Hoja Fukunyuku: Brand ya mchezaji inaanzia kwa jina lake

Hoja Fukunyuku: Brand ya mchezaji inaanzia kwa jina lake

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Unasikia mwamba anaitwa Rodri baasi. Unajua hii mashine, jina tu linambeba. Mara unasikia Zico, Pele, Garincha, Kaka, Socrates, Romario, Ronaldinho, Bebeto. Jina moja tu umemaliza kazi, unajua unazungumzia nani. Unaweza ukaishi maisha yako yote haujui jina lao lingine na hautakutana na mwingine mwenye jina kama lake.

Sisi sasa, star kabisa ila utasikia Bakari Nondo Mwamnyeto! Utasikia Kibu Denis Prosper, whhhy? Eti Fiston Kalala Mayele! Mara Clatous Chota Chama! Chota ya nini sasa? Kuna Mayele wangapi tunaowajua hadi uone ulazima wa kuongeza Kalala?

Hivi kwa nini tunapenda kuita watu majina matatu ilhali hakuna ulazima wa kufanya hivyo?

Nashauri wachezaji wa kibongo wakishajipata na nyota ikaanza kuwawakia, wasipunguze tu umri, waende pia kwa babu na bibi zao wapewe jina tofauti kabisa la "kilugha". Itawasaidia sana katika branding.
 
Unasikia mwamba anaitwa Rodri baasi. Unajua hii mashine, jina tu linambeba. Mara unasikia Zico, Pele, Garincha, Kaka, Socrates, Romario, Ronaldinho, Bebeto. Jina moja tu umemaliza kazi, unajua unazungumzia nani. Unaweza ukaishi maisha yako yote haujui jina lao lingine na hautakutana na mwingine mwenye jina kama lake.

Sisi sasa, star kabisa ila utasikia Bakari Nondo Mwamnyeto! Utasikia Kibu Denis Prosper, whhhy? Eti Fiston Kalala Mayele! Mara Clatous Chota Chama! Chota ya nini sasa? Kuna Mayele wangapi tunaowajua hadi uone ulazima wa kuongeza Kalala?

Hivi kwa nini tunapenda kuita watu majina matatu ilhali hakuna ulazima wa kufanya hivyo?

Nashauri wachezaji wa kibongo wakishajipata na nyota ikaanza kuwawakia, wasipunguze tu umri, waende pia kwa babu na bibi zao wapewe jina tofauti kabisa la "kilugha". Itawasaidia sana katika branding.
Mwezi mchanga.
 
Kuna mtangazaji wa Azam yeye kila mchezaji anataka amtungie jina mara ukuta wa yeriko, mar sgr, na upuuz mwngi tu

Ilitosha tu kutaja Aucho, Zimbwe jr, Kapombe, Kibur, Ki Aziz, Nzengeli, Baka, n.k
 
Eg
1.Bahanuzi....
2.Nzengeli
3. Mzinze
4. Kiemba
5. Chasambi
6. Bocco

Sijui naandika Nini aloo
 
Eg
1.Bahanuzi....
2.Nzengeli
3. Mzinze
4. Kiemba
5. Chasambi
6. Bocco

Sijui naandika Nini aloo
Nakiri kuna baadhi ya wachezaji wetu majina yamekaa poa kibrand kama hayo uliyoorodhesha.

Ninachosema ukiangalia kama kwa wabrazil, huwa wanatajwa jina moja tu hata katika machapisho ya kimaandishi, hiyo inasaidia branding yao. Nadhani majina yao kamili utayakuta kwenye mikataba yao tu huko.
 
Nakiri kuna baadhi ya wachezaji wetu majina yamekaa poa kibrand kama hayo uliyoorodhesha.

Ninachosema ukiangalia kama kwa wabrazil, huwa wanatajwa jina moja tu hata katika machapisho ya kimaandishi, hiyo inasaidia branding yao. Nadhani majina yao kamili utayakuta kwenye mikataba yao tu huko.
Mkuu,mimi nimekuelewa vizuri sana,
Naunga mkono hoja yako,jina moja ndio linakua brand yako,pia ni rahisi kua maarufu zaidi kuliko majina mengi.
 
Back
Top Bottom