Hoja: Sio kila anayelia na kuumia anastahili huruma, ni mavuno yake hayo

Hoja: Sio kila anayelia na kuumia anastahili huruma, ni mavuno yake hayo

Katika maisha kuna hali tofauti tofauti. Hali zingine ni kutokamilika kwetu,au kujisahau kwetu.
Kwa tulipofikia sasa si kila mtu anastahili kuonewa huruma na kusaidiwa na jamii. Wakati mwingine ni mavuno ya alichopanda. Hebu fikiria hii.

1.UHALIFU
Ulikuwa mwizi,umewaibia watu sana,umewapa hasara sana sasa ukakamatwa na kuvunjwa mguu au mkono au umelogwa,unateseka sasa unarudi mtaani kutafuta huruma za jamii(kuomba omba) nani akusaidie sasa,unalaumu jamii kwa kukutenga!?

2. KWENYE JAMII Ulikuwa unaringa kipindi una mafanikio,labda kazi nzuri,kipato cha uhakika, marafiki wa level zako. sasa maisha yamebadilika urudi chini,unataka wale uliowadharau wawe pamoja na wewe,wanapokukataa unawalaumi hawana upendo,wanafiki. Mbona mwanzo hukuwaona hivyo?

3. STAREHE: wewe ulikuwa mla bata,pedeshee,mutu ya watoto umewagonga weweee...mpaka wamekuachia magonjwa ya zinaa,sasa umeanza kunyauka wamekukimbia,umefilisika sababu ya matibabu sasa unataka uende sawa na wastaarabu nani akukubali? Kula mavuno yako mwenyewe.

4. SIASA
Mnafanya uchaguzi, wananchi mmechuja sera,mumeambiwa chama hiki hakifai,sera zao zile zile, tabia zao zile zile mkachagua hivyo hivyo.
Sasa mavuno yenu ni tozo ya miamala sa simu, miamala ya benk kodi ya jengo kupitia LUKU n.k

Mifano ni mingi, ukitafakari makosa mengi ya mwanadamu zaidi ya 60% mengine yana epukika. Kabla ya kufanya jambo lolote fikiria na matokeo yake au mwishowe.

KILE APANDACHO MTU NDICHO ATAKACHOVUNA.
Ndio maana siamini kabisa kuhusu kila jambo ni mipango ya Mungu,au baada ya kukosa unasingizia ni Shetani kanipitia kumbe ni mavuno yako tu.
True say. Nimeona sana wapo watu wanateseka na maisha yao yamejaa majonzi unaweza fikiri Mungu amewasahau ila kumbe wamefanya mambo mabaya sanà ktk jamii wameibia watu, wamedhulumu watu leo wanavuna walicho panda. Miaka kadhaa bwana mmoja akiwa ananafasi mahali fulani alitumia nafasi yake kudhalilisha watu na kuwa dharau hakujuwa ipo siku yaweza kuwa yeye pia akadhalilika. Siku moja akajikuta dampo na wale aliwadharau wakiwa na mandinga yao mtaani yeye akisaidia waoshea. Mimi napenda kusema hata kama unajiona wewe ni Rais ndio cheo chako jaribu kuwathamini watu na hali zao. Wapo viongozi mnao waona leo ambao wanajeuri na dhihaka kwa wa Tz watakuwa hawana kitu yani hata wakikwapua hazina yote ipo siku miaka kumi ijayo hawatokuwa na kitu why? Utajijibu mwenyewe.
 
Ndio maana siamini kabisa kuhusu kila jambo ni mipango ya Mungu
Yesu mwenyewe alikua ahamini km atapigiliwa misumali msalabani ndio maana alimlilia Mungu-Mwenye Enzi 'Baba ikiwezekana kikombe hiki kini....' acha kabisa unaambiwa shetani alipogombana na Mungu huko mbinguni aliondoka na ⅓ ya kundi la malaika na hio ⅓ yote ilitupwa pamoja nae duniani

Jitafakari
 
Mkuu nimekuelewa ila sikuzungumza general,kuna matukio mengine ni ya kusababishiwa. Mfano unaendesha gari, unafuata sheria zote za rodi lakini anatokea mlevi anakugonga kwa nyuma labda gari inapinduka unaumia,hapo huruma lazma sababu hukupanda ww. Ila hoja zako kuhusu starehe hazina mashiko sababu ungetazama athari kwanza kabla ya kuvuta mchepuko wako. Kwanini hukupima nae kama ana magonjwa? Huoni kama unalima ww,na utavuna tu mabaya?
Hiyo ya starehe za mchepuko nilichomekea tu mkuu, binafsi nimeielewa vizuri hoja yako [emoji1666]
 
Mnahangaika sana na maisha!
Wakati nahangaika na maisha kama ninyi, prayer item yangu ilikuwa ndefu sana.
Ningeweza kuomba hata kwa masaa mawili.
Lakini tangu niache kuhangaika na maisha, siku hizi nikiomba sana dk tano nyingi. Naomba kumshukuru Mungu kuniamsha salama na kumuomba anijalie siku njema. Pia nafunga siku moja kwa wiki kwa ajili ya kutubu dhambi zangu... Baasi.
 
True say. Nimeona sana wapo watu wanateseka na maisha yao yamejaa majonzi unaweza fikiri Mungu amewasahau ila kumbe wamefanya mambo mabaya sanà ktk jamii wameibia watu, wamedhulumu watu leo wanavuna walicho panda. Miaka kadhaa bwana mmoja akiwa ananafasi mahali fulani alitumia nafasi yake kudhalilisha watu na kuwa dharau hakujuwa ipo siku yaweza kuwa yeye pia akadhalilika. Siku moja akajikuta dampo na wale aliwadharau wakiwa na mandinga yao mtaani yeye akisaidia waoshea. Mimi napenda kusema hata kama unajiona wewe ni Rais ndio cheo chako jaribu kuwathamini watu na hali zao. Wapo viongozi mnao waona leo ambao wanajeuri na dhihaka kwa wa Tz watakuwa hawana kitu yani hata wakikwapua hazina yote ipo siku miaka kumi ijayo hawatokuwa na kitu why? Utajijibu mwenyewe.
Kweli kabisa,lazma uvune tu.
 
Yesu mwenyewe alikua ahamini km atapigiliwa misumali msalabani ndio maana alimlilia Mungu-Mwenye Enzi 'Baba ikiwezekana kikombe hiki kini....' acha kabisa unaambiwa shetani alipogombana na Mungu huko mbinguni aliondoka na ⅓ ya kundi la malaika na hio ⅓ yote ilitupwa pamoja nae duniani

Jitafakari
Ni wapi uliona Shetani anamlazimisha mtu,kufanya mambo mabaya? Nipe ushahidi kama upo
 
Back
Top Bottom