine za kilimo, au kutengeneza magari kama wenzetu Kenya na Rwanda?
Maana uagizaji wa magari, zana za kilimo na mashine zingine unatupotezea pesa nyingi na kuathiri mzunguko wa pesa ndani ya nchi, kuchangia ukosefu wa ajira na kuathirika kwa kasi ya ukuaji wa uchumi.
Je sisi hatulioni hilo? Au hatuwezi? Au muda wetu wa kuamua bado?
Sent using Jamii Forums mobile app