Hizi njemba(hawa ma-legend) za JF zinatufanya kizazi cha sasa tuonekane tuna upeo mdogo wa kufikiri

Hizi njemba(hawa ma-legend) za JF zinatufanya kizazi cha sasa tuonekane tuna upeo mdogo wa kufikiri

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Nimeanza kufuatilia JF tangu 2010 hivyo mpaka sasa ni miaka 12. Hivyo ninauzoefu WA kutosha na mambo ya humu ndani. Ingawaje kipindi kile yaani 2010-2013 nikiwa sekondari nilikuwa Kama msomaji tuu lakini bado ninakumbukumbu nzuri ya mambo yalivyokuwa.

Nakiri kuwa humu JF kuna miamba inatupa chakufanya kizazi cha sasa. Ili kutopoteza muda nitataja njemba/ma-legend/ miamba 20 ya JF inayowakilisha vyema kizazi cha Kaka au Baba zetu. Ninaposema Kaka au Baba zetu nijazungumzia watu wote waliozaliwa miaka kuanzia 1960 - 1989.
Sisi wa 1990 mpaka Leo tujiite ndio kizazi cha Leo.

Miamba au njemba hizo ni Kama ifuatavyo;

1. Mshana Jr ( Mzee wa Vilinge, Lozi la kimataifa)
2. Pascal Mayalla. (Mzee wa Kura moja)
3. Malcom Lumumba (
4. Gudume. (Mzee wa Fix na Storyteller)
5. Vuta Nkuvute ( Kwa sasa Dodoma)
6. Kiranga. ( Mzee wa metaphysics)
7. Barafu
8 Nguruvi3 (wakimataifa)
9. Mzee Mwanakijiji
10. NyaniNgabu ( USA Baby)
11. MsemajiUkweli
12. Habíb Hanga ( The Bold)
13.. MTAZAMO
14. Mag3
15. Bujibuji (Simba nyatiaji)

Hao ni wawakilishi WA kizazi cha Kaka na Baba zetu.
Embu linganisha vitu wanavyoandika, namna wanavyoandika, alafu linganisha na siye watoto wa 1990 mpaka hivi leo.
Ndio utajua Sisi bado tunakunywa Uji wa Mgonjwa. Yaani bado uwezo wetu ni mdogo Sana WA kufikiri na kupokea mambo.

Yaani Storage yetu ipo chini.
Sio ajabu watu kulalamika nyuzi zikiwa ndefu,
Nataka kukuhakikishia Makala nyingi zilizondefu ndizo zinazoweza mfanya mtu awe na contents nyingi kichwani.
Kadiri unavyosoma vitu na mambo mengi ndivyo akili yako inavyozidi kupanuka na kutanuka.
Akili yako lazima Uizoeshe kusoma vitu vizito, virefu, na kuweza kuviweka akilini na kuvichambua.

Kuna Taaluma hauwezi Kuhitimu Kama akili yako imezoea vitu vifupifupi au maandiko mafupi fupi mathalani;
Uanasheria, uinjinia, udaktari, Falsafa, uchambuzi wa maandiko n.k.

Ukiona mtu anachoka mapema kusoma maandiko marefu ujue ubongo wake ni Low Storage.
Jambo moja nataka nikuibie Siri, ukiona mtu yeyote ana-content nzito na kubwa kichwani elewa huyo ni msomaji wa vitu virefu na vizito.
Mtu yeyote Yule ukiona unamu-appreciate kuwa Anauwezo mkubwa wa kufikiri au Akili au kuchambua mambo elewa kuwa Siri ni kusoma vitu virefu na vizito.

Kadiri unavyosoma Sana ndivyo ubongo wako unavyozidi kutumika na kuwa Bora zaidi.

Hongereni Sana Kaka na Baba zetu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Halafu unaposema sisi kizazi cha miaka ya 90 unamaanisha nini? Kuna watu wamejiunga JF miaka ya karibuni, na bado hawapo kwenye kizazi chenu cha miaka ya 90!

Sema tu nyinyi madogo mnapenda sana kutukana tukana hovyo kila mtu aliye mbele yenu. Halafu mna u much know sana.
 
Halafu unaposema sisi kizazi cha miaka ya 90 unamaanisha nini? Kuna watu wamejiunga na JF miaka ya karibuni, na bado hawapo kwenye kizazi chenu cha miaka ya 90!

Sema tu nyinyi madogo mnapenda sana kutukana tukana hovyo kila mtu aliye mbele yenu. Halafu mna u much know sana.
Naomba nimsaidie kujibu,

Aliposema kizazi cha tisini kamaanisha waliozaliwa kuanzia 1990 mpaka miaka ya 2000

Sisi tuliozaliwa kuanzia 1989 kurudi nyuma hatupo

Alimaanisha miaka ya kuzaliwa sio ya kujiunga/kutumia jamii forum
 
Halafu unaposema sisi kizazi cha miaka ya 90 unamaanisha nini? Kuna watu wamejiunga JF miaka ya karibuni, na bado hawapo kwenye kizazi chenu cha miaka ya 90!

Sema tu nyinyi madogo mnapenda sana kutukana tukana hovyo kila mtu aliye mbele yenu. Halafu mna u much know sana.

😀😀😀
Tuna-stress zetu lazima tuwatukane ili tuwe wote Sawa.

Vijana wa siku sio kwamba ni much know Bali ni wapumbavu, hawana wajualo wanashindwa mpaka na vitu vidogo tuu
 
Mshana Jr sio mzee ana miaka 40 tu sasa huyo mnamuitaje legend sema yupo na Maarifa Mengi kwa kichwa

Unafiki kufikisha miaka 40 ukabaki timamu wa Akili ni KAZI ndogo?😀😀😀
Angalia Vijana wa sasa miaka 25 tuu mtoto maisha yashamtoa Knockout, kijana kachanganyikiwa, wengine wanataka kujiua, wengine wamejiingiza kwenye ushoga, wengine madawa ya kulevya, n.k.

Miaka 40 alafu mtu bado yupo timamu huyo ni Legend.
 
Back
Top Bottom