Hizi simu....mmmh!

HII KALI JAPO SIO REALISTIC,UNAANZA KUPOROMOSHA MATUSI BILA KUSIKILIZA UNAONGEA NA NANI?HUYO JAMAA ATAKUWA CHIZI AU ALIKUWA TUNGI LA gongo NA MSUBA MWINGI
 
mpe pole sana. I hope amekoma, hatarudi tena
 
Mke na nyumba ndogo ni sawa, mume na nyumba ndogo mume nayo je? Mbona sioni watu mkisema aachane na mambo ya nyumba ndogo?
 
Hahahaa, mimi kuna siku nilikuwa nimekaa na rafiki yangu tunakula weekend mahali, Sinza. Jamaa siku hiyo alikuwa na furaha sana maana alikuwa amelipwa hela kwenye tender fulani aliyokuwa ameifanya. Akaniambia "leo fulani (akamtaja msichana ambaye amekuwa akimsumbua kila siku) lazima anikome. Ngoja nimwite hapa, atakuja tu". Akaandika ujumbe "Mama mpenzi wangu...(akaandika jina la msichana), njoo hapa (akataja tulipokuwepo) upate unachokitaka, nitakuwekea mafuta ya 100,000/= kwenye gari yako, leo hutajutia kukaa na mimi....akamalizia "I love you so much sweet". Jamaa alivyo ***** na nadhani alikuwa anaitesa sana familia yake kimahitaji hivyo Mungu akaamua kumwadhibu, si akaituma kwa MKE WAKE. In seconds akajibiwa navaa baby, nakuja sasa hivi, ni mimi ...(akaandika jina la msichana aliyetajwa kwenye simu" Jamaa kuja kugundua amemtumia mke wake, mkojo ukamtoka. Akasimama akashidwa, akaniambia "nimeshaharibu". Akaweweseka, akaingia kwenye gari, alivyorudisha nyuma ili atoke, akamgonga aliyekuwa nyuma yake, zikamtoka 170,000/= za kutengeneza. Nikamwambia sasa unaniachaje hapa Mkuu wakati wewe ndo ulinipigia nije una hela leo. Alinifurumishia matusi mpaka baa nzima ikataharuki. Currently the man is no longer with his wife. Take care my friend with mobile phones usage.
 
Hebu mpelekee huyo jamaa sheria zetu mama, na azingatie kwa kina Sheria namba 12. Nimemwekea Link Hapo. Waweza kumprintia kama hana access na net.

https://www.jamiiforums.com/mahusia...jue-sheria-mama-za-infidelity.html?highlight=
 
Hii nayo kali, inabidi kuwa makini na hizi simu!
 
Huyo jamaa yako hajasettle teh! teh! Kigogo-Luhanga nin?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…