Hofu ya kufa imefanya dunia ianze safari ya kiama

Hofu ya kufa imefanya dunia ianze safari ya kiama

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Utabiri wa mwisho wa dunia umetolewa miaka mingi na mbali mbali huko nyuma.Utabiri wa namna hiyo ulipita na kuondoka na baadae watu kurudi kwenye shughuli zao na starehe zao kama kawaida.

Tangu kuzuka kwa corona binadamu wamepatwa na hofu iliyo kubwa kiasi kwamba wale waliozowea kuona dunia kama sehemu ya kustarehe wameingiwa na hofu kubwa sana kiasi kwamba wanakufa kwa hofu kabla ya corona.

Wale matajiri wa dunia na wenye fedha nyingi hasa Ulaya na mashariki ya kati wameona ugonjwa huu umewakatishia furaha zao.

Wamejiona hawana pa kutokea hasa kila kukicha wanapata taarifa za wimbi la kwanza na la pili na la tatu linafuatia.

Pamoja na kugunduliwa kwa chanjo mataifa tajiri wanaona haitoshi na wanazidi kujifungia ndani ya majumba na mipakani mwa nchi zao. Dunia imegeuka sura na kuanza kujivisha kiza cha siku ya kiama.

Mwenyezi Mungu azidi kutuhofisha na iwe sababu ya kumuogopa na kuachana na upuuzi wa dunia wa kudhulumiana na kufanya ufisadi wa kila namna.
 
Tanzania tumezoea shida wala hatuna hofu nabkicorona chao, maisha yetu tu ni covid 25
 
Chinese virus kama anavyotambuliwa na Trump kaikalisha chini Dunia

Hapa kwetu alimchukua mkapa,Burundi kawachukua wale madikteta wastaafu
 
NADHANI KUNA AGENDA KUBWA SANA NYUMA YA HILI SUALA LA CORONA.NI MUDA TU UTATUPA MAJIBU
 
NADHANI KUNA AGENDA KUBWA SANA NYUMA YA HILI SUALA LA CORONA.NI MUDA TU UTATUPA MAJIBU
Inawezekana kwani mwanzoni Trump alisema yeye anafahamu na mpaka leo hataki kuchomwa sindano ya chanjo na barakoa anavaa kwa kulazimishwa.
 
Inawezekana kwani mwanzoni Trump alisema yeye anafahamu na mpaka leo hataki kuchomwa sindano ya chanjo na barakoa anavaa kwa kulazimishwa.
Jana nimeona clips za viongozi wawili wakubwa wa nchi za magharibi "wakichomwa" sindano za chanjo hiyo kimagumashi. Unaona kabisa viongozi wenyewe hawana imani na chanjo hiyo lakini wanahadaa watu wao na ulimwengu mzima kuwa wao wamechanjwa ili raia nao wachanjwe.

Huku ni kuusaliti ubinadamu. Unamshawishije mtu kutumia kitu ambacho wewe mwenyewe huna imani nacho? Nimejenga hofu ya chanjo hiyo, pengine sio salama kama weupe wanavyotuaminisha!
 
Chinese virus kama anavyotambuliwa na Trump kaikalisha chini Dunia

Hapa kwetu alimchukua mkapa,Burundi kawachukua wale madikteta wastaafu
Dah,Kenya imemchukua papa shindula na waziri Joe Nyaghah.
 
Jana nimeona clips za viongozi wawili wakubwa wa nchi za magharibi "wakichomwa" sindano za chanjo hiyo kimagumashi. Unaona kabisa viongozi wenyewe hawana imani na chanjo hiyo lakini wanahadaa watu wao na ulimwengu mzima kuwa wao wamechanjwa ili raia nao wachanjwe.

Huku ni kuusaliti ubinadamu. Unamshawishije mtu kutumia kitu ambacho wewe mwenyewe huna imani nacho? Nimejenga hofu ya chanjo hiyo, pengine sio salama kama weupe wanavyotuaminisha!
Ni hatari
 
Sisi binadamu ndio tunaharibu hii dunia! Itafika mahali dunia ijitoe kwenye mhimili wako na itokomee kusikojulikana na binadamu afutike katika uso wa dunia.
 
Sisi binadamu ndio tunaharibu hii dunia! Itafika mahali dunia ijitoe kwenye mhimili wako na itokomee kusikojulikana na binadamu afutike katika uso wa dunia.
Una maana mpaka Chato itatoweka maskini bandugu bane abhanu turiruha sana
 
Mkuu Ami, kufa sio jambo baya hata siku moja. Suala ni je, unakufa ukiwa katika uhusiani gani na Mungu wako? Je, unakufa ukiwa umeacha "legacy" ipi katika jamii unamoishi?

“The only thing that walks back from the tomb with the mourners and refuses to be buried is the character of a man"
 
Kwa kweli mimi nangojea kila siku taarifa nzuri,news ni tofauti!... nawaaga kabisa wana JF byeee..tutaonana dunia ya pili,lol, kama ipo
 
Kwa kweli mimi nangojea kila siku taarifa nzuri,news ni tofauti!... nawaaga kabisa wana JF byeee..tutaonana dunia ya pili,lol, kama ipo
Sijui utajificha wapi ambako Mwenyezi Mungu hatokuona. Bora ubaki hapa hapa duniani na ufanye mema na uwache mabaya.
 
Back
Top Bottom