Hivi Wazungu wao wanajisikiaje katika Dunia yenye 'Miafrika Ndivyo Ilivyo'?

Hivi Wazungu wao wanajisikiaje katika Dunia yenye 'Miafrika Ndivyo Ilivyo'?

Shule ya kinadharia haitanishawishi mimi. Kitakachonishawishi ni sisi Miafrika kufanya kweli na kuanza kuishi maisha bora kama mizungu. Longolongo nyingi hazitatui matatizo yoyote.

Haya nendeni kule Mbinga mkajenge shule bora zenye viti na sio wanafunzi kukaa chini kwenye vumbi. Is that too hard?
Mkuu haiwezekani kwa sababu hiyo hiyo kuwa tunajaribu kuishi kama wazungu.. huwezxi kubadilisha mazingira ya Serengeti anakoishi Simba ili kumwezesha simba huyo huyo aishi kama Bear wa Vancouver, pamoja na kwamba wanyama wote hawa wana mahitaji sawa ya Kinyama.

Sisi kama Simba tutayatengeneza mazingira yetu kutuwezesha sisi Simba kuwinda kwa urahisi ktk mazingira haya haya na sii kuibadilisha Serengeti inaze kuwa na snow ili nasi tunanze kuwinda samaki Salmon.
Siku tutakapo elewa kwamba sisi tunaishi Serengeti na shule yetu itakuwa kujifunza mazingira ya Serengeti, kuwafundisha watoto wetu jinsi ya kuwinda ndani ya mbuga zetu badala ya kupendelea kusoma elimu ya Ulaya inayotufundisha sisi kucheza katika Zoo na sarakasi za Ulaya ni vigumu kuyabadilisha maisha ya Waafrika.
Nimekwisha sema hata Elimu tunayoipata nyumbani ni Elimu tegemezi ya Ulaya kwenye kila kifaa cha kutuchezesha sarakasi ndio maana wasomi wetu wameshindwa hata kutengeneza sindano.. tunashindwa hata kutengeneza Baiskeli ya kurudi nyuma, bajaj zinaagizwa toka India na kadhalika.

Nchi ina joto kali lakini tunashindwa hata kutengeneza Humidfier ya kupunguza joto ndani ya nyumba zetu kitu ambacho kinatengenezwa kirahisi kabisa na motor ndogo ya feni..Badala yake tunajenga nyumba sawa na za Ulaya zenye fire place, sauna na kadhalika. Imean hivi kweli mkuu wangu kuna haja ya kujenga nyumba yenye indoor garage?.. hatuna snow wala hali mbaya ya hewa inayoweza athiri bodi la gari tukiegesha magari yetu nje na pembeni ya nyumba..lakini kwa sababu tu Ulaya wanafanya hivyo basio nasi tunajenga nyumba zetu kama za Ulaya, ceramic tiles hadi living room wenyewe wakisema ni Marble..Haya ndio maendeleo ya mtu mweusi..

Tutakapo weza kupanga vipaumbele vyetu tukasoma na kuelewa nini mahitaji yetu (matatizo) bila shaka tutaweza kuwa na maendeleo yetu.. Maisha bora siui lazima watu wote wale kwa visu na kuvaa suti..Maisha bora sii lazima tule kwa vijiti kama Wachina..
Waziri mkuu Pinda kasema kidogo tu kuhusiana na vazi la suti, Miafrika tumekuja juu vibaya sana hali tukijidai sisi sio Ndivyo Tulivyo - Malimbukeni wa Kuiga.

First we have to accept who we are na kisha kuboresha mazingira yetu ili kumwezesha kila Mtanzania kumudu mahitaji muhimu na yenye manufaa..
 
Socrate Alikuwa ana maana kubwa sana katika dhana yake ya kuuliza 'WHY?' Hakuna Mafanikio au Solution yeyote inayopatikana out of 'WHY?' Newton asked himself 'WHY?' so is Einstein any many other dudes, Waafrika wengi chukulia mfano Watanzania hatupendi kujishughulisha, maadam tunakula, tunatembelea Gari au baiskeli tunapenda Kula Raha badala ya kujishughulisha akili zetu na Ndio maana Wataalamu wengi wanakimbilia Siasa.
 
