Hivyo ndivyo vijana wa kazi wa Kitanzania wanavyoturudisha nyuma na kututia hasara kubwa

Hivyo ndivyo vijana wa kazi wa Kitanzania wanavyoturudisha nyuma na kututia hasara kubwa

Usinikumbushe,yaani nilikuta kifua kinajaa ghafla kama nashindwa kupumua flani hivi,nikafanikiwa kuishusha,angetokea mapema basi ningepiga tukio dunia ingeweka katika kumbukumbu
Hakika mkuu mimi jasho lilinivaa ghafla yaani kama yupo karibu na nina bastola kwisha habari yake.
 
Kweli changamoto Sana,Mimi naililia milioni moja na km laki tatu ilipotea yote Mazima.
Kuna jamaa tulikubaliana kulima pamoja,then tugawane faida mwishoni,Ni jamaa nilikuwa namwamini kabisa.
Kazi ikaanza,tukakodi shamba,akaweka kila kitu sawa na pesa nikatoa,Tena ya mkopo,hahahaha.
Kwa vile ilikuwa mkoa jirani jamaa akawa anaenda Mara moja moja kucheck shughuli na kila Mara alikuwa akinipa updates.
Kilimo kilikuwa Cha vitunguu kwa njia ya umwagiliaji,.
Eebwaneee,shughuli imekwenda ile karibu kuvuna,story zikaanza,maji yameisha bwawani so tutafute namna nyingine,Mara wafanyakazi wametoroka ,daaaa.
Mwisho kabisa sikupata hata shilingi kumi.
Kuanzia hapo nikapata SoMo kuwa ukitaka kazi yako iende vizuri,jitahidi kuisimamia mwenyewe kwa aslilia kubwa.
Mkuu ni ngumu sana asee kusimamia mwenyewe na kwa namna hii hatuwezi piga hatua kabisa.
imagine family ipo Dar miradi yako iko mwanza utajigawa vipi? je kama una miradi zaidi ya2 utajigawa vipi?

Tatizo ni sisi wenyewe wa Tz hatuhurumiani tumejaa wivu na husda na unafiki.
 
Zamani nilikuwa namaindi sana nikiona taasisi na kampuni nyingi za kigeni zikiajiri Zaid wakenya kuliko wazawa(wabongo)... Lakini baada ya Mimi kuanza kujichanganya Kwenye soko la ajira na kuona jinsi gani wabongo tunavyozingua na hatuna seriousness na kazi Zaid ya kuwaza malipo tu, Sasa hivi hata nikiskia TBL wameajiri warundi na hawajaajiri mtanzania hata mmoja nitawaona wako sahihi kabisa.
Hata mimi. Hivi kuna rafiki yangu naye yupo katika process ya kuwekeza katika kupiga story akaniambia katika usimamizi wa kazi zake atamuweka ndg yake mtoto wa mama yake mkubwa nimemshauri usithubutu kabisa japo kamfagilia sana yule ndg katoka chuo anajua kila kitu nimemwambia heri hata mtu baki ukikoswa warudi au mtu yeyote wa nje.
 
Mr Ukifa mke wako asiolewe kwanza nakupa pongezi kwa kuwa umekuwa ni kawaida yako kushare Tips za michongo na maisha. Na mimi nimekuwa nikijifunza sana kutoka kwako.

Pili nikupongeze kwa kuqa mpambanaji na unanitia moyo sana.

Ukisikia mtu anakulaumu kwa kulima kwa mutumia simu basi huyo naye hajielewi. Maana mtu mmoja hawezi kucanya kazi 5 kwa wakati mmoja lazima upate wasaidizi.

Hii ni Tabia ya Mtu Maskini. At time anaweza kujjfanya mchapa kazi lakini ile hulka ya uvivu itajionesha tu.

Imagine mtu kama huyo umempa ulaji na mchongo. Kabla hata hamjavuna ameshaanza kutafuna Starehe na ngono( Laan hii).

Hata sasa tunapokea simu nyingi za watu wakiwemo ndugu zetu kutupiga vibomu maea elfu 50, elfu 30 au hata buku teni. Wengine wanatuomba ada ,a watoto wao.

