Hizi ni baadhi tu za maneno ya hekima ya mzee Jakaya Kikwete

Hizi ni baadhi tu za maneno ya hekima ya mzee Jakaya Kikwete

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Hizi ni baadhi tu za maneno ya hekima ya mzee wa msoga.
1. Akili ya kuambiwa changanya na ya kwako
2. Kelele za chura hazimzuii mtu kuteka maji

Karibuni tuongezee zingine ikiwezekana tuweke na mazingira/context ambapo jkauli hizo zilitoka. kwa mfano kauli ya "akili ya kuambiwa changanya ya kwako" ilitoka wakati akiwaasa wafanyakazi wasimsikilize kiongozi wa TUCTA alipokuwa anawahamasisha kuanzisha mgomo wakishinikiza kuongezeka kwa kima cha chini cha mshahara.
Mzee wa msoga atabakia kuwa kipenzi cha wafanyakazi maana katika kipindi chake karibuni kila mwaka kulikuwa na ongezeko la mshahara na walimu wote waliokuwa wanamaliza vyuo walikuwa wanaajiriwa. watu husema mnyonge mnyongeni lakini haki nyake apewe! Namtakia mzee wa msoga maisha marefu yenye amani na fanaka!!
 
"Uwe na akili kama za Mbayuwayu"
"Lete maneno"
"Ukitaka kula lazima uliwe kwanza"
"CCM sasa hatuachiani maji mezani"


Mzee wetu yule, hana mambo mengi, No complications..aka Kijana wa Saigon, aka Msoga Inc, aka Boyz 2 men, aka Born town.
JK huwa anayajua mengi sana ya nchi hii ndio maana kuna kipindi anaishia tu kutabasamu refer alikuwepo toka enzi za JKN na Mzee Nyerere alimtambua kama kijana wake, alikuwepo enzi za Mwinyi, akahudumu kwa BWM ...
 
1. "Wanafunzi wanapata mimba kwa sababu ya kiherehere chao"
2. "Tutasheherekea miaka hamsini ya uhuru mwaka mzima"
3. "Ukiona unagombana na wenzio sababu ya uongozi ujue wewe hautoshi"(lilikuwa dongo kwa sofia simba)
4. "Mwanangu anasingiziwa tu"(akimtetea ridhwani sakata la bifu na masauni umoja wa vijana)
 
"Uwe na akili kama za Mbayuwayu"
"Lete maneno"
"Ukitaka kula lazima uliwe kwanza"
"CCM sasa hatuachiani maji mezani"


Mzee wetu yule, hana mambo mengi, No complications..aka Kijana wa Saigon, aka Msoga Inc, aka Boyz 2 men, aka Born town.
JK huwa anayajua mengi sana ya nchi hii ndio maana kuna kipindi anaishia tu kutabasamu refer alikuwepo toka enzi za JKN na Mzee Nyerere alimtambua kama kijana wake, alikuwepo enzi za Mwinyi, akahudumu kwa BWM ...
Nyerere alimtambua JK pamoja na Kinana akasema tunavijana wazuri ambao watatufaa huko mbeleni. Kama muasisi wa Taifa Hili alikua na Imani nao binafsi nakua na amani sana nikiwaona wazima wa afya tele najua nchi hii akiharibiki kitu.
 
Nyerere alimtambua JK pamoja na Kinana akasema tunavijana wazuri ambao watatufaa huko mbeleni. Kama muasisi wa Taifa Hili alikua na Imani nao binafsi nakua na amani sana nikiwaona wazima wa afya tele najua nchi hii akiharibiki kitu.

JK mwamba sana yule jamaa, sidhani kama Saigoni watapata mwamba mwingine kama yule...... Kijana mtiifu wa Saigoni....amejaribu kutengeneza vijana wengi lakini hawafikii kile kiwango chake.....

Namuona Riz anajaribu kufuata njia za mzee the good thing mentor ni mwenyewe....
 
Mzee wa msoga ni mzee wa kutabasamu!! Tanzania bado tunalihitaji tabasamu lake!! QAnajua kurahisisha mambo!! Wapinzani walimwita rais dhaifu yeye akacheka tu halafu walipompata JPM wenyewe wakamkumbuka JK!!
 
Upuuzi mtupu.

Wengi wenu humu ndy ninyi mliomlaum huyo mzee kwa upole wake kuwa anacheka na mafisadi na hajui kusimamia vzr viongoz wake.

Ndyo ninyi pia mlimlaumu kwa kuwaletea yule jiwe alye kwenda zake.

Mahaba ya kinafiki haya, waTz tuache unafiki jmn, unafiki si mzur, ama tufukue nyuzi zenu humu mlizokuwa mkimsema kwa mabaya?
 
Fu
Hizi ni baadhi tu za maneno ya hekima ya mzee wa msoga.
1. Akili ya kuambiwa changanya na ya kwako
2. Kelele za chura hazimzuii mtu kuteka maji

Karibuni tuongezee zingine ikiwezekana tuweke na mazingira/context ambapo jkauli hizo zilitoka. kwa mfano kauli ya "akili ya kuambiwa changanya ya kwako" ilitoka wakati akiwaasa wafanyakazi wasimsikilize kiongozi wa TUCTA alipokuwa anawahamasisha kuanzisha mgomo wakishinikiza kuongezeka kwa kima cha chini cha mshahara.
Mzee wa msoga atabakia kuwa kipenzi cha wafanyakazi maana katika kipindi chake karibuni kila mwaka kulikuwa na ongezeko la mshahara na walimu wote waliokuwa wanamaliza vyuo walikuwa wanaajiriwa. watu husema mnyonge mnyongeni lakini haki nyake apewe! Namtakia mzee wa msoga maisha marefu yenye amani na fanaka!!
fika uhamiaji haraka sana, hizi ndio maneno?? Kiswahili cha wapi hiko?
 
Upuuzi mtupu.

Wengi wenu humu ndy ninyi mliomlaum huyo mzee kwa upole wake kuwa anacheka na mafisadi na hajui kusimamia vzr viongoz wake.

Ndyo ninyi pia mlimlaumu kwa kuwaletea yule jiwe alye kwenda zake.

Mahaba ya kinafiki haya, waTz tuache unafiki jmn, unafiki si mzur, ama tufukue nyuzi zenu humu mlizokuwa mkimsema kwa mabaya?
Wanaume huwa hawakasiriki milele! tuache tufurahie ucheshi wa mzee wetu!
 
Back
Top Bottom