HOJA: Je, umahiri wa lugha ya kigeni ni kipimo cha akili?

HOJA: Je, umahiri wa lugha ya kigeni ni kipimo cha akili?

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Kumekuwa na hoja miongoni mwetu Watanzania kuhusu matumizi ya lugha za kigeni hasa Kiingereza kutumika kama kipimo cha mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili. Je, hoja hii ikoje? na ina ukweli kiasi gani?

HOJA NAZOWAZA ZITHIBITISHE KWAMBA KUJUA KIINGEREZA SIO KUWA NA AKILI NI KAMA IFUATAVO:

- Lugha ya Kiingereza ni njia tu ya mazungumzo kama lugha nyingine yoyote ya hapa nyumbani au ya kimataifa.
  • Lugha unayoimudu haifasili usomi wako.
  • Bila shaka mtu anaezungumza lugha nyingi anachukuliwa kama mwerevu na anayeweza kwa sababu anaweza kuwasiliana na watu wengi lakini hicho sio kipimo kwamba maudhui ya anachowasiliana nao kinaakisi uwezo wake wa akili.
  • Hata katika historia wafalme walikuwa na maafisa ambao walijua kuzungumza zaidi ya lugha moja lakini hawakuwa watu wenye akili kuwazidi wengine.

SASA NI BAHATI MBAYA HAPA KWETU TANZANIA
- Watu wanaozungumza Kiingereza wanachukuliwa kama wajanja,na wenye uwezo wa akili kiasi kwamba wanapewa kipaumbele kwenye mambo mengi hata ajira lakini ukweli ni kwamba umahiri katika Kiingereza au Lugha yoyote anuai hakumaanishi kwamba wewe una akili sana kuwazidi wasiomudu kuzungumza lugha hiyo unayoiwezea kwa ufasaha.

TUKILINDE KISWAHILI ila pia TUSIKIBEZE KIINGEREZA maana tayari kina nguvu na ishakuwa lugha ya dunia.
 
Rais wetu keshasema anajua Kingereza, hebu mtupumzishe kidogo!
 
Tatizo Kiswahili kimejaa maneno ya kijinga kijinga mengi mno kiasi kwamba kinafanya hata waswahili wenyewe tuwe hivyo hivyo.
 
Ni uwezo wa ubongo katika aspects mbalimbali za maisha
Lugha sio aspect ya maisha? Kama aspect mtu akiweza kwa ufasaha kwanini asiwe na akili, yes namaanisha hiyo uliyoitaja.
 
Lugha sio aspect ya maisha?, kama aspect mtu akiweza kwa ufasaha kwanini asiwe na akili, yes namaanisha hiyo uliyoitaja.
Yap inawezekana ndio hii wanaiita linguistic intellegence
 
Kutokana na mfumo wa elimu yetu lazima uonekane unaakili.

Kuijua kufahamu kiingereza kwa ufasaha ina hitajika akili.
 
Kumekuwa na hoja miongoni mwetu watanzania kuhusu matumizi ya lugha za kigeni hasa Kiingereza kutumika kama kipimo cha mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili. Je hoja hii ikoje? na ina ukweli kiasi gani?
Nimepitia baadhi ya list ya wale Watu wa zamani ( hasa Wanafilosophia na Wanasayansi ) ila ndiyo inajulikana kuwa walikuwa Werevu sana na Kugundua 98% walikuwa si tu hawajui Kuzungumza Lugha ya Kiingereza bali pia hawakuipenda (hawakuishobokea ) kama ilivyo sasa.

Kwangu Mimi Kipimo cha Mtu kuwa na Akili ( Mwerevu ) si kujua Kwake Lugha ya Kiingereza bali ni jinsi gani Elimu yake imemsaidia Yeye na wana Jamii wanaomzunguka hasa katika kutatua Changamoto ili kutoa Dira ya Maendeleo na Ufanisi wa Kiujumla.

Hata hivyo pia Kujua ( Kuzijua ) Lugha mbalimbali pia siyo Jambo baya kama una Fursa ya Kuzijua ila zisikufanye ukaanza Kutamba (Kujimwambafai) nazo kwa Watu kwani si tu utakuwa ni Ushamba bali pia utathibitisha Upumbavu wako.
 