Mkuu Companero hebu Tembelea thread ya Wamarekani kuupiga Mabomu Mwezi uone Mawazo ya Waaafrika, mawazo yamejaa woga wa kutokuwa na Uhakika na matokeo ya Zoezi hilo, kwa kawaida Waafrika Tukishindwa kitu tunamsingizia Mungu utasikia TUMWACHIE MUNGU
 
Obama ni nusu mzungu nusu mwafrika. Nadhani hapa tunazungumzia full bantus kama kina Mugabe....
Kwa hiyo dawa ni kuji-lactify/whiten kwa kuoa na kuona na wazungu? Lakini mbona Brazili walijaribu na bado nao ni Dunia ya 3? Hivi kuna magic gani kwenye hivyo vinasaba vya kizungu?
 
Hebu Kuleni Jani la Marley kwanza

[FONT=Trebuchet MS, Verdana, Arial][SIZE=-1]Emancipate yourselves from mental slavery;
None but ourselves can free our minds.
Have no fear for atomic energy,
'Cause none of them can stop the time.
How long shall they kill our prophets,
While we stand aside and look? Ooh!
Some say it's just a part of it:
We've got to fulfil de book. [/SIZE][/FONT]
 
We are Mentally Slaves kaka, cheki hata Curriculum zetu, hivi mkuu wangu unategemea Mwanafunzi aliyekuja kuiona Pendulum Bob akiwa Chuo kikuu atakuwa na uwezo wa Kutumia Gravitation laws kwenda Mwezini?
 
Kwa hiyo dawa ni kuji-lactify/whiten kwa kuoa na kuona na wazungu? Lakini mbona Brazili walijaribu na bado nao ni Dunia ya 3? Hivi kuna magic gani kwenye hivyo vinasaba vya kizungu?

Brazil ndio haijaendelea kama Marekani au Ujerumani lakini Brazil huwezi kuilinganisha na nchi yeyote ile ya Afrika. Halafu huko Brazil Miafrika ya huko ndio inataabika zaidi ya wazungu na wale waliochanganya damu. Why?

Halafu nyinyi Miafrika yenye akili hebu fanyeni kweli basi mlitatue tatizo la umeme bongo. Au mnasubiri mizungu ije iwasaidie?
 
Hebu niwekee hizo picha za hao "African Americans" niwaone maana Wamarekani weusi wengi wamechanganya damu na wazungu na wahindi wekundu.

Hata W.E.B. DuBois alikuwa ni Mmarekani mweusi lakini hebu mwangalie vizuri...jamaa ni mulatto fulani hivi..kama alivyo Obama.

Cuthbert Walker huyu hapa...hebu mtazame vizuri...siyo full bantu huyu...
Frederick Gregory huyu hapa chini. Naye siyo full bantu huyu..Lol

Sawa J. nilijua tu argument itakayofuata ni hii ya kwamba hawa jama siyo full bantus kwa kuangalia wanavyoonekana.

Ila kuna mtu aliwahi kuniambia kwamba kule Ntuzuland watu wanaong'aa ng'aa kama Chenge vile huwa wanachaguliwa kiulaini kwa sababu ya mentality kwamba ukiwa na rangi nyeupe nyeupe basi wewe siyo mwafrica per se na una akili nyingi! Hope this has nothing to do with the saying 'Miafrika Ndivyo Ilivyo'.
 
Hebu tumsikilize mchambuzi maarufu wa uzungu na uafrika:

"At the risk of arousing the resentment of my coloured brothers, I will say that the black is not a man"

"The black man wants to be white. The white man slaves to reach a human level"

"There is a fact: white men consider themselves superior to black men"

"There is another fact: black men want to prove to white men, at all costs, the richness of their thought, the equal value of their intellect"

"However painful it may be for me to accept this conclusion, I am obliged to state it: for the black man there is only one destiny: And it is white"

- Frantz Fanon on Black Skin White Masks
 
Companero,
Mkuu aloandika hapo kadhihirisha maneno yangu kwamba tatizo la mwafrika ni mwafrika mwenyewe kwani malengo ya maendeleo yake ni kuwa kama mzungu..
Sasa tunaposhindwa kuelewa kwamba hata Simbawe tu hawezi kuwa sawa na Simba aliyteko zoo Ulaya.. mbwa wetu hawezi kuwa sawana mbwa wa Ulaya,Nyani wa Afrika hawezi kuwa sawa kimaisha na yule wa Ulaya, kifupi wanyama wote hawa wa Ulaya wana maisha bora kulko Afrika, hivyo swala la ndivyo tulivyo haliwezi kuwa ni AKILI zetu bali mazingira ya sehemu tunazoishi ndio hutengeneza maisha ya wahusika.

