Hofu ya CCM na wana CCM kuhusu Katiba

Hofu ya CCM na wana CCM kuhusu Katiba

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
9,571
Reaction score
35,475
Ukweli siku alipokufa nilifurahi, sikufurahia kifo chake, bali nilifurahi kwa sababu ameondoka kwenye kiti cha taifa. Nilifurahi kapisha kiti hicho kwa sababu Mimi nilimuona hakufaa kukalia kiti hicho.

Alikua ana uwezo lakini hakufaa. Kwa sababu gani alikua ana uwezo lakini hakufaa Nina sababu nyingi mno. Lakini chache ni hizi. Kazi kubwa ya Rais ni kuiunganisha nchi yaani kuwafanya raia wawe wamoja, hakua na dhamira hiyo, hakua na uwezo huo.

Kama ni ujenzi wa miundombinu, waliomtangulia walijenga na watakaokuja baada yake watajenga. Hakufata katiba, sheria, kanuni, miongozo, Mila na desturi zetu tulizojiwekea.

Ningefurahi pia kama angeondoka madarakani kwa njia yoyote ile. Furaha yangu sio njia ya kuondoka,furaha yangu Ni kupisha kiti.

Ningefurahi angeondolewa kwa nguvu,

Angejiuzilu,

Angeugua,

Angekubali kushindwa na namna nyingine yoyote ya kuondoka, mimi ningefurahi tu.

CCM ndio chama dhaifu Sana hapa nchini na Duniani kote, lakini Ni miongoni kwa vyama vyenye propaganda kubwa na uongo mwingi Sana.

Sababu kubwa ya CCM na wafuasi wake kuikataa katiba Bora ni hofu ya kutoka madarakani.

CCM inadanganyaga watu kuwa inapendwa,imeshinda kwa kishindo,Marais wake wanapendwa lakini pamoja na kujitekenya yenyewe hucheka yenyewe. CCM hakiwezi kuruhusu kuleta kwa katiba itakayotoa haki kwa sababu itapelekwa Shimoni kwa speed ya 6G.

Hivyo basi kila kiongozi kutoka Chama hicho huogopa kuleta katiba Bora kwa sababu anaogopa lawama za kuwa Raisi aliepelekea CCM kuondolewa madarakani.

Wao hawaangalii maslahi mapana ya Taifa,hawaangalii iko siku nchi inaweza kuingiza machafukoni kwa sababu ya katiba hii ya sasa kutokua bora.

Kwa hiyo viongozi wetu hawa wanawazaga chama tu badala ya nchi. Chama kinaweza kikafa lakini nchi ikabaki. Mfano KANU haipo kivile lakini KENYA inastawi.

Samia nilimshangilia Sana, sio kwa sababu ni mtu anefaa sana, hapana, kwa sababu alikalia kiti kilichoachwa na mtu ambae kwangu Mimi hakufaa. Nilimfurahia Samia kwa sababu ya kuwazomea wafuasi wa yule. Nilimfurahia kwa sababu sasa ndoto za kutawala milele zimezikwa rasmi. Nilimfurahia kwa sababu Naamini hawezi kuwa na tabia za ajabu kama za yule.

Ila nilijua na ninajua Samia ni zao la CCM na CCM na katiba ni kama Binadamu na corona19. Binadamu anaiogopa korona kwa sababu inaua,na CCM anaiogopa katiba mpya kwa sababu itamuondoa.

Na kwa sababu Samia ni zao la CCM,na Viongozi wa kutoka CCM hawana ujasiri kama aliokua nao Fredrick De Klerk aliewahi kuwa Rais wa mwisho Kaburu wa Afrika KUSINI.

Samia anaenda kupuuzwa kwa Kasi ya mwanga. Atachekwa na kupuuzwa na Magufuli Gang, atapuuzwa na wastaarabu wote duniani.

Kitu pekee Cha kufanya ili Jina lake kubaki hai milele na milele kama Shujaa wa kweli wa Tanzania na Afrika Ni kuwa upande wa wananchi na kuachana na kikundi kidogo tu ndani ya CCM.

Atumie Maguvu ya Urais aliyonayo kuleta katiba,atumie ubabe wa Urais kwa manufaa ya nchi sio kama Yule alitumia Maguvu kwa faida binafsi. Mama Jina lake litaishi Miele kama akileta katiba Bora.

Wapo watu Kama akina Fredrick De Klerk ambao wanakumbukwa kwa kuifanya SA kuwa Taifa Moja. Kikundi kidogo Sana Cha Makaburu wachache kilimpinga,lakini Makaburu wengi na Dunia vilimuunga mkono.

Karibu Samia suluhu Hassan. Usiruhusu kuingia kwenye Historia ya akina Mwendazake na Ben waliokuja kujuta na kuomba misamaha ikiwa too late.

Walikua na nguvu wakazitumia kwa kufanya ujinga.
 
Inahitajika wazalendo watakaochukua kuhakikisha nchi inapata Katiba yenye kuleta haki, usawa na umoja kwa wote pamoja na kuchochea maendeleo kuondokana na umaskini uliodumu kwa zaidi ya nusu karne.
 
Lea maoni Mama tumuache naamin ataleta katiba mpya ktk kipindi chake cha pili cha uongozi kama alivyofanya JK tumpe muda
 
Eti kwa sasa tunajenga uchumi kwanza!! Mama amezingua kama mtangulizi wake. Bora hata angeahidi kuurejesha ule mchakato kabla ya 2025.