Sasa mwambie aisee njoo mjini kuna kazi yenye hela tuifanye. You will be surprised akijitahi ni mwezi mmoja na si zaidi ya miezi mitatu. Ataikimbia na atakutangaza kwa watu eti unamnyanyasa.

Wao wakikuona uko mjini unaenda na Mndinga wako wanadhani pesa unziokota kumbe na wewe una henya sana.
Umenena vyema mkuu uwekezaji wowote unahitaji man power ili upige hatua hata uwe mama ntilie una migawaha 4 lazima utakuwa na watu tu. TUKO PAMOJA MKUU NA AHSANTE SANA.
 
Hizi nyimbo za Simba na group lake linawadanganya sana. Ukizisikiliza utadhani Maisha ni kama maji. Zinaimba Anasa na starehe tu. Lakini hazisemi hizo starehe unazila vipi bila kazi bila pesa.

Tofauti na enzi zetu Wagosi wa kaya, TMK Family, J Nature, Inspector Harun Nyimbo zilitufundisha ukakamavu, kupiga kazi ngumu bila kuchoka na kukaza kiume.
Usimsahau mwamba wa kuitwa 20% bila bangi angekuwa mbali sana.
 
Kupata watu sahihi wa kufanya nao kazi tabu sana mkuu.

Tanzania tuna vijana wa hovyo sana mkuu, inatakiwa tuwe makini.

Jipange tena upya, kipindi hiki uwe muangalifu zaidi, Pole sana.
Ahsante sana mkuu siwezi kataa tamaa hata siku moja sema nawasikitia sana vijana wenzangu kama huyu niliye eleza hapo uhakika wa kupata hata laki1 moja ya mpingo kwa sasa na ana family maisha magumu nyumba mbaya hadi huruma. Tulipovuna nikampa m6 za hela bila kuzisimamia mimi angezitapanya. mke aliniambia usimpe njoo nae mnunue mabati chakula nk na nikafanya hivyo.

kwa sasa hawezi pata hiyo hela. Ahsante sana mkuu
 
Wakute sasa kwenye Simba na Yanga jitihada zao😅😅😅
Huyu jamaa siku inacheza simba usimwabie kitu kabisa kuhusu shamba sana sana omba mechi iwe usiku hapo kazi
atafanya lakini mawazo yake yote mpiran. itokee mechi inachezwa saa10 jioni shambani sahau kabisa na usitegemee tena anaenda mapema kuwahi viti vya mbele kwenye banda umiza. Ni ukichaa haswa.
 
Huyu jamaa siku inacheza simba usimwabie kitu kabisa kuhusu shamba sana sana omba mechi iwe usiku hapo kazi
atafanya lakini mawazo yake yote mpiran. itokee mechi inachezwa saa10 jioni shambani sahau kabisa na usitegemee tena anaenda mapema kuwahi viti vya mbele kwenye banda umiza. Ni ukichaa haswa.
Nawajua vizuri.....nikisha ona mfuasi wa hizi team tayari najua hapa kuna viwango vidogo vya akili
 
Ahsante sana mkuu siwezi kataa tamaa hata siku moja sema nawasikitia sana vijana wenzangu kama huyu niliye eleza hapo uhakika wa kupata hata laki1 moja ya mpingo kwa sasa na ana family maisha magumu nyumba mbaya hadi huruma. Tulipovuna nikampa m6 za hela bila kuzisimamia mimi angezitapanya. mke aliniambia usimpe njoo nae mnunue mabati chakula nk na nikafanya hivyo.

kwa sasa hawezi pata hiyo hela. Ahsante sana mkuu
Umaskini Kaka huwa unaanzia kichwani.

Pamoja na kwamba umembeba sana lakini bado habebeki.

Niliwahi kuishi Zanzibar kipindi fulani nikakutana na mzee mmoja amechoka mbaya. Wenyeji wakaniambia ni Kaka Yake Rais Wa Zanzibar wakati huo Dr Ali Mohamed Shein.
Yule mzee alikuwa kachoka anauza urojo.
Nikauliza imekuwaje Kaka yake Rais anakuwa na maisha magumj hivi? Yaani ndugu yakw ameshindwa jinsi ya kumnyanyua? Watu wanamlaum sana Rais Mstaafu Shein.

