Hodi hodi kutoka kwa Kiranga

Hodi hodi kutoka kwa Kiranga

BrantCawen

Member
Joined
Nov 20, 2010
Posts
25
Reaction score
2
Ndugu zanguni wajuvi, wadadisi na wengineo,

Mie ndugu yenu Kiranga cha Ngeda wa viunga vya bandari iso salama, Kiranga wa upande wa Mbwamaji, Kiranga wa Mkuranga,kakae Muamini na mwana wa Fundi Shomvi na Sikudhani binti Muhamedi.

Mara nilivyotoka pande za Msanga Kisiju nikaambiwa ukishangaa maajabu ya Rufiji gari kupita juu ya mto hutafika Utete wala Mpwapwa, zaidi ya hapo maendeleo siku hizi yako huku bandari iso salama kwenye majumba yaliyopandiana, nikachungulia nikaona kweli mnafaudu, hata Mbagala na Charambe tu harufu wanaisikia, na mimi nikaona niombe kugonga hodi hodi mnikaribishe mlionitangulia.Nisambe nimenyimwa maji wakati kisima chatitiri.

Salamu sana kutoka Msanga Kisiju, Kilwa Pande, Kilwa Kivinje, Kilwa Kisiwani, Songo Songo, Somanga, Muhoro mpaka pande za Sala Sala na Mkuranga.Ningewatumia pepeta na mabumunda ya motomoto lakini nimeambiwa humu naweza kutuma picha tu, na mie kamera sina, labda siku nyingine wakija wapima viwanja na midarubini yao ile nitawaomba wanipige picha niiweke muone ninavyofukuzana na ngedere na kima. Sasa niage nikimbilie kuangalia hesabu za minazi maana wakwezi na komba hawakawii kumuadhiri mwenzenu huku. Baada ya hapo mkiniona kimya mjue safari ya Mafia imewadia.__________________________
mother of the bride dresses
discount wedding dress
mother of the groom dress
 
Kiranga wa Mkuranga
Kiranga wa Mkuranga na Brant wa Cawen wapi na wapi?

Umelimbukia mizungu ukakataa majina ya babu zako, soni na karaha.

Mtwa Mkwawa aliwakata mutwe wacharambe kama nyinyi.
 
Karibia, Sema pepeta nazimiss!!!! sijaziona zaidi ya miaka kumi, jamani wakija wapima ramani, nifungashie kidogo nikumbuke enzi za mwalimu.
 
Najisikia kuchanganyikiwa hapa. N'way karibu BrantCawen a.k.a Kiranga cha Ngeda wa viunga vya bandari iso salama, Kiranga wa upande wa Mbwamaji, Kiranga wa Mkuranga,kakae Muamini na mwana wa Fundi Shomvi na Sikudhani binti Muhamedi!
 
Wewe BrantCawen huna adabu kweli,

Yaani umeenda kuichukua post yangu ya mwanzo kabisa niliyojitambulishia hapa na kuituma tena kwa jina lako, watu wengineutawachanganya wafikiri mie na wewe ni mtu mmoja.

Ingawa umenikumbusha mbali sana kwa kurudisha utambulishi wangu, nakuomba uieleze jamii wazi kwamba mimi na wewe ni watu tofauti, na labda utueleze ni kwa nini umerudisha post hii.


Original post iko hapa
https://www.jamiiforums.com/utambulisho-member-intro-forum/23684-hodi-hodi-kutoka-kwa-kiranga.html
 
Wewe BrantCawen huna adabu kweli,

Yaani umeenda kuichukua post yangu ya mwanzo kabisa niliyojitambulishia hapa na kuituma tena kwa jina lako, watu wengineutawachanganya wafikiri mie na wewe ni mtu mmoja.

Ingawa umenikumbusha mbali sana kwa kurudisha utambulishi wangu, nakuomba uieleze jamii wazi kwamba mimi na wewe ni watu tofauti, na labda utueleze ni kwa nini umerudisha post hii.


Teh teh teh teh, hakuna marefu yasokuwa na ncha. Sijakubamba nimekubamba.
 
Teh teh teh teh, hakuna marefu yasokuwa na ncha. Sijakubamba nimekubamba.
Bwe he he he..kwa hiyo kumbe ulianzisha hii thread kumchokoa huyu mzee wa 'Theory of Everything'
 
Bwe he he he..kwa hiyo kumbe ulianzisha hii thread kumchokoa huyu mzee wa 'Theory of Everything'

Hahaha, eti Theory of Everything, string theory wanavyozidi kuichimba ndivyo wanaona mi dimensions inazidi, theory of everything is an elegant idea, but until you reconcile quantum physics na cosmology, you have absolutely no hope of a Theory of Everyting, because the realm of the very small (quantum physics) ni tofauti sana na the realm of the very larege, quantum physics rule the former while gravity rules the latter.

Einstein died trying to reconcile the two and couldnt, nobody has done it.
 
Hahaha, eti Theory of Everything, string theory wanavyozidi kuichimba ndivyo wanaona mi dimensions inazidi, theory of everything is an elegant idea, but until you reconcile quantum physics na cosmology, you have absolutely no hope of a Theory of Everyting, because the realm of the very small (quantum physics) ni tofauti sana na the realm of the very larege, quantum physics rule the former while gravity rules the latter.

Einstein died trying to reconcile the two and couldnt, nobody has done it.

Kaka mi nilidhani wewe tayari umeshaifyatua ! bado tu kumbe?? lol
 
Nami nilikuwa najiuliza huyu new commer mbona mjanja sana inaelekea ni mwenyeji fulani. Kumbe Kiranga!!
 
Kaka mi nilidhani wewe tayari umeshaifyatua ! bado tu kumbe?? lol

Kaka huwezi kufyatua visivyofyatulika, huwezi kufanya visivyofanyika just because some Asimov, Wells, Hugo, Clarke or Adams ali pen a popular SF item back in the days.

Why should natural laws converge all the way to a single point? After all, even if you take the standard model of theoretical physics and it's big bang, ukasema big kila kitu tunachoweza kuki measure kinatoka katika point moja ya big bang, the big bang is a singularity by definition, and all known laws break down there.

It is an interesting proposition, I am even prepared to entertain the notion that all natural law stemmed from the same nugget of spacetime, but that does not mean we must be able to find something today that can encompass all.

DNA ya natural law katika cosmogony ina exhibit convergence, kama kuna somo tunaloweza kujifunza kutoka maisha ya Einstein ni kwamba kutafuta ku reconcile gravity na quantum physics (the holy grail of Grand Unified Theory) kwa technology yetu hii ya sasa ambayo haiwezi hata kutest string theory, ni kupoteza muda tu. Einstein angeweza kufanya mambo mengine mengi ya maana sana kama angeachana na hii illusion.

A grand unified theory was in the history of cosmogony, at the singularity, unless one can study a singularity sufficiently, hii habari ni more SF than science.

Now I know I meant it like " Mr. know it all" and not necesarily GUT per se, but you touched a subject I have much passion about, so there you are. It is sad when someone shows a little average knowledge, amongst ourselves he is taken to be "Mr. Know it all"

Those who know at least know that they don't know.
 
Kisha huyu Kiranga cha Ngeda Sangala Kandumbwa kabadilika ghafla, kutoka kukimbizana na komba hadi kukimbizana na Grand Unified Theory!

Kweli bandari isiyo salama si mchezo
 
Back
Top Bottom