Ni kweli. Kuwa na uwezo wa kumudu lugha za kigeni ambazo hukuzaliwa nazo ni ishara ya uwezo mkubwa wa kiakili.

Sio tu Kiingereza, bali lugha yoyote ile.

Maana yake ubongo wako una uwezo mkubwa wa kuchakata taarifa na mawazo katika lugha tofauti tofauti kwa wakati mmoja na ukaweza kuzungumza bila kubabaika ama kuchanganyikiwa.

Ni ufundi. Ukiwa goigoi wa akili huwezi kuzungumza lugha zaidi ya mbili.

Ndio maana wengine mpaka leo hawawezi kutamka Kiswahili kikaeleweka maana bongo zao zimeelemewa na tope zito la lugha mama.
 
Kiingereza kinapatikana shuleni.

Mazingira magumu ya kufundishia kwa shule za serikali zinafanya atakayekijua aonakane ana akili.
 
Nimepitia baadhi ya list ya wale Watu wa zamani ( hasa Wanafilosophia na Wanasayansi ) ila ndiyo inajulikana kuwa walikuwa Werevu sana na Kugundua 98% walikuwa si tu hawajui Kuzungumza Lugha ya Kiingereza bali pia hawakuipenda ( hawakuishobokea ) kama ilivyo sasa...
Actually, kwa mtanzania kuweza kumudu Kiingereza ni kipimo cha uwezo wa juu wa kiakili.

Ndivyo hivyo hivyo, unapomuona mzungu kama Bongozozo anazungumza Kiswahili fasaha, utambue ana uwezo mkubwa wa kumudu lugha (linguistic intelligence).

Kwa mtu goigoi wa akili sio rahisi kumudu lugha ngeni. Ni ngumu sana tena sana.

Ubongo wako unahitaji kuwa sharp kuweza kuchakata lugha mpya usiyoitambua.

Ni cognitive ability ya hali ya juu ya ubongo katika kuchakata mawazo na kuyawakilisha kwa kutumia lugha tofauti tofauti.
 
Inategemea na elimu yako, elimu ya juu Tanzania inafundishwa kwa Kiingereza. Kuanzia A level unaandaliwa kwa insha na mijadala uwezo wa kujenga hoja.

Shahada pia inajumlisha uwezo wa kuandika na kuongea. Unapopata cheti kinathibitisha ukifundishwa kwa Kiingereza na una uwezo wa kuandika na kuongea kwa ufasaha.
 
Inategemea na elimu yako, elimu ya juu Tanzania inafundishwa kwa Kiingereza. Kuanzia A level unaandaliwa kwa insha na mijadala kujenga uwezo wa kutoa hoja.

Shahada pia inajumlisha uwezo wa kuandika na kuongea. Unapopata cheti kinathibitisha ukifundishwa kwa Kiingereza na una uwezo wa kuandika na kuongea kwa ufasaha.
Notes za ubaoni kwa kiingereza lakini ufafanuzi wa mdomoni mwalimu anaufanya kwa Kiswahili.

Katika baadhi ya shule za secondary zenye sera ya "Speak English" unakuta wanafunzi wanaongea kiingereza shuleni lakini wakirudi mtaani ni mwendo wa Kiswahili tu.

Sisi wakati tupo wadogo, baba yetu alikuwa hapendi kabisa tuangalie tamthilia ile ya "La Revancha" lakini akawa anatoa excuse moja kwamba angalieni kwa maana inawapa exposure nzuri katika kukifahamu vema Kiingereza.
 
Notes za ubaoni kwa kiingereza lakini ufafanuzi wa mdomoni mwalimu anaufanya kwa Kiswahili.

Katika baadhi ya shule za secondary zenye sera ya "Speak English" unakuta wanafunzi wanaongea kiingereza shuleni lakini wakirudi mtaani ni mwendo wa kiswahili tu.

Sisi wakati tupo wadogo, baba yetu alikuwa hapendi kabisa tuangalie tamthilia ile ya "La Revancha" lakini akawa anatoa ecuse moja kwamba angalieni kwa maana inawapa exposure nzuri katika kukifahamu vema kiingereza.
Ni kweli unaweza kujua kuandika lakini matamshi yakawa shida. Wanaposema kutema yai si utani. Unaweza kusema bata (butter) wenzako wanasema burrer.
 
Back
Top Bottom