Hizi ndio Taasisi zenye mishahara minono Tanzania

Nimekuelewa mkuu.
Ila hii nchi ina uonevu.
Form four anampita mshahara mtu mwenye degree.
Dahh
Hahaha nchi ngumu hii majeshi siku hizi yameanza kujineemesha, ndio maana juzi hapa bungeni wametoa cheti cha jkt na jku kama kigezo kimojawapo cha kujiunga na majeshi, ili wapate kuingiza watoto wao ambao hawataki kusota jakata

Wakati zamani kazi za majeshi zilionekana ni za kizalendo na kimbilio la watoto wa masikini, na zilidharaulika sababu ya maslahi madogo, ila siku hizi wakubwa nao wanawapigania watoto wao waingie huko

Tena kama JWTZ ndio kabisa miaka hii hata hawatangazi wanaitana kimya kimya, unakuja tu kushitukia maaskari 3000 wameapa Kihangaiko, hujakaa sawa mara maafisa 500 wameapa Monduli ukiuliza wote wameingia kwa connection
 
Wanajeshi walianza kupiganiwa na kikwete ndio maana wana vitambi , Kikwete alitoa pesa sana ,kwanza wana mikopo mizuri kuliko hata walimu ... Kuanzia mwaka 2010 hata watu waliokuwa form six walikimbilia jeshini kwa sana ,kwa sasa sijajua kama wameongezew maslahi ila jamaa mpaka vitu wananunua kwa bei ya chini kweny maduka ya kambini.
 
Nimekuelewa mkuu.
Ila hii nchi ina uonevu.
Form four anampita mshahara mtu mwenye degree.
Dahh
Ni balaa polisi mwenye nyota moja na ana degree kumbuka mpaka kupata hiyo nyota kasota si chini ya miaka minne na bado anakunja 950k salary lakini jeshini form four tu anakunja million na zaidi. Hahaha maisha hayapo fair kabisa yani
 
Na siku hizi uafisa unapatikana kama karanga.
Zamani MONDULI kulikuwa na intake moja tu mwaka mzima, sasa zinapishana 3 mpaka 4.
Rais kila robo mwaka anaapisha maafisa ambao hawazalishi chochote.
Pesa nyingi zinapotea kizembe kwenye nchi maskini ambayo licha ya kujaaliwa kila kitu bado umeme ni tatizo
 
Kuko njema
 
Ni balaa polisi mwenye nyota moja na ana degree kumbuka mpaka kupata hiyo nyota kasota si chini ya miaka minne na bado anakunja 950k salary lakini jeshini form four tu anakunja million na zaidi. Hahaha maisha hayapo fair kabisa yani
Polisi wanakula Kaz ngumu mno kuliko maslahi yao
 
Unajua mishahara ya junior officers Tpdf?

Sent from my SM-G998B using JamiiForums mobile app
 

Yeah makambini kwao vitu vingi vinauzwa kwa nusu bei, na maslahi yao yaliongezwa pia, ukishakuwa afisa tu unapewa mkopo kwa lazima
 
Ndugu hawa vijana wanapelekwa vyuo tofauti hapa nchini na nchi za nje.
Karibu kila baada ya miezi 3 au 4 wanamwagwa makambini.
Yes si wote wanapata mafunzo MONDULI lakini hukutana mwishoni kwa kutambuana na kufanya rehearsal pamoja kabla hawajavalishwa uchawi (nyota).
Unaweza kunieleza zaidi maana Mimi sio mjeshi na sijui mengi ya huko
 
Yeah wapo wanaopata course monduli na wengine nje, ila mwisho wa siku lazima wakutane kwenye graduu ambayo ni mara moja kila mwaka, kambi inayoweza kutoa intake zaidi ya moja kwa mwaka ni rts ya maaskari ndio unaweza kukuta course mbili tofauti zinapigwa kwenye kambi moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…