Sisi Miafrika tunachojaribu kufanya ni kuwa sawa na wazungu. zamani tulikuwa tukilima chakula chetu siku hizi tunaagiza vya makopo kama wazungu..itafikia siku hata mbwa wetu wanavikwa masuti kama wale wa Ulaya maadam tu tuwaonyeshe wazungu kwamba hata sisi tunaweza kuwa kama wao.
 
Kweli mmepevuka kiakili, mara nyingi watu huwa hawatambui wala kukubali kuwa wanamatatizo,

Shida ni elimu na wenye madaraka,

Hakuna walimu wa masomo ya Sience na waliopo hawafanyi kwa kiwango wanachoweza kufanya sababu ni mshahara kiduchu,
Wataalam mainjinia unawakuta wamo maofisini mpaka mainjinia wa kutoka china ndo waje watuchimbie mitaro na kujenga nyumba,

Kila mtu anataka akae ofisini tu! Me huwa inaniuma yaani kwa mtu ambae anafanya kazi na wazungu atagundua hili suala yaani wazungu huwa wana ufeel udhaifu wetu lakini tupo waafrika ambao tupo makini kuliko wazungu sema tu mazingira.
 
sisi wa-afrika kwa wazungu tunaonekana kama ''nyani'',kana kwamba haitoshi sisi wenyewe tuna tabia za kinyani vilevile, kwa mfano, tazama jinsi tulivyo warahisi kushawishiwa na wazungu juu ya mambo yetu muhimu yanayotuhusu mfano mzuri ni jinsi wazungu walivyo behind vita zote zinazo endelea hapa Afrika aidha kwa kupandikiza chuki au kusponsor kwa kutupa silaha mambo mengine ni wanavyo chukua madini kwa kututisha na soko lao huria, sasa utasema sisi ni wazima kweli?WACHA WATUDHARAU TU NYANI SISI!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo tunajidharau. Hii mada inaonyesha kuelekea huko! Kwa nini mnaabudu wazungu? mimi hata siku moja siwezi kujidanganya niko chini ya wazungu! All humans are made equal! Ukimweka mwaafrika katika equal level...na yeye atafanya mambo yale yale.

Kitu kinachofanya wazungu waendelee ni jinsi walivyojenga society yao. Wale walio na mawazo mazuri wanapewa nafasi ya kuyafanyia kazi. Wachovu wanafunikwa chini. Sisi tumekuwa na mtindo wa kubebana kwa wingi. Hii ndo tofauti kuu ninayoiona. Siku tutakapoacha wataalamu wetu wafanye kazi...ndipo na sisi tutapiga hatua. Ukitaka kujua wazungu wana-value wataalamu...wewe soma nao alafu uwe unafanya vizuri. They will help u and will try 2 keep you katika system yao. Hata kazi NASA utapata tu!


sisi tumekuwa kwanza tukidharau wataalamu wetu. Na pia wataalamu wetu wakati mwingine wanajifanya wajanja sana. Yani unaweza kukutana na mtu amefanya vitu kibao, lakini yupo simple sana. Lakini hilo kwa bongo, huyo mtu angependa misifa kibao.
Mfano mzuri ni angalia marais marekani. Mtu akimaliza huyoo ametoka na wala humsikii. Lakini sisi ndo hao wanabaki na blaa blaa nyingi. Watu wanakaa kwenye siasi kwanzia uhuru mpaka leo - Kingunge. Achieni ngazi na tuwe wepesi kukubali ideas za wengine pale zinapozidi za kwetu. Hii ndo ilikuwa weakness ya Nyerere
 
Back
Top Bottom