Hoja: Sio kila anayelia na kuumia anastahili huruma, ni mavuno yake hayo

Hoja: Sio kila anayelia na kuumia anastahili huruma, ni mavuno yake hayo

Kibosho1

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2017
Posts
2,621
Reaction score
4,293
Katika maisha kuna hali tofauti tofauti. Hali zingine ni kutokamilika kwetu, au kujisahau kwetu.

Kwa tulipofikia sasa si kila mtu anastahili kuonewa huruma na kusaidiwa na jamii. Wakati mwingine ni mavuno ya alichopanda. Hebu fikiria hii;

1. UHALIFU
Ulikuwa mwizi, umewaibia watu sana, umewapa hasara sana, sasa ukakamatwa na kuvunjwa mguu au mkono. Ama umelogwa, unateseka, sasa unarudi mtaani kutafuta huruma za jamii(kuomba omba), nani akusaidie sasa, unalaumu jamii kwa kukutenga?!

2. KWENYE JAMII
Ulikuwa unaringa kipindi una mafanikio, labda kazi nzuri, kipato cha uhakika, marafiki wa level zako. Sasa maisha yamebadilika umerudi chini, unataka wale uliowadharau wawe pamoja na wewe. Wanapo kukataa unawalaumu hawana upendo, wanafiki. Mbona mwanzo hukuwaona hivyo?

3. STAREHE
wewe ulikuwa mla bata, pedeshee, mutu ya watoto, umewagonga wewe mpaka wamekuachia magonjwa ya zinaa. Sasa umeanza kunyauka wamekukimbia, umefilisika sababu ya matibabu sasa unataka uende sawa na wastaarabu nani akukubali? Kula mavuno yako mwenyewe.

4. SIASA
Mnafanya uchaguzi, wananchi mmechuja sera, mmeambiwa chama hiki hakifai, sera zao zile zile, tabia zao zile zile, mkachagua hivyo hivyo. Sasa mavuno yenu ni tozo ya miamala sa simu, miamala ya benki, kodi ya jengo kupitia LUKU n.k

Mifano ni mingi, ukitafakari makosa mengi ya mwanadamu zaidi ya 60% mengine yana epukika. Kabla ya kufanya jambo lolote fikiria na matokeo yake au mwishowe.

Kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Ndio maana siamini kabisa kuhusu kila jambo ni mipango ya Mungu, au baada ya kukosa unasingizia ni shetani kanipitia kumbe ni mavuno yako tu.
 
Nakumbuka kipindi cha tumbuatumbua ya kipindi cha Magu, ndo nilikuwa nahamia idara fulani, kuna jamaa alikuwa ndio kiongozi wetu wa section alipigwa chini kwa sababu ya vyeti feki.

Kuna watu wakasema msimwonee huruma huyo, acha yamkute kwani aliwahi kuwa mwiba mchungu kwa wafanyakazi wenzie, istoshe kipindi hicho mkurugenzi alikuwa kabila lake..

Nikasema kweli Karma inaishi..
 
Nakumbuka kipindi cha tumbuatumbua ya kipindi cha Magu, ndo nilikuwa nahamia idara fulani, kuna jamaa alikuwa ndio kiongozi wetu wa section alipigwa chini kwa sababu ya vyeti feki.

Kuna watu wakasema msimwonee huruma huyo, acha yamkute kwani aliwahi kuwa mwiba mchungu kwa wafanyakazi wenzie, istoshe kipindi hicho mkurugenzi alikuwa kabila lake..

Nikasema kweli Karma inaishi..
Hapo utakuta alimlaumu tu kumbe tatizo ni mwenyewe
 
Sasa, toka lini wananchi wakachagua viongozi? Sisi wananchi hatujawahi kuchagua viongozi, tunaletewa tu.. na hayo matozo tumeletewa tu sio matokeo ya matendo yetu!
 
Karma is cause and effect.

Amin kwamba unapokutwa na maswaibu sababu ni mbili
1. Ni ngazi ya kupanda level nyingine
2. Ni malipo ya uliyowahi kuwatendea wengine.
 
Katika maisha kuna hali tofauti tofauti. Hali zingine ni kutokamilika kwetu,au kujisahau kwetu.
Kwa tulipofikia sasa si kila mtu anastahili kuonewa huruma na kusaidiwa na jamii. Wakati mwingine ni mavuno ya alichopanda. Hebu fikiria hii.

1.UHALIFU
Ulikuwa mwizi,umewaibia watu sana,umewapa hasara sana sasa ukakamatwa na kuvunjwa mguu au mkono au umelogwa,unateseka sasa unarudi mtaani kutafuta huruma za jamii(kuomba omba) nani akusaidie sasa,unalaumu jamii kwa kukutenga!?

