HOJA: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya

HOJA: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Hoja: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya.

Katika Katiba Mpya, Nafikiri kuna umuhimu kufanya mageuzi ya muundo wa utawala na uongozi wa kisiasa nchini. Mbunge wa kuchaguliwa, awe ni Mkuu wa serikali katika Wilaya, aongoze kuanzia baraza la Usalama Wilaya, (Kamati ya ulinzi na Usalama). Vichache hivyo mkuu wa Mkoa apatikane kwa kuchaguliwa na ndie awe mkuu wa serikali ya mkoa. Hili litaondoa mkanganyiko ulipo sasa katika nchi yetu kutumik miundo miwili ya kutawala.

Mfano, Kuna miundo miwili inaongoza serikali katika nchi moja. Kwanza ni kuanzia Mwenyekiti wa Mtaa/Kitongoji ni Mkuu wa serikali ya Kitongoji/Mtaa, Diwani wa Kata ni Mkuu wa Serikali ya kata. Pili ni kuanzia kwa Mkuu wa Wilaya ambae si wa kuchaguliwa anakuwa ndie mkuu wa serikali, wakato huo katika Wilaya hiyo hiyo kuna kuwa na Mbunge ambae ni waluchaguliwa akiongoza watu na kuwakilisha matatizo/mahitaji ya watu lakini hana uwakilishi wa moja kwa moja kwa mkuu wa nchi ambae watu wamemchagua (rais). Badala yake Rais anawakilishwa na Mku wa Wilaya/Mkoa ambae hana uhusiano wa moja kwa moja na wananchi.

Hili linaleta pengo la Wananchi kumfikia Rais wao. Lakini pia linaongeza gharama ya uendeshaji wa serikali kwakuwa kuna serikali mbili ndani ya nchi moja. Yaani kuanzia Mtaa hadi kata kuna serikali y kuchaguliwa na wananchi ambayo inafanya kazi moja kwa moja na Wananchi hao. Pili kuanzia Wilaya kuna serikali mbili moja imechaguliwa na wananchi na inawakilisha wananchi, lakini inakatika uwakilishi wake kwakuwa haimfikii Rais kama mwakili wa wananchi waliomchagua rais, inamegeka na kuelekea Bungeni. Badala yake Rais ametuma mwakilishi wake (kisiasa tu) ambae hana mizizi kwa wananchi na hawafiii wananchi walipo, ana udola tu anaitwa Mkuu wa Wilaya/Mkoa, Kama ni uwakilishi wa rais kiserikali ulitakiwa kukomea kwa Mkurugenzi. Cheo hiki cha udola wa DC na RC kilitakiwa kubebwa na kutumikiwa na Mbunge wa kuchaguliwa kama nchi zingine wanamuita Gavana. Anakuwa na full control ya Polisi Wilaya, chini yake anakuwepo mtendaji ambae ni Mkurugenzi atakayepatikana kwa kuomba kazi hiyo kupitia mchakato wa kiutumishi katika Wilaya/Mkoa.

Kwamantiki ya mabadiliko hayo, Majimbo yatafutwa na badala yake tutakuwa na Mbunge wa Wilaya, Nafasi za DAS na RAS ambazo leo ni za kisiasa tu, zinafutwa. Kazi zao atazifanya Mkurugenzi. Vigezo vya ubunge vitabadilika, viwe kuanzia shahada moja na kuendelea, kuliko iliyo sasa ambapo sifa ya kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika kiswahili tu, Yaani mtu yoyote anaweza kuwa Mbunge, kisha anakwenda kutunga sheria bungeni ambazo sheria hizo, zinataka Mtu anayetakiwa kwenda kuzitumia yaani mwanasheria, lazima asome shahada ya kwanza ya sheria miaka mitatu/minne, kisha aende kusoma shule ya sheria miaka mitatu, akafanye mazoezi kwa vitendo mwaka mmoja ndipo atunukiwe leseni ya kuzutumikia sheria zilizotungwa na mambumbu wanaojua kusoma na kuandika tu kisha wakawa Wabunge wa Tanzania.

Naleta hoja.

