Hivi WCB huwa wana mpango gani na LAVALAVA?

Hivi WCB huwa wana mpango gani na LAVALAVA?

Huyu jamaa licha ya watu kusema ana gundu ila mimi naona sio gundu tu, ni kwamba menejimenti yake pia haimpush vile inavyopaswa. Nimeshuhudia mara nyingi Mbosso/Zuchu na boss mwenyewe wakiandaliwa zinduzi mbalimbali za Album/EP kwa gharama kubwa, huku wakipewa promo kubwa na Wasafi Tv/Redio bila kusahau machawa wao lakini sikumbuki kama Lavalava amewahi kufanyiwa hivi. Hata ukikakaa kwenye TV yao nyimbo za Boss, Mbosso na Zuchu zinachezwa sana kuanzia mpya hadi za zamani, lakini ni nadra kuona nyimbo za Lavalava. Na si kwamba Lavalava hatoi ngoma kali, ana nyimbo nzuri nyingi tu. Je, wana mpango gani na huyu mtu pale WCB mbona anaishi kama mtoto yatima?
Ndo maana adi dulla makabila kamuimba mwamba
 
Aondoke tu usafini aende akajaribie kwengine maybe Kondegang huko,,,huwa sielewi jamaa anakwamaga wapi coz wenzake wote except for Zuchu wameshatoa album ila yeye yupo yupo tu.
Hiyo kondegang wamemtoa msanii gani mpaka useme aende huko?
 
Sio kweli.

Kwangwaru- Hit Song

Sukari - Hit song

Wah- Hit song

Tetema - Hit song

Nakupenda - Hit song
Nafikiri alimaanisha mega hits kama muziki ya darasa au kwangwaru ya diamond & harmonize.
 
Huyu jamaa licha ya watu kusema ana gundu ila mimi naona sio gundu tu, ni kwamba menejimenti yake pia haimpush vile inavyopaswa. Nimeshuhudia mara nyingi Mbosso/Zuchu na boss mwenyewe wakiandaliwa zinduzi mbalimbali za Album/EP kwa gharama kubwa, huku wakipewa promo kubwa na Wasafi Tv/Redio bila kusahau machawa wao lakini sikumbuki kama Lavalava amewahi kufanyiwa hivi. Hata ukikakaa kwenye TV yao nyimbo za Boss, Mbosso na Zuchu zinachezwa sana kuanzia mpya hadi za zamani, lakini ni nadra kuona nyimbo za Lavalava. Na si kwamba Lavalava hatoi ngoma kali, ana nyimbo nzuri nyingi tu. Je, wana mpango gani na huyu mtu pale WCB mbona anaishi kama mtoto yatima?
Ata mimi naona kuna shida mahali wangejaribu kumfanyia uzinduzi wa albamu tuone ni kweli watanzania kama hawamuelew tuone kama namba za mauzo zinaongezeka ama vipi
 
Ata mimi naona kuna shida mahali wangejaribu kumfanyia uzinduzi wa albamu tuone ni kweli watanzania kama hawamuelew tuone kama namba za mauzo zinaongezeka ama vipi
Uzinduzi amefanyiwa hadi Barnaba ambaye sio member wa WCB
 
Jambo hilo liko sehemu zote ata kwenye maisha kuna baadhi ya familia baadhi ya watoto hupewa kipaumbele kuliko wengine.

Lavalava ana kipaji labda ni bahati au namna anajiweka
Viti maalyum
 
Sio kweli.

Kwangwaru- Hit Song

Sukari - Hit song

Wah- Hit song

Tetema - Hit song

Nakupenda - Hit song
Sijui jamaa hit song anaipima kwa vigezo gani.

Au labda wingi wa nyimbo kali kitaa zilizobamba(hit songs) unamchanganya na kukalili kua ngoma huwa inahit moja tu kwa muda fulani.

Nakupenda ya jaymelody imesumbua kinoma mtaa, kwangwaru enzi hizo, sukari nk
 
Back
Top Bottom