2. KWENYE JAMII Ulikuwa unaringa kipindi una mafanikio,labda kazi nzuri,kipato cha uhakika, marafiki wa level zako. sasa maisha yamebadilika urudi chini,unataka wale uliowadharau wawe pamoja na wewe,wanapokukataa unawalaumi hawana upendo,wanafiki. Mbona mwanzo hukuwaona hivyo?

3. STAREHE: wewe ulikuwa mla bata,pedeshee,mutu ya watoto umewagonga weweee...mpaka wamekuachia magonjwa ya zinaa,sasa umeanza kunyauka wamekukimbia,umefilisika sababu ya matibabu sasa unataka uende sawa na wastaarabu nani akukubali? Kula mavuno yako mwenyewe.

4. SIASA
Mnafanya uchaguzi, wananchi mmechuja sera,mumeambiwa chama hiki hakifai,sera zao zile zile, tabia zao zile zile mkachagua hivyo hivyo.
Sasa mavuno yenu ni tozo ya miamala sa simu, miamala ya benk kodi ya jengo kupitia LUKU n.k

Mifano ni mingi, ukitafakari makosa mengi ya mwanadamu zaidi ya 60% mengine yana epukika. Kabla ya kufanya jambo lolote fikiria na matokeo yake au mwishowe.

KILE APANDACHO MTU NDICHO ATAKACHOVUNA.
Ndio maana siamini kabisa kuhusu kila jambo ni mipango ya Mungu,au baada ya kukosa unasingizia ni Shetani kanipitia kumbe ni mavuno yako tu.
Basi hakuna anayestahili huruma.

Unajua makosa ya kibinadamu yanayopelekea watu kulia na kuumia ni mengi mno.

Hata mtoto anapozaliwa mlemavu kuna uwezekano mkubwa mama hakufuata njia za kisayansi za kukuza viungo vya mtoto akiwa tumboni, mfano matumizi ya folic acid. Sasa huyu mtoto akizaliwa miguu imeungana kwa mfano, bado hastahili kuhurumiwa?

Nataka kusema hivi, kama unaweza kumhurumia na kumsaidia mtu, ikiwa huo msaada haukuumizi wewe basi msaidie tu bila kujali sababu ulizotoa hapo juu. Makosa tumeumbiwa na kama wewe huna kosa umewahi fanya maishani basi umepungukiwa ubinadamu, umeukaribia utakatifu.
 
Leo analia Makonda kule Sabaya maisha anayekupiga leo huenda kesho ukam kojolea
 
Basi hakuna anayestahili huruma.

Unajua makosa ya kibinadamu yanayopelekea watu kulia na kuumia ni mengi mno.

Hata mtoto anapozaliwa mlemavu kuna uwezekano mkubwa mama hakufuata njia za kisayansi za kukuza viungo vya mtoto akiwa tumboni, mfano matumizi ya folic acid. Sasa huyu mtoto akizaliwa miguu imeungana kwa mfano, bado hastahili kuhurumiwa?

Nataka kusema hivi, kama unaweza kumhurumia na kumsaidia mtu, ikiwa huo msaada haukuumizi wewe basi msaidie tu bila kujali sababu ulizotoa hapo juu. Makosa tumeumbiwa na kama wewe huna kosa umewahi fanya maishani basi umepungukiwa ubinadamu, umeukaribia utakatifu.
Huyo mtoto kasababishiwa,hakulima yeye. Hayo ni mavuno ya mamake.
 
Sasa, toka lini wananchi wakachagua viongozi? Sisi wananchi hatujawahi kuchagua viongozi, tunaletewa tu.. na hayo matozo tumeletewa tu sio matokeo ya matendo yetu!
Shambani kwako ukiona magugu yanaota utayaacha? Kama ukiavha umeyapenda, kwenye mavuno utalia tu
 
Huyo mtoto kasababishiwa,hakulima yeye. Hayo ni mavuno ya mamake.
Katika hoja yako ninachosisitiza ni kuhurumiana. Ni kweli mtoto hakulima yeye, sasa je, tuachane nae kwa vile ni mavuno ya mamake?

Kimsingi tukianza kuangalia mkulima na mvunaji hata hoja ulizotoa zinakosa mashiko;

Mfano 1. UHALIFU: waharifu wengi wanasababishiwa, tunaweka system inashindwa kutumikia watu, watu wanakuwa waharifu.