Na Yericko Nyerere
 
Mbunge kuwa mkuu wa serikali katika Jimbo au wilaya nadhani sio sawa. Kutapelekea muingiliano wa kimajukumu kati ya serikali na bunge na hatimae bunge kuwa goigoi.
Majukumu ya mbunge yanapaswa yabaki kama yalivyo ambayo ni kuwawakilisha wananchi na kuwasemea changamoto zao bungeni pamoja na kitunga sheria.
Mkuu wa mkoa anapaswa kuchaguliwa na wananchi then kuwe na bunge la mkoa ambalo litaundwa na madiwani wa mkoa.
Mkuu wa mkoa ndie atakuwa mkuu wa serikali katika mkoa na atasimamia shughuli zote za serikali katika mkoa.
Vyeo kama mkuu wa wilaya,katibu tawala,das pamoja na wakurugenzi wa halimashauri vinapaswa kufutwa ili kupunguza gharama na matumizi kwa serikali.
 
Tuwe na majimbo kila Jimbo liwe na bunge lake lipange mambo yake
Mkuu upo sahihi kabisa. Hii Nchi ni kubwa sana, haipendezi hata choo cha shule ya awali ama msingi kauli lazima itoke Dodoma. Leo hata Serikali za Mitaa (Local Government )ime-mezwa na Serikali Kuu (Central Government ), Serikali za Mitaa siku hizi hazina vyazo vya Mapato ya kueleweka. Muda umefika sasa tubadilishe Muundo wa Serikali.
 
Hoja: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya.

Katika Katiba Mpya, Nafikiri kuna umuhimu kufanya mageuzi ya muundo wa utawala na uongozi wa kisiasa nchini. Mbunge wa kuchaguliwa, awe ni Mkuu wa serikali katika Wilaya, aongoze kuanzia baraza la Usalama Wilaya, (Kamati ya ulinzi na Usalama). Vichache hivyo mkuu wa Mkoa apatikane kwa kuchaguliwa na ndie awe mkuu wa serikali ya mkoa. Hili litaondoa mkanganyiko ulipo sasa katika nchi yetu kutumik miundo miwili ya kutawala.

Mfano, Kuna miundo miwili inaongoza serikali katika nchi moja. Kwanza ni kuanzia Mwenyekiti wa Mtaa/Kitongoji ni Mkuu wa serikali ya Kitongoji/Mtaa, Diwani wa Kata ni Mkuu wa Serikali ya kata. Pili ni kuanzia kwa Mkuu wa Wilaya ambae si wa kuchaguliwa anakuwa ndie mkuu wa serikali, wakato huo katika Wilaya hiyo hiyo kuna kuwa na Mbunge ambae ni waluchaguliwa akiongoza watu na kuwakilisha matatizo/mahitaji ya watu lakini hana uwakilishi wa moja kwa moja kwa mkuu wa nchi ambae watu wamemchagua (rais). Badala yake Rais anawakilishwa na Mku wa Wilaya/Mkoa ambae hana uhusiano wa moja kwa moja na wananchi.

Hili linaleta pengo la Wananchi kumfikia Rais wao. Lakini pia linaongeza gharama ya uendeshaji wa serikali kwakuwa kuna serikali mbili ndani ya nchi moja. Yaani kuanzia Mtaa hadi kata kuna serikali y kuchaguliwa na wananchi ambayo inafanya kazi moja kwa moja na Wananchi hao. Pili kuanzia Wilaya kuna serikali mbili moja imechaguliwa na wananchi na inawakilisha wananchi, lakini inakatika uwakilishi wake kwakuwa haimfikii Rais kama mwakili wa wananchi waliomchagua rais, inamegeka na kuelekea Bungeni. Badala yake Rais ametuma mwakilishi wake (kisiasa tu) ambae hana mizizi kwa wananchi na hawafiii wananchi walipo, ana udola tu anaitwa Mkuu wa Wilaya/Mkoa, Kama ni uwakilishi wa rais kiserikali ulitakiwa kukomea kwa Mkurugenzi. Cheo hiki cha udola wa DC na RC kilitakiwa kubebwa na kutumikiwa na Mbunge wa kuchaguliwa kama nchi zingine wanamuita Gavana. Anakuwa na full control ya Polisi Wilaya, chini yake anakuwepo mtendaji ambae ni Mkurugenzi atakayepatikana kwa kuomba kazi hiyo kupitia mchakato wa kiutumishi katika Wilaya/Mkoa.

