Hizi ni dalili za ugonjwa gani

Raj kapool

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2018
Posts
1,352
Reaction score
2,160
Aiseee salaam kwanza popote mlipo natanguliza shukrani
Mi ni kijana 24 years sina historia yoyote ya kuugua uhonjwa mkubwa wowote ule tofauti na homa ndogo ndogo za mafua na kikohoo labda,, sasa kuna dalili naziona ningependa kujua hii itakua dalili ya ugonjwa gani
,, nikikaa nimetulia upande wa kushoto mwa kifua changu pale usawa wa moyo hua kama kuna kitu kinatembea hapaumi ila panakua kama panabana ivi na kuachia hii hufika hadi nyuma kwenye mgogo usawa uleule upamde ule ule
Hii hutokea nikiwa nimetulia au nimelala ila nikiwa na shughuli haitokei hata ikitokea hua kwa dakika 1 tu
Nikitulia huchukua hata dakika 5
Wajuzi mnijuze jamani
 
i
Dalili ya mtu mwenye ugonjwa wa presha
Mara nyingi presha haina dalili hadi ilete madhara na hivyo huitwa( silent killer ) muuaji wa kimyakimya
kichwa kuuma
kizunguzungu
kubanwa na pumzi
kutokuona vizuri
kichevuchevu
Fanya sana mazoezi hiyo ni dalili ya pressure

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mazoezi yapi niongeze mkuu yawezekana ni tofauti na ninayofanya
Mazoezi yoyote ila yawe yenye faida kwako. Mfano kukimbia, kuruka kamba kucheza mpira. Mafuta yakiwa mengi mwilini ni tatizo na hakuna namna ya kuyapunguza kama hujafanya mazoezi haswaaa.

Lakini kumwona daktari wa moyo ni vyema zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ook asante
 
Mazoezi yapi niongeze mkuu yawezekana ni tofauti na ninayofanya

Kabla ujaandika soma umuelewe mtu kasema nini, anajuaje aina ya mazoezi unayofanya, unauliza maswali halafu tena unakuwa mjuaji kweli.....

Huyo ni dalili ya pressure, fanya vitu vyote ambavyo mtu hufanya kukwepa pressure au anapokuwa na pressure
 
Kabla ujaandika soma umuelewe mtu kasema nini, anajuaje aina ya mazoezi unayofanya, unauliza maswali halafu tena unakuwa mjuaji kweli.....

Huyo ni dalili ya pressure, fanya vitu vyote ambavyo mtu hufanya kukwepa pressure au anapokuwa na pressure
Broo kwani kujua aina ya mazoezi ni kosa? mbona kaishanijibu fresh tu kanielewa ila we ndio hujaelewa
 
Mkuu hizo ni hatua za awali za HEART BURN itakayokupelekea kupata vidonda vya tumbo
hii usababishwa na wingi wa ACID tumboni au BACTRERIA wa H pylori

kupata presha au ugonjwa wa moyo si rahisi kama watu wanavyofikilia
Moyo ni kifaa strong sana kama hujazaliwa na hitirafu yoyote ya moyo au kupata ajari ukadamage moyo directy ni ngumu sana hasa kwa vijana kupatwa ugonjwa wa moyo
km utakuwa unazingatia chakura unachokura kuwa makini na life staili yako unavyoishi na kuzingatia kanuni za afya

na moja ya kanuni ya AFYA inayotumaliza vijana wengi ni kunywa dawa bila kujua ugonjwa halisi unaotusumbua wengi wetu tumekuwa wabahiri sana kupima vipimo tunapojihisi maradhi

Ila Moyo unaweza kushinda fanya kazi ipasavyo kutokana na maradhi fulani fulani
Mfn kama hvyo wadudu wa h pylori au wingi wa ACID tumboni nk
Kwa hiyo moyo kushindwa kufanya kazi inavyopaswa haimaanishi MOYO wako una hitirafu lah !
Bali usipotibu au kung'amua
(mana magonj'wa mengne hayahitaji hata kumeza dawa ni kubadili tu mfumo wa maisha hususani chakura tunachokura kila siku ni tiba tosha)
kinachosababisha MOYO kutofanya kazi ipasavyo basi hapo ndo unanunua matatizo ya moyo halisi

Kwanza Nenda upime H pylori na kiasi cha ACID tumboni
Lakini unaweza kuchukua hatua za awali acha kubeba vitu vizito badili mfumo wa chakura Punguza kura vyakura vyenye ACID kwa wingi hasa SODA achana nazo kabisa kama mnywaji pombe acha kabisa kuwa more relaxed(punguza mawazo) fanya mazoezi mepesi mepesi mara kwa mara

USIKUBARI MADAKTARI KUKUANDIKIA DAWA YOYOTE BILA KUPIMWA NA KUJUA KIPI KINAKUSUMBUA WATAKUTIA HASARA NA KUKUZIDISHIA MATATIZO ZAIDI

HUO UGONJWA UKIPAMBA MOTO UNAKUWA NA DARIRI ZOTE ZA MTU MWENYE UKIMWI au TB




Soma Angalizo: Baadhi ya dalili za vidonda vya tumbo hufanana na dalili za magonjwa ya moyo - JamiiForums

Nimeambiwa sina vidonda vya tumbo, nina hpylori tu, iweje nisikie kiungulia(Heart burn) - JamiiForums
 
Ndugu,
Naomba unijibu swali hili kabla sijaendelea.
Umepatwa na tatizo lolote linalokusababishia kuwaza sana hivi karibuni?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…