Ila hata wafanyeje! Tutaendelea tu kudai Katiba Mpya! Hatutachoshwa kamwe na kejeli zao. Tumeanza kuidai kwa kutumia njia ya amani. Nani ajuaye kitakachotokea siku za baadae?

Nguvu ya umma ikiamua tu, kinaeleweka.
 
Ili tufanye vizuri zaidi kwenye mchakato huu wa katiba na upatikanaji wake uwe ni rahisi

Hisia za kisiasa ni kuziweka kando kabisa,

Kwani, Wakati chama kikionekana kuwa mbele kudai katiba, kuna baadhi ya wananchi wasiokuwa wa chama hicho ama wale ambao hawana kabisa chama, wataamini tu kuwa, hili ni takwa la kisiasa, na Mh Raisi ataona ni wapinzani wake waonadai katiba kitu ambacho anadhani kitawanufaisha wao, asiione sura ya utaifa kwa kuwa kelele za katiba mpya zinatoka upande wa mmoja tu tena ni chama

Maana yake sasa, Kinachotakiwa, ni kujitokeza makundi yasiyoegemea chama chochote, ili kulifanya jambo hili kuonekana ni hitaji la watu wote

La sivyo, Mtapuuzwa tu
 
katiba sio msaafu au bible.

wakati ambao wewe na wengine mlifurahi rais kufia madarakani,tuliwasihi sana kwamba furaha yenu ni kama mshindo wa kufika kileleni tu,haitachukua hata mwaka mmoja mtaanza kulia tena,sababu moja ni kwamba hamjui adui yenu ni yupi.

1.kama adui ni utawala bora basi mnatakiwa mjijenge katika kushauri na kufanya kwa mfano.

2.kama adui ni ccm,basi magufuli kama mtu yeye hakuwa wa kutupiwa mawe,mlitakiwa mrudi no moja hapo.

3.kama adui ni kufinyangwa kwa katiba,basi dawa si kuileta nyingine,bali kuhimiza hii ifatwe kwa busara.

sababu ya kutotambua adui kimkakati inasababisha kurukia kila jambo linalopita,mfano kwa sasa,baada ya mzee kufariki mkahisi mama ndiye masihi,nayeye kawabwaga.kwa kauli moja tu.
 
Ccm wana hofu ya kupoteza privilege waliyonayo sasa ya kuamua nani awe raisi na nani awe mbunge....uimara wa ccm kwa sasa umeegemea hpo ikitokea ikaundwa katiba mpya yenye tume huru ccm watakuwa na hali mbaya sana

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
hata simba huwa ana himaya yake,huhakikisha anaua kila mnyama ambaye anaweza kuwa anasumbua katika mawindo eneo lile.

ujinga ni kudhani simba na fisi wana uwezo sawa.
 
Duniani kote katiba mpya hupiganiwa. Haiombwi! Kwasabb katiba bora ni sawa na msumeno mkali unaokata hata chama tawala.

Kwahiyo kamwe hawataweza kukubali kuunoa msumeno ili uje kuwakata

Bila kupigana tutakaa sana!
 
Natamani watu wangetambua kuwa Tanzania ipo, ilikuwepo na itaendelea kuwepo bila wao. Na wajitahidi maamuzi yao wanayofanya yawe ni kwa maslahi mapana ya Tanzania kuliko kukinufaisha wao Binafsi.

Kifo cha John walau kitufundishe kuwa sisi ni wapitaji tu, ila nchi itabaki. Tusijione wa muhimu zaidi kuliko Nchi yetu na wananchi wenzetu.
 
Wapo watu Kama akina Fredrick De Klerk ambao wanakumbukwa kwa kuifanya SA kuwa Taifa Moja. Kikundi kidogo Sana Cha Makaburu wachache kilimpinga,lakini Makaburu wengi na Dunia vilimuunga mkono.
Friederick De Klerk aliesimama na kuikomboa SA kutoka kwenye DHAMBI kubwa waliyokuwa wakitenda dhidi ya sehemu ya wananchi wake, hakika ataenda peponi.
-Kutokana na maguvu ya dola aliyokuwa nayo kama Rais, angeweza kabisa kufanya lolote ikiwamo hata kujipa au kuwapa vibaraka wake, ushindi wa kishindo ili kuendelea kutawala anavyotaka.
-Tofauti na matarajio/mategemeo ya wengi DUNIANI, alikubali kuupoteza hata URAIS aliyokuwa anaushikilia ili kuanza kuleta maridhiano na AMANI.
-Kama kweli anapenda nchi hii, Mama bado anayo nafasi ya kujifunza kutoka huko.
-Kutoka moyoni mwangu ninamuomba Mungu amuongoze ili aweze kuwa na busara hiyo ili tujenge Tanzania isiyo na UBAGUZI.
AMEN
 
Unaweza kuwa na hoja lakini baadhi ya mtazamo wako unatia Shaka. Unapodai CCM ndio chama dhaifu Zaid Nchini na Duniani sikuelewi. I'll kukuelewa inabidi uwe taahira kuona mantiki ya hoja hii
 
Katiba mpya linapaswa kuwa Jambo muhimu Sana kwa mustakabali wa taifa letu
 
Back
Top Bottom