Kwamantiki ya mabadiliko hayo, Majimbo yatafutwa na badala yake tutakuwa na Mbunge wa Wilaya, Nafasi za DAS na RAS ambazo leo ni za kisiasa tu, zinafutwa. Kazi zao atazifanya Mkurugenzi. Vigezo vya ubunge vitabadilika, viwe kuanzia shahada moja na kuendelea, kuliko iliyo sasa ambapo sifa ya kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika kiswahili tu, Yaani mtu yoyote anaweza kuwa Mbunge, kisha anakwenda kutunga sheria bungeni ambazo sheria hizo, zinataka Mtu anayetakiwa kwenda kuzitumia yaani mwanasheria, lazima asome shahada ya kwanza ya sheria miaka mitatu/minne, kisha aende kusoma shule ya sheria miaka mitatu, akafanye mazoezi kwa vitendo mwaka mmoja ndipo atunukiwe leseni ya kuzutumikia sheria zilizotungwa na mambumbu wanaojua kusoma na kuandika tu kisha wakawa Wabunge wa Tanzania.

Naleta hoja.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2549764
je Wilaya yenye majimbo zaidi ya moja itakuwaje ? ukifuta majimbo unalogwa haraka sana !
 
Hoja dhaifu kwa sababu ukichanganya legislative powers na executional powers kwa pamoja unaiminya democracy.
Pia ukumbuke kuwa rais ni mbunge (Parliament = National assembly + The President).
Ukitaka kugawa mkate mara mbili usiwe wa kwanza kuchagua kipande.
 
Hoja: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya.

Katika Katiba Mpya, Nafikiri kuna umuhimu kufanya mageuzi ya muundo wa utawala na uongozi wa kisiasa nchini. Mbunge wa kuchaguliwa, awe ni Mkuu wa serikali katika Wilaya, aongoze kuanzia baraza la Usalama Wilaya, (Kamati ya ulinzi na Usalama). Vichache hivyo mkuu wa Mkoa apatikane kwa kuchaguliwa na ndie awe mkuu wa serikali ya mkoa. Hili litaondoa mkanganyiko ulipo sasa katika nchi yetu kutumik miundo miwili ya kutawala.

Mfano, Kuna miundo miwili inaongoza serikali katika nchi moja. Kwanza ni kuanzia Mwenyekiti wa Mtaa/Kitongoji ni Mkuu wa serikali ya Kitongoji/Mtaa, Diwani wa Kata ni Mkuu wa Serikali ya kata. Pili ni kuanzia kwa Mkuu wa Wilaya ambae si wa kuchaguliwa anakuwa ndie mkuu wa serikali, wakato huo katika Wilaya hiyo hiyo kuna kuwa na Mbunge ambae ni waluchaguliwa akiongoza watu na kuwakilisha matatizo/mahitaji ya watu lakini hana uwakilishi wa moja kwa moja kwa mkuu wa nchi ambae watu wamemchagua (rais). Badala yake Rais anawakilishwa na Mku wa Wilaya/Mkoa ambae hana uhusiano wa moja kwa moja na wananchi.

Hili linaleta pengo la Wananchi kumfikia Rais wao. Lakini pia linaongeza gharama ya uendeshaji wa serikali kwakuwa kuna serikali mbili ndani ya nchi moja. Yaani kuanzia Mtaa hadi kata kuna serikali y kuchaguliwa na wananchi ambayo inafanya kazi moja kwa moja na Wananchi hao. Pili kuanzia Wilaya kuna serikali mbili moja imechaguliwa na wananchi na inawakilisha wananchi, lakini inakatika uwakilishi wake kwakuwa haimfikii Rais kama mwakili wa wananchi waliomchagua rais, inamegeka na kuelekea Bungeni. Badala yake Rais ametuma mwakilishi wake (kisiasa tu) ambae hana mizizi kwa wananchi na hawafiii wananchi walipo, ana udola tu anaitwa Mkuu wa Wilaya/Mkoa, Kama ni uwakilishi wa rais kiserikali ulitakiwa kukomea kwa Mkurugenzi. Cheo hiki cha udola wa DC na RC kilitakiwa kubebwa na kutumikiwa na Mbunge wa kuchaguliwa kama nchi zingine wanamuita Gavana. Anakuwa na full control ya Polisi Wilaya, chini yake anakuwepo mtendaji ambae ni Mkurugenzi atakayepatikana kwa kuomba kazi hiyo kupitia mchakato wa kiutumishi katika Wilaya/Mkoa.

