Hizi imani za kishirikina imekuwa Changamoto

Tariq f

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2021
Posts
233
Reaction score
347
Sina uhakika sana na wala sio wa muumini wa hivi vitu ila kama itakuwa kweli basi hizi imani zimekuwa changamoto sana hapa dsm

Nilikuwa katika harakati zangu za kutafuta fremu kwa ajili ya biashara na nikapata baadhi, kitu cha ajabu nilipokuwa nikiulizia kuhusiana na baadhi ya hizo fremu kwa watu wa karibu niliambiwa kuwa ili nifanye biashara hapo inabidi niwe mzito kwa mambo ya kishirikina la sivyo sitaweza, maana waliotoka nao walishindwa kutokana na kutojipanga kishirikina kwani hilo eneo si la kitoto

Fremu nyingine naambiwa hata kama nitapanga basi kazi bure maana mtaa huo ni wahuni ukifanya biashara hela yote wanachukua wakulungwa kwa hiyo lazima ujipange kisawa sawa

Najaribu kuwaambia kuwa imani yangu ni kwa mungu na naamini kwenye dua lakini jamaa wamekuwa wagumu kunisisitiza kuwa kujipanga kishirikina ni muhimu kwani waliotoka na kula hasara walikuwa ni kama mimi

Nabaki nachoka sana huku nikijiuliza inakuwaje haya masuala, au mimi nd mjinga wenzangu wote wanaofanya biashara wanatumia ushirikina!!??

Sijaelewa haya mambo mpaka naanza kuogopa sasa hili jiji lipoje
 
Mkuu kama Una Nia ni mda wako wa kudhihirisha Imani Kwa Mungu wako , hakuna shujaa anahetokea bila mapambano , dhibitisha sasa Imani unayoiamini , ingia mzigoni vunja frem , piga kazi Kibabe .... Japo ni kweli watu wengi wanaroga kinyama , Ila wew simama upande unaouona ni sahihi..utatoboa tuu mkuu
 
Wenyeji wamekuambia. Wenyeji wa kuwaheshim mno
 
Eeh kikubwa afanye hivyo afu tuone sasa una imani alafu unakuja kulialia humu what is your take care about your mobile
 
Nashkuru kaka
 
Matapeli wa mjini huimbaga mapambio kuwa "kwa Mungu ni tambarare"

Ufalme wa mbinguni wenyewe utarithiwa na Watu mahodari, tangu lini Hodari akapatikana bila ya vita/mapambano [emoji848][emoji38]
 
mungu [emoji777] Mungu [emoji736]
 
mkuu ujue over 90% ya watanzania ni waamini wa dini, wanadai wanamwabudu Mungu. Na ujue kati yao hao zaidi ya 75% ni washirikina. siku za ibada wanajaa makanisani, misikitini na kwenye majumba yao ya ibada. Lakini wakibanwa kidogo tu hao mbio kwenda kwa wachawi, hawamkumbuki Mungu.
 
Aisee!! Maisha yanaenda kasi sana
 
Watanzania tunaishi kinafiki sana. Dini imekuwa kama fashion tu ila kwenye matatizo yao wanakimbilia kwa masangoma, ila iseme vibaya dini yake anahasira hata kukukata panga wakati ni muumini jina tu hafuati makatazo ya Mungu kuhusu ushirikina . Anaona Mungu anachelewa kujibu maombi na ukimshtukia anarejea maandiko kwa tafsiri potofu ya '' JISAIDIE NAMI NITAKUSAIDIA''
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…