Hivi Wizara ya Afya bado ipo? maana imekuwa kimya sana kama vile kila kitu kiko sawa.
Mimi binafsi ninachokiona kwenye wizara hii ya afya ni kama ka mgomo baridi vile,
Nikisikiliza kwenye mitandao ya kijamii naona wanasiasa ambao hawana timu za kuchezea msimu huu wa 2020/2025 wakizusha tafrani na kudai matangazo. hawa unaweza kuwaelewa kwamba wanatafuta usajiri pengine sijui.
Lakini kwa wizara ya afya najiuliza kuna nini?
Mara kadhaa nimesikiliza viongozi wa nchi hii wakisema "kuna matatizo ya upumuaji" na kuongeza "watanzania tuchukue tahadhari" na tutumie njia zetu za hapa kupambana na haya.
Kwangu mimi msimamo huu wa serikali maagizo tosha kwa wizara ya afya kufanya kampeni kabambe za kuhamasisha wananchi kujikinga na matatizo haya ya kupumua na kupambana kwa kutumia dawa zetu.
Msimamo wa serikali haijalishi kila mtanzania anaukubali au haukubali, haijalishi kama jamii za kimataifa zinaukubali au haziukubali
Kitu kikubwa kinachotizamwa ni matokeo na matokeo hayatokani na matamko ya serikali bali ile kazi inayoanzia wizara ya afya na kusambaa kwa kila Mtanzania.
Ila kwa kile ninachokiona ni kama Wizara ya Afya kuna watu hakubaliani na msimamo wa serikali pengine na wameamua kukaa kimya ili kuiprove wrong serikali yetu, nalazimika kuwaza hivyo.
Wizara ya afya ndiyo ya kuzima kelele au kutishana tunakokusikia mitaani na sio matamko ya serikali.
Hawa ni kuelimisha watu matatizo haya ya upumuaji yanasambaa kwa njia gani na kusisitiza watu kujikinga na hasa hili ndilo lenye nguvu.
Kuna maelekezo mengi mitandaoni ambayo wizara ingetolea ufafanuzi
Kuna orodha ya madawa sijui aspirin junior, sijui azuma, sijui amoclave, n.k
Hivi matumizi sahihi ya hizi dawa ni yapi? maana kinachoendelea mitaani ni kichwa kikigonga mtu anakimbia ananunua Aspirin junior na kumeza. Wafamasia hawatuelezi habari za kutosha maana ukienda wanakuandikia tumia 1 x 1 kwa mda gani sijui.
Je, dawa hizi unaweza kuchanganya ipi na ipi? hatujui, mtu unaweza kumeza zote kumbe inatakiwa aina kama mbili au tatu.
Je, kama nimepewa vidonge vitatu vya azuma, nikameza na bado naendelea kujisikia vibaya nikanunue nyingine au niache niendelee na dawa nyingine.
Hapa ninachokiona ni matumizi ya holela ya dawa mitaani na hili linaweza kuleta athari nyingine.
Pengine Pale juu Wizara ya Afya tunahitaji mtu ambaye sio daktari kwa taaluma ili aweze kubalansi vizuri maagizo ya kisiasa na ushauri wa wataalamu.
Maana inaonekana Daktari akipewa maagizo kwanza anaanza kuyapima maagizo kwa kutumia taalauma yake.
Mimi binafsi ninachokiona kwenye wizara hii ya afya ni kama ka mgomo baridi vile,
Nikisikiliza kwenye mitandao ya kijamii naona wanasiasa ambao hawana timu za kuchezea msimu huu wa 2020/2025 wakizusha tafrani na kudai matangazo. hawa unaweza kuwaelewa kwamba wanatafuta usajiri pengine sijui.
Lakini kwa wizara ya afya najiuliza kuna nini?
Mara kadhaa nimesikiliza viongozi wa nchi hii wakisema "kuna matatizo ya upumuaji" na kuongeza "watanzania tuchukue tahadhari" na tutumie njia zetu za hapa kupambana na haya.
Kwangu mimi msimamo huu wa serikali maagizo tosha kwa wizara ya afya kufanya kampeni kabambe za kuhamasisha wananchi kujikinga na matatizo haya ya kupumua na kupambana kwa kutumia dawa zetu.
Msimamo wa serikali haijalishi kila mtanzania anaukubali au haukubali, haijalishi kama jamii za kimataifa zinaukubali au haziukubali
Kitu kikubwa kinachotizamwa ni matokeo na matokeo hayatokani na matamko ya serikali bali ile kazi inayoanzia wizara ya afya na kusambaa kwa kila Mtanzania.
Ila kwa kile ninachokiona ni kama Wizara ya Afya kuna watu hakubaliani na msimamo wa serikali pengine na wameamua kukaa kimya ili kuiprove wrong serikali yetu, nalazimika kuwaza hivyo.
Wizara ya afya ndiyo ya kuzima kelele au kutishana tunakokusikia mitaani na sio matamko ya serikali.
Hawa ni kuelimisha watu matatizo haya ya upumuaji yanasambaa kwa njia gani na kusisitiza watu kujikinga na hasa hili ndilo lenye nguvu.
Kuna maelekezo mengi mitandaoni ambayo wizara ingetolea ufafanuzi
Kuna orodha ya madawa sijui aspirin junior, sijui azuma, sijui amoclave, n.k
Hivi matumizi sahihi ya hizi dawa ni yapi? maana kinachoendelea mitaani ni kichwa kikigonga mtu anakimbia ananunua Aspirin junior na kumeza. Wafamasia hawatuelezi habari za kutosha maana ukienda wanakuandikia tumia 1 x 1 kwa mda gani sijui.
Je, dawa hizi unaweza kuchanganya ipi na ipi? hatujui, mtu unaweza kumeza zote kumbe inatakiwa aina kama mbili au tatu.
Je, kama nimepewa vidonge vitatu vya azuma, nikameza na bado naendelea kujisikia vibaya nikanunue nyingine au niache niendelee na dawa nyingine.
Hapa ninachokiona ni matumizi ya holela ya dawa mitaani na hili linaweza kuleta athari nyingine.
Pengine Pale juu Wizara ya Afya tunahitaji mtu ambaye sio daktari kwa taaluma ili aweze kubalansi vizuri maagizo ya kisiasa na ushauri wa wataalamu.
Maana inaonekana Daktari akipewa maagizo kwanza anaanza kuyapima maagizo kwa kutumia taalauma yake.