Kwamantiki ya mabadiliko hayo, Majimbo yatafutwa na badala yake tutakuwa na Mbunge wa Wilaya, Nafasi za DAS na RAS ambazo leo ni za kisiasa tu, zinafutwa. Kazi zao atazifanya Mkurugenzi. Vigezo vya ubunge vitabadilika, viwe kuanzia shahada moja na kuendelea, kuliko iliyo sasa ambapo sifa ya kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika kiswahili tu, Yaani mtu yoyote anaweza kuwa Mbunge, kisha anakwenda kutunga sheria bungeni ambazo sheria hizo, zinataka Mtu anayetakiwa kwenda kuzitumia yaani mwanasheria, lazima asome shahada ya kwanza ya sheria miaka mitatu/minne, kisha aende kusoma shule ya sheria miaka mitatu, akafanye mazoezi kwa vitendo mwaka mmoja ndipo atunukiwe leseni ya kuzutumikia sheria zilizotungwa na mambumbu wanaojua kusoma na kuandika tu kisha wakawa Wabunge wa Tanzania.

Naleta hoja.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2549764
Kweli aiseee, Gavana( Mbunge' anatosha.. ambaye kachaguliwa na wananchi wa mkoa husika na aliyesoma kuanzia degree etc..kama Kenya...
 
Uko sahihi 100%
Mbunge kuwa mkuu wa serikali katika Jimbo au wilaya nadhani sio sawa. Kutapelekea muingiliano wa kimajukumu kati ya serikali na bunge na hatimae bunge kuwa goigoi.
Majukumu ya mbunge yanapaswa yabaki kama yalivyo ambayo ni kuwawakilisha wananchi na kuwasemea changamoto zao bungeni pamoja na kitunga sheria.
Mkuu wa mkoa anapaswa kuchaguliwa na wananchi then kuwe na bunge la mkoa ambalo litaundwa na madiwani wa mkoa.
Mkuu wa mkoa ndie atakuwa mkuu wa serikali katika mkoa na atasimamia shughuli zote za serikali katika mkoa.
Vyeo kama mkuu wa wilaya,katibu tawala,das pamoja na wakurugenzi wa halimashauri vinapaswa kufutwa ili kupunguza gharama na matumizi kwa serikali.
 
Katika Katiba Mpya, Nafikiri kuna umuhimu kufanya mageuzi ya muundo wa utawala na uongozi wa kisiasa nchini. Mbunge wa kuchaguliwa, awe ni Mkuu wa serikali katika Wilaya, aongoze kuanzia baraza la Usalama Wilaya, (Kamati ya ulinzi na Usalama). Vichache hivyo mkuu wa Mkoa apatikane kwa kuchaguliwa na ndie awe mkuu wa serikali ya mkoa. Hili litaondoa mkanganyiko ulipo sasa katika nchi yetu kutumik miundo miwili ya kutawala.
Nakazia

Iwe katika Mkoa, kama RC anaweza kuzungukia Mkoa mzima na kushughulikia kero, mbunge anashindwaje kuzungukia mkoa kwa miaka mitano

Ifike wakati wananchi tuchague watu wa kufanya nao kazi na kuwafukuza sisi wenyewe badala ya kuletewa
 
U
Hoja: Mbunge awe Mkuu wa Serikali katika Wilaya.

Katika Katiba Mpya, Nafikiri kuna umuhimu kufanya mageuzi ya muundo wa utawala na uongozi wa kisiasa nchini. Mbunge wa kuchaguliwa, awe ni Mkuu wa serikali katika Wilaya, aongoze kuanzia baraza la Usalama Wilaya, (Kamati ya ulinzi na Usalama). Vichache hivyo mkuu wa Mkoa apatikane kwa kuchaguliwa na ndie awe mkuu wa serikali ya mkoa. Hili litaondoa mkanganyiko ulipo sasa katika nchi yetu kutumik miundo miwili ya kutawala.

Mfano, Kuna miundo miwili inaongoza serikali katika nchi moja. Kwanza ni kuanzia Mwenyekiti wa Mtaa/Kitongoji ni Mkuu wa serikali ya Kitongoji/Mtaa, Diwani wa Kata ni Mkuu wa Serikali ya kata. Pili ni kuanzia kwa Mkuu wa Wilaya ambae si wa kuchaguliwa anakuwa ndie mkuu wa serikali, wakato huo katika Wilaya hiyo hiyo kuna kuwa na Mbunge ambae ni waluchaguliwa akiongoza watu na kuwakilisha matatizo/mahitaji ya watu lakini hana uwakilishi wa moja kwa moja kwa mkuu wa nchi ambae watu wamemchagua (rais). Badala yake Rais anawakilishwa na Mku wa Wilaya/Mkoa ambae hana uhusiano wa moja kwa moja na wananchi.