Lakini Deep Down ni kuwa huenda Shein alishajaribu mbinu zote za kumnyanyua lakini ikawa habebeki.

Ndio kama Hawa.

Ndugu wa Prof Kabudi ni Choka Mbaya kama ndugu wa Prof Kapuya.

Unaweza kuwalaum kwanini wanajipenda wao tu. Kumbe ndugu wenyewe ni wenye akili kama za huyo Mfanya kazi wako.

Kuna Ndugu uking'ang'ania kuwasaidia watakurudisha nyuma na wewe utakuwa maskini kama wao
 
Umeniumiza Kaka
Pole Sana ,usiku mwema na Sasa siwezi kuongezea chochote zaidi ya kusema kidonda ni kibichi mno umekitonesha Kaka 😭😭
Pole sana asee mimi ilinichukua siku kadhaa bila kumwambia wife. katika kupta mtandaoni ndo nikaona hiyo video jamaa kapita mlemle nilimopitia mimi kasoro mtaji tu.

Nivyema mkuu ukatumbia hapa nasi tupate mawili m,atatu ama manne tujifunze pia.
 
Pole sana asee mimi ilinichukua siku kadhaa bila kumwambia wife. katika kupta mtandaoni ndo nikaona hiyo video jamaa kapita mlemle nilimopitia mimi kasoro mtaji tu.

Nivyema mkuu ukatumbia hapa nasi tupate mawili m,atatu ama manne tujifunze pia.
Kwasasa siwezi Kaka ,hata nikisema niandike nitaijaza simu machozi au keyboard machozi .
Wacha nijipe muda ,nikiwa sawa nitasimulia .
 
Umaskini Kaka huwa unaanzia kichwani.

Pamoja na kwamba umembeba sana lakini bado habebeki.

Niliwahi kuishi Zanzibar kipindi fulani nikakutana na mzee mmoja amechoka mbaya. Wenyeji wakaniambia ni Kaka Yake Rais Wa Zanzibar wakati huo Dr Ali Mohamed Shein.
Yule mzee alikuwa kachoka anauza urojo.
Nikauliza imekuwaje Kaka yake Rais anakuwa na maisha magumj hivi? Yaani ndugu yakw ameshindwa jinsi ya kumnyanyua? Watu wanamlaum sana Rais Mstaafu Shein.

Lakini Deep Down ni kuwa huenda Shein alishajaribu mbinu zote za kumnyanyua lakini ikawa habebeki.

Ndio kama Hawa.

Ndugu wa Prof Kabudi ni Choka Mbaya kama ndugu wa Prof Kapuya.

Unaweza kuwalaum kwanini wanajipenda wao tu. Kumbe ndugu wenyewe ni wenye akili kama za huyo Mfanya kazi wako.

Kuna Ndugu uking'ang'ania kuwasaidia watakurudisha nyuma na wewe utakuwa maskini kama wao
Ni sahihi kabisa. Nina uhakika jamaa atajuta sana alikuwa hajawahi kuwaza atanunu smart akanunua na saivi hana yaani ni huzuni kubwa. Watu kama ukifanikiwa ndo wanakuwa wa kwanza kukuita wee ni free mason na ole wako upoteze hata mtoto aisee wanapitia hapohapo
 
Hapo makosa yapo kwa mwenye mali. Yeye hayupo kazini na kamtoa kijana wake nani awe na uchungu na mali zake? Aliweka mifumo dhaifu ya kuwezesha upigwaji. Cha mtu mavi.
Mi nadhani ni kwa vijana wa kazi mkuu. Kama unashindwa kusimamia mali ya mtu je ya serkali utaweZa kuwa muadirifu kweli? Imagine hadi mchungaji wake anaye mwamini kashindwa hata kumpa taarifa tu? kazi ipo sana asee
 
Back
Top Bottom