Kumbe JF kuna mazuzu kiasi hiki?
Inatolewa hoja ya maana ila majibu yanayotolewa ni ya ajabu.
Yanga iliasisiwa na waasisi wa TAA/TANU kwa lengo la kuwezesha harakati za kupigania uhuru.
Ni kwamba, wakati wa ukoloni, mikusanyiko ya kisiasa ilizuiliwa ila mikusanyiko ya michezo iliruhusiwa.
Kwa hiyo Yanga ilianzishwa na TAA/TANU kwa lengo la kupata wasaa wa kujadili ajenda za kisiasa bila kujulikana na wakoloni.
Simba/Sandaland ilianzishwa na UTP-United Tanganyika Party, ambacho ni chama kilichounga mkono ukoloni na kupinga harakati za uhuru.
Kiufupi, muasisi wa bendera na rangi za Yanga ndiye mwanzilishi wa bendera na rangi za CCM, na ndiye mwanzilishi wa bendera ya Tanzania na ile ya South Africa pia ina mfanano na bendera ya Tanzania.
Kwa hiyo kufanana kwa Yanga na CCM siyo jambo la ghafla.