Hili linaleta pengo la Wananchi kumfikia Rais wao. Lakini pia linaongeza gharama ya uendeshaji wa serikali kwakuwa kuna serikali mbili ndani ya nchi moja. Yaani kuanzia Mtaa hadi kata kuna serikali y kuchaguliwa na wananchi ambayo inafanya kazi moja kwa moja na Wananchi hao. Pili kuanzia Wilaya kuna serikali mbili moja imechaguliwa na wananchi na inawakilisha wananchi, lakini inakatika uwakilishi wake kwakuwa haimfikii Rais kama mwakili wa wananchi waliomchagua rais, inamegeka na kuelekea Bungeni. Badala yake Rais ametuma mwakilishi wake (kisiasa tu) ambae hana mizizi kwa wananchi na hawafiii wananchi walipo, ana udola tu anaitwa Mkuu wa Wilaya/Mkoa, Kama ni uwakilishi wa rais kiserikali ulitakiwa kukomea kwa Mkurugenzi. Cheo hiki cha udola wa DC na RC kilitakiwa kubebwa na kutumikiwa na Mbunge wa kuchaguliwa kama nchi zingine wanamuita Gavana. Anakuwa na full control ya Polisi Wilaya, chini yake anakuwepo mtendaji ambae ni Mkurugenzi atakayepatikana kwa kuomba kazi hiyo kupitia mchakato wa kiutumishi katika Wilaya/Mkoa.

Kwamantiki ya mabadiliko hayo, Majimbo yatafutwa na badala yake tutakuwa na Mbunge wa Wilaya, Nafasi za DAS na RAS ambazo leo ni za kisiasa tu, zinafutwa. Kazi zao atazifanya Mkurugenzi. Vigezo vya ubunge vitabadilika, viwe kuanzia shahada moja na kuendelea, kuliko iliyo sasa ambapo sifa ya kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika kiswahili tu, Yaani mtu yoyote anaweza kuwa Mbunge, kisha anakwenda kutunga sheria bungeni ambazo sheria hizo, zinataka Mtu anayetakiwa kwenda kuzitumia yaani mwanasheria, lazima asome shahada ya kwanza ya sheria miaka mitatu/minne, kisha aende kusoma shule ya sheria miaka mitatu, akafanye mazoezi kwa vitendo mwaka mmoja ndipo atunukiwe leseni ya kuzutumikia sheria zilizotungwa na mambumbu wanaojua kusoma na kuandika tu kisha wakawa Wabunge wa Tanzania.

Naleta hoja.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2549764
Ulikuwa unamaanisha hawa wabunge kama mzee Mdee, Gwajima, Msukuma?

Ukishakuwa na huo mfumo, nani atamsimamia mwenzie?

Wabunge wabakie kama wabunge, wakuu wa wilaya wafutwe kabisa, hawana maana yoyote.
 
Yaani mtu yoyote anaweza kuwa Mbunge, kisha anakwenda kutunga sheria bungeni ambazo sheria hizo, zinataka Mtu anayetakiwa kwenda kuzitumia yaani mwanasheria, lazima asome shahada ya kwanza ya sheria miaka mitatu/minne, kisha aende kusoma shule ya sheria miaka mitatu, akafanye mazoezi kwa vitendo mwaka mmoja ndipo atunukiwe leseni ya kuzutumikia sheria zilizotungwa na mambumbu wanaojua kusoma na kuandika tu kisha wakawa Wabunge wa Tanzania.
Uko Sahihi; na inafikirisha sana.
 
Kiongozi Nyerere,hebu pitia Katiba hii chakavu,soma kazi za Mbunge,na mgawanyo wa majukumu ya Mhimili(pillars) hizi tatu(3) za dola,then urudi tena

Labda ungesema DC ambaye ndie Mkuu wa Serikali,katika wilaya awe anachaguliwa na wananchi na apewe majukumu makubwa zaidi kikatiba
 
Back
Top Bottom