2. KWENYE JAMII: Hapa mapungufu tunayoonesha tumesababishiwa kwa kiasi flani na familia zetu au dini zetu kwa kushindwa kutulea kimaadili

3. STAREHE: Ni sehemu ya maisha, kwa asili binadamu ni mnyama anayependa starehe, ndio maana unaona tunagundua vitu na mambo mbalimbali ya kutustarehesha; mziki, magari, godoro n.k.

Sasa ninapoibua mchepuko Ni sehemu ya kuisaka starehe, nikipata magonjwa nakuwa nimesababishiwa, huyo mrembo alijua ana ugonjwa kwanini hakuniambia?!,,,amenisababishia.

4. SIASA: Sisi tumewachagua baada ya kuwaelewa na kuwaamini. Hata tozo tunatoa kwa moyo wote ili tufikie maendeleo tunayoyataka. Sasa wao wanakengeuka, wanafuja mali ya umma.

Hawa watu wanatusababishia hali ngumu.,,,,kwahiyo tumesababishiwa.

TUHURUMIANE TU, matatizo mengi tunasababishiwa,,,,machache sana tunasababisha wenyewe.
 
Katika hoja yako ninachosisitiza ni kuhurumiana. Ni kweli mtoto hakulima yeye, sasa je, tuachane nae kwa vile ni mavuno ya mamake?

Kimsingi tukianza kuangalia mkulima na mvunaji hata hoja ulizotoa zinakosa mashiko;

Mfano 1. UHALIFU: waharifu wengi wanasababishiwa, tunaweka system inashindwa kutumikia watu, watu wanakuwa waharifu.

2. KWENYE JAMII: Hapa mapungufu tunayoonesha tumesababishiwa kwa kiasi flani na familia zetu au dini zetu kwa kushindwa kutulea kimaadili

3. STAREHE: Ni sehemu ya maisha, kwa asili binadamu ni mnyama anayependa starehe, ndio maana unaona tunagundua vitu na mambo mbalimbali ya kutustarehesha; mziki, magari, godoro n.k.

Sasa ninapoibua mchepuko Ni sehemu ya kuisaka starehe, nikipata magonjwa nakuwa nimesababishiwa, huyo mrembo alijua ana ugonjwa kwanini hakuniambia?!,,,amenisababishia.

4. SIASA: Sisi tumewachagua baada ya kuwaelewa na kuwaamini. Hata tozo tunatoa kwa moyo wote ili tufikie maendeleo tunayoyataka. Sasa wao wanakengeuka, wanafuja mali ya umma.

Hawa watu wanatusababishia hali ngumu.,,,,kwahiyo tumesababishiwa.

TUHURUMIANE TU, matatizo mengi tunasababishiwa,,,,machache sana tunasababisha wenyewe.
Mkuu nimekuelewa ila sikuzungumza general,kuna matukio mengine ni ya kusababishiwa. Mfano unaendesha gari, unafuata sheria zote za rodi lakini anatokea mlevi anakugonga kwa nyuma labda gari inapinduka unaumia,hapo huruma lazma sababu hukupanda ww. Ila hoja zako kuhusu starehe hazina mashiko sababu ungetazama athari kwanza kabla ya kuvuta mchepuko wako. Kwanini hukupima nae kama ana magonjwa? Huoni kama unalima ww,na utavuna tu mabaya?
 
KILE APANDACHO MTU NDICHO ATAKACHOVUNA
Kuna muda huwa sijihurumia Kwa magumu nipitiayo,nalia Kisha najisemea nimevuna nilichopanda.....Kila kitu kilichonitokea maishani ni ujinga wangu😥🤲
 
Basi hakuna anayestahili huruma.

Unajua makosa ya kibinadamu yanayopelekea watu kulia na kuumia ni mengi mno.

Hata mtoto anapozaliwa mlemavu kuna uwezekano mkubwa mama hakufuata njia za kisayansi za kukuza viungo vya mtoto akiwa tumboni, mfano matumizi ya folic acid. Sasa huyu mtoto akizaliwa miguu imeungana kwa mfano, bado hastahili kuhurumiwa?

Nataka kusema hivi, kama unaweza kumhurumia na kumsaidia mtu, ikiwa huo msaada haukuumizi wewe basi msaidie tu bila kujali sababu ulizotoa hapo juu. Makosa tumeumbiwa na kama wewe huna kosa umewahi fanya maishani basi umepungukiwa ubinadamu, umeukaribia utakatifu.
Kama vile nataka kukuelewa ....ila kuna majitu...linakutesaaa ukiweza kuvumilia kitambo sio kirefu unaanza kuliona linavoteseeeekaaaaa
 
Back
Top Bottom